Nicholas
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 25,260
- 7,217
Unaweza kuniambia "image mbaya ya mbwa" inatokana na kitu gani kwa mwafrika?Yani kihistoria ni kitu gani kilichofanya mbwa awe mnyama mbaya kwa waafrika specifically wabongo?
Haijaandikwa sana ila:
- Tusi maarufu na litolewa ni mbwa.
- Mbwa huwa hawakaribishwi ndani ka vile huonekana ni mchafu hata kata km kaoshwa.
- Mbwa akibweka kwa kilio kirefu usiku huwa watu humhusisha na balaa.
- Mbwa ni najisi kwa watu wengine."Ingawa huwa anatumika kuwinda".
-Mbwa huwa wanapewa mabaki, ama ya chakula kilichosazwa na binadamu ikiwepo mifupa,ama mabaki ya processed food katik machinjio au hata mahotelini(Mbwa wengi huwa wana upungufu wa virutubisho).
-Mbwa huwa anahusishwa na tabia mbaya.(kama umalaya na matendo ya ngono bila adabu).Utasikia watu wakiwaambia wenza mnat**** kama mbwa.
Na mengine mengi::
Kwa mambo ya kigeni,ila vipo kati ya waafrica, watu wanaamini kuwa wakiwa katika swala au hata wakishajiandaa kwa ibada mbwa hapaswi kumnusa na ikitokea basi huwa anaharibu ibada ile.
So Mchemba hakupaswa fanya au hata kukaa kimya bila kukemea hayo ,hata kama atakuwa anadhani kuwa naakaribia acha siasa.naogopa kusema kwani nitaitwa mkabila.Ila ukanda aliotoka kwa miaka ya karibu pamekuwa sana na kumomonyoka maadili.Vijana wamekuwa wepesi kufanya matendo yenye upungufu wa kimaadili na wazazi wamekuwa ama wanachekelea au hata kushiriki.Hii ndio shida ya kuwa kizazi cha vijana wapuuzi ambao baadaye wanakuwa wazee wapuuzi. Mwigulu ni kizazi kiovu kinachofuatia.Kawa carried away na upepo unaomwendea ndani ya CCM.Na uhuru bila kuwa na wajibu wa kurekebisha au kupima matendo na maneno yake.Dogo kakosa busara kidogo tuu.Hakufundwa kujua kuwa hata adui yako akikumbwa na baya pasipo stahili (pasipo haki,yaani makosa yake),huwa si vyema kuchekelea lets alone kushangilia.Hata kama si yeye aliyeamuru ila hakupaswa furahia ule utoto,sasa kahalalisha ujinga sana.kesho akisikia mwanamke mwana CDM kabakwa na watu na mbwa kwa ushirikiano wa binadamu, atathubutu kemea kam alibariki bila mipaka?
Kwa CDM hakuna hasara ila kwa mchemahaina matokeo mazuri na kulifuta hilo ni kazi.Kuna vitu wahusika wakifanya hakuna shida,ila akifanya mtu wa nje hakitakuwa that okay.Wamarekani wanaheshimu sana bendera yao,ingawa pia wameiweka katika kila kitu hadi katika underwears.Ila hawatakuwa na tafsiri hiyo mwingine akifanya. Watu marafiki huitana Dog,Nigger, etc ila mtu aliye nje ya hiyo circle akimiwta yeyote ni balaa.