Mwigulu amvisha mbwa bendera ya CHADEMA

Mwigulu amvisha mbwa bendera ya CHADEMA

Status
Not open for further replies.
huyu si ni muajiriwa wa serikali (civil servant) pale BOT? sheria za nchi zinasemaje kuhusu civil servant kujihusisha actively na siasa hata kuwa na cheo kinachomtaka kuwa active daily?
Hapa ndio vituko vya vyombo vya dola vinapoonekana(ga)..hapo wana usalama walikuwepo lakini probably nao walisaidia kuoiga makofi ya kushangilia hicho kitendo. I am sure ingekuwa Mnyika au Heche au Lema angemvalisha mbwa bendera ya CCM kwenye mkutano wa wazi mbele ya wanausalama, asingepona!!!
 
Mimi binafsi sioni sababu ya wana CHADEMA kukasirika kwa kitendo cha kumvalisha mbwa bendera ya CHADEMA. Kuanzia binadamu na viumbe vyote viishivyo Tanzania vinahitaji mabadiliko ili viweze kupata hazi zao sawia. Tumeona wanyama wanauawa huko Serengeti huku kundi la vigogo wakineemeka na mauaji hayo. Wafugaji walalizwa mifugo yako all over the country. Kumuonyesha huyo mbwa na aliyekondeana dalili za ukombozi ni faraja kwa wapenda mageuzi. Kwa nchi za wengine mbwa huyo angeonekana alivyokendeana hivyo, mwenye mbwa angeulizwa na vyombo husika, kulikoni!! Inaonekana huyo mbwa anakosa haki zaki kama mnyama wa kufugwa.

Hivyo hata wanyama pia wanahitaji mabadiliko wapate haki zao. Kweli Mwigulu anafanya kazi nzuri kuisadia CHADEMA.
 
Kila kiumbe chenye pumzi kiishicho majini au nchi kavu Tanzania kitajua umuhimu wa Vuguvugu la Mabadiliko (M4C). Huo ni mwanzo tu, mbwa alivishwa bendera ya CHADEMA akakimbia kwa nguvu zake zote akijua kuwa lile kundi alilokuwemo kabla hajavikwa bendera si mmoja wao.
Good work Mwigulu kwa kurahisisha kazi za CHADEMA.
 
nchemba naona ana utoto mwingi na hatokb akuwe kiakili.
 
Heee, kumbe mwigulu ni kichaa?
Mamaaaa!!
Masikini jimbo la Iramba!!
Lakini, ni nini maana yake?
Huu ndo mwanzo wa kuchafua hali ya hewa, ebu fikiria mimi pia nifanye ujinga kama aloufanya yeye kwa chama chake nini kitatokea?
Hapana, wananchi wa jimbo lake na Watanzania kwa ujumla wasisherehekee hilo ni hatari kwa amani ya taifa letu.
Huyu mtu ni hatari na ndiyo maana ana kesi za uendawazimu mahakamani Singida.
 
Binafsi nikushkur tu mwigulu kwa kuwajulisha Watanzania hasa wapiga kura wako kuwaza kulipoishia, ndivyo mtazamo wako ulivyomfupi na ndivyo wanairamba pia wanapoishia kuwaza.
Mtanisamehe wanairamba kwa kauli hiyo na wala kwa sasa hamtokwepa kashfa hiyo labda baada ya uchaguzi mwingine ndipo tutawatathmini upya je, mnamaanisha kweli huyo jamaa ndiye awawakilishe na hayo ndiyo mawazo yenu au kapita tu kwa bahati mbaya!! Nawatakia upimaji mwema wanairamba na poleni sana.
 
ccm wanatakiwa wafanye kuondoa miozo kwenye chama chao kwani kuwaacha haw ni kujiua tu.... hii ni sawa na mzungu kumuonesha mwafrika ndizi ya kuiva
 
Nawaomba viongozi wa Chadema hili jambo lisiwahangaishe kabisaa, wasijibizane na hicho chemba kisicho na chembe cha akili wala maadili. Bila shaka mazuzu wenzake ndani ya CCM yatakuwa yanamshangilia na kumpongeza kwa hilo tendo...si ndivyo walivyo? Mtu mwenye akili timamu, nasema na kurudia, mtu mwenye akili hawezi kukishabikia chama hicho ambacho kimejitambulisha kama kimbilio la wahalifu ... mafisadi, wapuuzi, wezi na wauaji. Huko wanapatikana tu wanafiki akina Mwigulu na Nape...watu ambao watasaliti hadi ndugu zao mradi wanatupiwa makombo chini ya meza.
 
Cha muhimu ni kumpoteze tu, hana akili timamu huyo!
 
Mimi naona sawa Tu!! Mbwa nae ni Mnyama ambaye ana Haki zake!! Kitendo cha baadhi ya watu kuona kinyaa kwa Vile bendera kavishwa mbwa naona si sawa!! Ni haki yetu kuvipenda kila kilicho na pumzi kama hakidhuru mwili!!
 
hivi kisheria ni sawa hii kweli, nadhani ni sababu tosha kumshitaki mahakamani napo ikishindikana tunamshtaki kwa wapiga kura wake kwa maana sidhani walimchagua kufanya mambo ya kijinga kiasi hicho..
 
Kama mbwa alivyofungwa bendera ya Chadema ndivyo Mwigulu anavyofunga skafu yake SHINGONI, hivyo akili ya Mwigulu anairithi kwa MBWA ingawa yeye anaonekana ni Binadamu
 
Huyo jamaa aliye defect mbona anadai kulala porini kukimbia kuuwawa na haohao CCM mpaka kaamua kujisalimisha kwao? Au mimi silelewi vizuri? Angalia hiyo clip kuanzia 6.23
 
hata mbwa wanaipenda chadema.. Mwambie awavike ya ccm kama hawajashikwa kichwa..dogs are friends of people
.Mwigilu kubeba bendera ya chama, kama kweli ni ishara kuwa CDM ipo akilini mwake na anaikubali
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom