Mwigulu atawaponza wengi!

Mwigulu atawaponza wengi!

hz porojo peleka huko kwa wanawake wenzio


mkuu kumbuka hata mama yako pia ni mwanamke...so usuwadharau sana wamama. waambie mabwana zako wa lumumba wakufundishe uachane na fikra za kibaguzi.
 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mwigulu Nchemba ni mwanasiasa wa ajabu sana. Hajali. Hasikii.Haelewi. Anachojali yeye ni kujijenga(pia kujibomoa) katika siasa.Anataka kuaminika kama dawa pekee ya kuwadhibiti CHADEMA kati ya makada wote wa CCM.

Ndiyo maana anafanya anayoyafanya. Mwigulu Nchemba anaamini kuwa anaungwa mkono na Mwenyekiti wa chama pamoja na viongozi wengine waandamizi wa CCM Taifa. Ndiyo maana anaweza hata kubuni 'mijivazi' yake hata inayokwenda kinyume na sare rasmi za chama.Anaweza asiwe sahihi.Aweza kuwa anapotoka. Mwigulu amelewa sifa. Anapepesuka. Kwa wasio makini kisiasa na wanaomtii Mwigulu Nchemba kwa kila alisemalo wataponzeka.

Watasawajika kisiasa na kichama. Jana tu, kijana Mtela Mwampamba ameingia mkenge wa Mwigulu.Amekurupuka na habari za kizushi kuwa eti Mgombea wa Udiwani wa Elerai wa CHADEMA amejiunga CCM. Sasa kijana Mtela Mwampamba HAAMINIKI TENA. Hapa JF ameshapata 'zawadi' yake.

Bado chamani.Bado uraiani.Bado maishani. Bado akilini mwake. Bado atakavyomuona kivingine Mwigulu Nchemba. Bado. Ni wakati sasa wanachama wenzangu wa CCM kuchuja kila kauli na vitendo vya viongozi wetu kama Mwigulu Nchemba ili tuwe huru.Tuwe makini. Kama tunamtegemea Mwigulu Nchemba na siasa zake za aina hii ionekanayo,hatutakuwa makini. Tutakimbiwa.

Siasa iwe ni hoja na si vihoja. Vinginevyo, Mwigulu Nchemba ataponza wengi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Ulitakiwa kuwa Makamu wa Karibu mkuu kwenye hilo Chama lenu ungaliweza kuwa msaada sana
 
Mwampamba amekuwa robot la mwigulu. Anaamriwa afanye ki2 fulani naye anafanya kweli,nahisi hata 0713 akiambiwa na mwigulu atakuwa tayari kumegea angalau mini kabang

Kanunuliwa huyo hana hiari yake, Mwigulu ndo anamuweka mjini, mwingulu akiwa ndo mwalimu wako wa siasa unadhani utajifunza nini kwake zaidi ya kuropoka tu?
 
Mwampamba amekuwa robot la mwigulu. Anaamriwa afanye ki2 fulani naye anafanya kweli,nahisi hata 0713 akiambiwa na mwigulu atakuwa tayari kumegea angalau mini kabang

Ha ha haaaaa, mkuu naona umefika mbali du!
 
VUTA-NKUVUTE ama kweli post zako ni za faraja, Endelea kuwaelimisha na wale wengine wanaowaza kumwaga damu za watanzania halafu wakipanda jukwaani mchana kweupe wanaanza kuwadanganya watanzania kile kilichotokea usiku.

Waerevue kuwa TANESCO imesaidia kuwaangazia watu hata kama ni usiku basi ni kama mchana na hakuna kinachofichikana katika matendo ya mwanadamu.
 
Huyo mwendawazimu mnahangaika naye wa nini? Acheni hata kutaja jina lake hapa.
 
nimekaa, nikatafakiri, na ku google mtu mwenye character za mwigulu ni jina gani lina mfaa...nimeona ni ZUZU!
 
chama tawala kinapaswa kijitasmini katika sera zake, kwani watanzania wa sasa niwaelewa hawakubali kubuluzwa.
 
Wewe endelea kuwaokota wajinga wenzako kwa uwongo na uzandiki ukijifanya kada wa CCM makao makuu wakati hata ofisi zake huzifahamu achilia mbali kuwa mwanachama wa CCM.

Sheria za JF haziruhu name calling lakini tunakufahamu vizuri sana.

CCM umewabana mpaka mnatengeneza ID na kujifanya makada wa CCM katika mwendelezo wa siasa zenu za KILAGHAI kwa watanzania.

Kuonyesha ni kiasi gani mlivyo walaghai, unaweka thread halafu viongozi wako wanaanza kuchangia.

Kama Mwigulu anaiumiza CCM huoni kama ni neema kwa chama chako CHADEMA.

Kwa sasa mnapanga foleni kuleta thread JF kuhusu makada wa CCM kuonyesha ni jinsi gani tunavyowabana kisiasa.

Mtaandika sana kuhusu Mwigulu.

It's only 2013.
Mw, ug uli unatisha kaka mimi nakuita live kwa jina lako coz unakimbiza mbaya, CCM tunakukubali moto huo huo kaka, na tutakupa ukatibu kabisa wa chama chetu soon, ila najiuliza hapo top tupafanyeje maana wewe ni mtu wa Lowa hasa, naPe yeye ni kundi kuvua gamba mzee wa mapengo/Mangule kanywea nywiiiiiiii, mwakani si utatuua wenzako tusipomsapoti Mfadhili wako Lowa asha
 
Mwigulu Nchemba anatumia nguvu nyingi akili ndogo, hatimaye watu makini hawataki tena kumsikiliza maana yeye hata ikitokea dawa hamna hospitalini utamsikia akisema, "CHADEMA wameshirikiana na MSD kuchelewesha madawa makusudi ili kuwachochea wananchi waichukie serikali..." He is very poor to present logical argument!
 
