VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mwigulu Nchemba ni mwanasiasa wa ajabu sana. Hajali. Hasikii.Haelewi. Anachojali yeye ni kujijenga(pia kujibomoa) katika siasa.Anataka kuaminika kama dawa pekee ya kuwadhibiti CHADEMA kati ya makada wote wa CCM.
Ndiyo maana anafanya anayoyafanya. Mwigulu Nchemba anaamini kuwa anaungwa mkono na Mwenyekiti wa chama pamoja na viongozi wengine waandamizi wa CCM Taifa. Ndiyo maana anaweza hata kubuni 'mijivazi' yake hata inayokwenda kinyume na sare rasmi za chama.Anaweza asiwe sahihi.Aweza kuwa anapotoka. Mwigulu amelewa sifa. Anapepesuka. Kwa wasio makini kisiasa na wanaomtii Mwigulu Nchemba kwa kila alisemalo wataponzeka.
Watasawajika kisiasa na kichama. Jana tu, kijana Mtela Mwampamba ameingia mkenge wa Mwigulu.Amekurupuka na habari za kizushi kuwa eti Mgombea wa Udiwani wa Elerai wa CHADEMA amejiunga CCM. Sasa kijana Mtela Mwampamba HAAMINIKI TENA. Hapa JF ameshapata 'zawadi' yake.
Bado chamani.Bado uraiani.Bado maishani. Bado akilini mwake. Bado atakavyomuona kivingine Mwigulu Nchemba. Bado. Ni wakati sasa wanachama wenzangu wa CCM kuchuja kila kauli na vitendo vya viongozi wetu kama Mwigulu Nchemba ili tuwe huru.Tuwe makini. Kama tunamtegemea Mwigulu Nchemba na siasa zake za aina hii ionekanayo,hatutakuwa makini. Tutakimbiwa.
Siasa iwe ni hoja na si vihoja. Vinginevyo, Mwigulu Nchemba ataponza wengi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Ndiyo maana anafanya anayoyafanya. Mwigulu Nchemba anaamini kuwa anaungwa mkono na Mwenyekiti wa chama pamoja na viongozi wengine waandamizi wa CCM Taifa. Ndiyo maana anaweza hata kubuni 'mijivazi' yake hata inayokwenda kinyume na sare rasmi za chama.Anaweza asiwe sahihi.Aweza kuwa anapotoka. Mwigulu amelewa sifa. Anapepesuka. Kwa wasio makini kisiasa na wanaomtii Mwigulu Nchemba kwa kila alisemalo wataponzeka.
Watasawajika kisiasa na kichama. Jana tu, kijana Mtela Mwampamba ameingia mkenge wa Mwigulu.Amekurupuka na habari za kizushi kuwa eti Mgombea wa Udiwani wa Elerai wa CHADEMA amejiunga CCM. Sasa kijana Mtela Mwampamba HAAMINIKI TENA. Hapa JF ameshapata 'zawadi' yake.
Bado chamani.Bado uraiani.Bado maishani. Bado akilini mwake. Bado atakavyomuona kivingine Mwigulu Nchemba. Bado. Ni wakati sasa wanachama wenzangu wa CCM kuchuja kila kauli na vitendo vya viongozi wetu kama Mwigulu Nchemba ili tuwe huru.Tuwe makini. Kama tunamtegemea Mwigulu Nchemba na siasa zake za aina hii ionekanayo,hatutakuwa makini. Tutakimbiwa.
Siasa iwe ni hoja na si vihoja. Vinginevyo, Mwigulu Nchemba ataponza wengi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam