Mwenye nyumba yako anaweza kukuvumilia miezi mingapi bila kumlipa kodi yake?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,579
44,821
Maisha yenyewe ya sasa ukijichanganya ukaishi maisha fake ya kuigiza lazima u collapse tu kuna mpangaji mwenzangu single mother aliforce kumpeleka mtoto shule hizi za mamilion sasa hata baba mtoto amegoma kulipa ada mambo magumu Leo hii kafikisha miezi Sita anadaiwa tu kodi ila baba mwenye nyumba wetu mvumilivu sana anapigwa tu sound ametulia kuna mwingine yeye alidaiwa kodi ya mwaka mzima hadi akakimbia chumba kaacha kitanda na vyombo mwenye nyumba na mjumbe wamevunja mlango Mwenyenyumba kachukua Mali hizo.Mimi binafsi sijawahi kupitisha miezi miwili bila kulipa yaani bora nidaiwe kausha damu huko kuliko kodi ya chumba nacholala.
 
Kudaiwa kodi kwa mtu muadilifu ni mateso makubwa ya nafsi......unakosa hata raha ya kutulia na familia yako.....

Lakini yote kwa yote si vyema kumkimbia anayekudai....kuwa muwazi kwake juu ya Hali unayopitia kwa wakati na yeye umuachie nafasi ya kuamua bila kumshinikiza afanye maamuzi unayoyataka wewe........

Akisema ondoka kwangu basi huna budi kufanya hivyo kwani ni haki yake kukudai na ni wajibu wako kumlipa.....

Mungu awafanyie wepesi wale wanaopitia changamoto hiyo.......
 
Maisha yenyewe ya sasa ukijichanganya ukaishi maisha fake ya kuigiza lazima u collapse tu kuna mpangaji mwenzangu single mother aliforce kumpeleka mtoto shule hizi za mamilion sasa hata baba mtoto amegoma kulipa ada mambo magumu Leo hii kafikisha miezi Sita anadaiwa tu kodi ila baba mwenye nyumba wetu mvumilivu sana anapigwa tu sound ametulia kuna mwingine yeye alidaiwa kodi ya mwaka mzima hadi akakimbia chumba kaacha kitanda na vyombo mwenye nyumba na mjumbe wamevunja mlango Mwenyenyumba kachukua Mali hizo.Mimi binafsi sijawahi kupitisha miezi miwili bila kulipa yaani bora nidaiwe kausha damu huko kuliko kodi ya chumba nacholala.
Baba mwenye nyumba wangu hana uvumilivu. Yeye anataka kodi ya miezi 6 sasa hata ukimuomba kuwa umlipe ya miezi minne na hiyo ya miezi miwili iliyobaki utalipa ukilipwa mshahara hata kama bado wiki 2 ulipwe anakwambia ni heri pabaki tupu yaani uondoke kuliko kulipa miezi minne. Tulikuwa wapangaji 6 tumeondoka wote wamebaki wawili.
 
Tatizo ni pale unapomkimbia mwenye nyumba. Kama umekwama ni vizuri kuwa muwazi kwa mwenye nyumba ; mwenye nyumba ni binadamu atakuelewa. Vijana Hapana kuishi maisha ya cinema ndio maana mnakwama!
 
Mtaa ninapoishi kuna mzee mmoja ye hataki kabisa kusumbuana na wapangaji, na hataki kabisa mazoea. Ukikaa mwaka mmoja tu anakupa notes uondoke then anaingia mpangaji mwingine.

Vyumba yoyote utaratibu ndio huo huo.
 
Maisha yenyewe ya sasa ukijichanganya ukaishi maisha fake ya kuigiza lazima u collapse tu kuna mpangaji mwenzangu single mother aliforce kumpeleka mtoto shule hizi za mamilion sasa hata baba mtoto amegoma kulipa ada mambo magumu Leo hii kafikisha miezi Sita anadaiwa tu kodi ila baba mwenye nyumba wetu mvumilivu sana anapigwa tu sound ametulia kuna mwingine yeye alidaiwa kodi ya mwaka mzima hadi akakimbia chumba kaacha kitanda na vyombo mwenye nyumba na mjumbe wamevunja mlango Mwenyenyumba kachukua Mali hizo.Mimi binafsi sijawahi kupitisha miezi miwili bila kulipa yaani bora nidaiwe kausha damu huko kuliko kodi ya chumba nacholala.
Wa kwangu huwa anadai hata kabla ya muda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom