Mwanza jiji zima hakuna Brown Bread?

Haya mambo sijui ya brown bread, brown sugar, low fat milk etc Tanzania bado sana. Wengi tumeyajua tulipoenda majuu hivyo wengi ambao hawatoka yanawatesa. Kwa mfano ukienda dukani unasema nipe sukari na unapewa sukari yoyote.
Mimi nimejua brown bread hapa hapa bongo tena nikiwa mdogo sana
 
Royal oven ipo, cafeteria ipo
 
SAUT imehamishia wachaga wengi sana Mwanza luchelele, buhongwa, mkolani, nyegezi mmepateka
 
Hakuna mgeni atapendelea brown bread unless awe na kisukari, ni mikate isio na ladha kabisa hata upake jam na peanut butter bado haina taste.
 
Hiyo ni fursa fungua kiwanda cha mikate ya brown
 
Ipo mingi,nikiwa Mwanza nishatumia iyo mikate mara kwa mara.
Kerla beckery.
Mwanza beckery.
Buswelu beckery.
War same beckery.
izoπŸ‘†ni baadhi ya beckery ambazo nimeshatumia mikate yao ya brown.
 
Nilipoenda Mara ya kwanza Mwanza, nilishangazwa sana na uwingi wa Mbwa
 
Kuna kule Kiseke jamani hupigi hatua 2 bila kukutana na mbwa koko 15. Yaani nahisi kiseke mbwa koko ni wengi kuliko watu wanaoishi. Jioni pale mjini wapika vitumbuka kila baada ya hatua moja.

All in all mwanza ni mji mzuri sana kuishi hata kama unaanza maisha kila kitu kipo affordable kuanzia vyakula, usafiri mpaka nyumba za kupanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanza ni ukubwa tu ila ni jiji la kishamba sana huwezi compare na Arusha au Dar, tuiacha Dar ni kubwa sana ila huwezi ilinganisha na Arusha kamwe.
Hakuna cha mkate wala nini kiini cha mada yako ni hayo manenoπŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†
Wivu na chuki dhidi ya mwanza vitawauwa, wewe endelea kutibu kisukari chako tena pole sana, hizo mikate ya brown inapatikana sehemu nyingi tu mwanza lakini watu hawapendelei na bei yake ipo chini kulinganisha na white bread.
 
Hoyo mikate mingi sana royal oven isifie tu Arusha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…