Mwigulu Nchemba anatumia nguvu nyingi akili ndogo, hatimaye watu makini hawataki tena kumsikiliza maana yeye hata ikitokea dawa hamna hospitalini utamsikia akisema, "CHADEMA wameshirikiana na MSD kuchelewesha madawa makusudi ili kuwachochea wananchi waichukie serikali..." He is very poor in logical argument!
 
Huwezi kufanya siasa za kikatili na kifedhuli kama mwigulu ukabaki salama hata yesu akiwa mjomba wako na bikira maria akawa bibi mzaa mama.
 
sawasawa hivi social kuna cdm?

Mbona wagombea wenu huwa mnawambia wajifanye CDM wanapoomba kura hapo hapo social au unadhani kuwa CDM mpaka kubebana njaa ikiuma kwenda kuomba buku kwa lema kama ninyi mnavyofanya .....vp juice ya kwa EL ilikuwa tamu mlipoenda kuomba buku mlipolewa juice mkajikuta mnalopoka eti mmetumwa muombe agombee urais, huo ndio usomi tz? CDM iko moyoni sio kelele zenu kwa kubebwa na kikura na mlacha....kikao cha chama(ccm) mnashirikisha management halafu mnasema siasa mwiko chuoni. Mnatumika tu kama kondom mtatupwa .
 
NAULIZA HIVI LILE KUNDI LA WABUNGE WA CCM WALIOJULIKANA KAMA WAPAMBANAJI WA IFISADI WAMEFIA WAPI? Mbona wamepata kigugumizi CHA longolongo Yao ya RICHMOND, DOWANS NA SASA SYMBION. Jamani kulikoni. SITTA,MWAKYEMBE, na wenzao. Sasa wamenyoosha mikono kwa mchumi mahiri Mh. ZITTO KABWE. MWAKYEMBE sasa amegeuka fisadi mkubwa Kule Wizarani. YUKO BUSY NA hongo za TPA na mradi ya kununua Ndege. PESA Bwana mbaya Bwana. Wameshasahau waliyo yatunga ya Richmond sasa wao wanakula tu. Vipi Mwigulu unaonaje Hilo. Nawe upewe WAPI uanze KULA kwa ulafi na kujinufaisha ILI uachane na CHADEMA
 
Laana ziwe nawe daima Mwingulu Nchemba!kama Mungu aishivyo na akulaani kwa kadiri ya matendo yako!Nijuavyo siasa si uadui!siasa ni undugu kwa kushindana na sera za mwingine!sasa huyu anaingiza chuki(Mwingulu),siyo mtu bali ana roho za kinyama!Auaye kwa upanga atakufa kwa upanga.
 
Sisi wengine wavivu wa kusoma sheria, kama umeponzwa na mtu ban kwa nini msipewe wote? Kama ni kweli Mtela haitendei haki Elimu yake na hakitendei haki chuo chake na fani yake kwa ujumla
 
Sisi wengine wavivu wa kusoma sheria, kama umeponzwa na mtu ban kwa nini msipewe wote? Kama ni kweli Mtela haitendei haki Elimu yake na hakitendei haki chuo chake na fani yake kwa ujumla
Sasa na Nchemba kapata ban!
 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mwigulu Nchemba ni mwanasiasa wa ajabu sana. Hajali. Hasikii.Haelewi. Anachojali yeye ni kujijenga(pia kujibomoa) katika siasa.Anataka kuaminika kama dawa pekee ya kuwadhibiti CHADEMA kati ya makada wote wa CCM.

Ndiyo maana anafanya anayoyafanya. Mwigulu Nchemba anaamini kuwa anaungwa mkono na Mwenyekiti wa chama pamoja na viongozi wengine waandamizi wa CCM Taifa. Ndiyo maana anaweza hata kubuni 'mijivazi' yake hata inayokwenda kinyume na sare rasmi za chama.Anaweza asiwe sahihi.Aweza kuwa anapotoka. Mwigulu amelewa sifa. Anapepesuka. Kwa wasio makini kisiasa na wanaomtii Mwigulu Nchemba kwa kila alisemalo wataponzeka.

Watasawajika kisiasa na kichama. Jana tu, kijana Mtela Mwampamba ameingia mkenge wa Mwigulu.Amekurupuka na habari za kizushi kuwa eti Mgombea wa Udiwani wa Elerai wa CHADEMA amejiunga CCM. Sasa kijana Mtela Mwampamba HAAMINIKI TENA. Hapa JF ameshapata 'zawadi' yake.

Bado chamani.Bado uraiani.Bado maishani. Bado akilini mwake. Bado atakavyomuona kivingine Mwigulu Nchemba. Bado. Ni wakati sasa wanachama wenzangu wa CCM kuchuja kila kauli na vitendo vya viongozi wetu kama Mwigulu Nchemba ili tuwe huru.Tuwe makini. Kama tunamtegemea Mwigulu Nchemba na siasa zake za aina hii ionekanayo,hatutakuwa makini. Tutakimbiwa.

Siasa iwe ni hoja na si vihoja. Vinginevyo, Mwigulu Nchemba ataponza wengi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

umetumwa wewe
 
Back
Top Bottom