Mwanza inarudi nyuma huku Arusha ikiendelea

Mwanza inarudi nyuma huku Arusha ikiendelea

Bukoba tangia ile vita mlianguka sana... Ila naona sasa mnaanza kustawi tena.. Kila la heri huko, chapeni kazi, ongezeni na base ya viwanda kutoka Kagera Sugar mkifungua vingine vichache mtapiga hatua sana...

Tatizo lenu ni moja tu, vigogo wenu tunakunywa nao bia huku mijini tu nyumbani wamekusahau..
Kesho tuanzishe thread ya tanga vs mbeya
 
Ni kweli huna akili na kama unazo basi umeshindwa hoja ila hutaki kukubali... Data ulizoleta wewe mwenyewe zimekuambia wazi Arusha iko mbele ya Mwanza, data nilizoleta zinasema hivyo hivyo.. Hizi data ni za Serikali ila wewe umekimbia unasema Zitto kawaambia sijui Mwanza, sijui Shinyanga... Huyo Zitto yeye ni serikali?? Huo utafiti wa Zitto umetoka wapi??

Yaani wewe uko hapa kubishana na TRA, NBS, UN kwa sababu eti Zitto aliwaambia... Hivi hapo nikikwambia huna akili unakasirika nini??
Hujui hata kusoma data, website ya Arusha imekosea, The citizen wamekosea, Zitto hayupo sahihi, zile data za NBS wewe ndio umezielewa zaidi kiasi kwamba unafafanua na kufafanua...

Hao wote hawajaelewa ila ni wewe mwenyewe umeelewa na upo sahihi, endelea kubaki hivyo hivyo tu...

Kama vipi temana na mimi...
 
Hivi hapo Arusha mbona sijaona kiti cha ajabu? Ni kama Iringa tu!
 
Sikusema Mkapa alipendelea huko ila katika awamu yake ya pili alipakumbuka huko aliweka lami akaweka na miundombinu alijitahidi...

Na kipindi hicho ndio ikaanza kukua sasa kwa kasi...

Lakini hapa tunajadiliana tu, sioni haja ya kuanza kutukanana, kama vipi mi nakutema tu...
Wewe niteme tu mkuu ila nadhani leo utalala ukiwa unaujua ukweli... Msikimbilie kubishana wakati data za kusupport ubishi wenu hamna.. Ila msiwaze sana watu wa Mwanza, hapo ameletwa kichwa TRA Mzee Nyange, mkimtumia vizuri mtapiga hatua kwenye ukusanyaji wa mapato..
 
Hujui hata kusoma data, website ya Arusha imekosea, The citizen wamekosea, Zitto hayupo sahihi, zile data za NBS wewe ndio umezielewa zaidi kiasi kwamba unafafanua na kufafanua...

Hao wote hawajaelewa ila ni wewe mwenyewe umeelewa na upo sahihi, endelea kubaki hivyo hivyo tu...

Kama vipi temana na mimi...
Unaleta website za watu na magazeti ya nini wakati all sources zipo kwenye website za serikali..

Nilivyoona ubishani kwa data za kiuchumi ndio nikajua kumbe hujui lolote.. Jedwali la NBS ambalo wewe unaling'ang'ania hizo data haziko kwenye current price... Hivi Dar ingekuwa na GDP ya Million 13 aisee si ingekuwa ni maajabu.. Yaani kama Dar ingekuwa na hiyo GDP per Capita ya Million 13 ina maana Whole Dar City GDP yake ni Tshs. Trillion 65... Hivi wewe hayo huoni ni maajabu??
 
Kesho tuanzishe thread ya tanga vs mbeya
teh teh teh teh itabidi tupate watu wa kuitetea Tanga... Motochini mapendekezo hayo, mimi nitajaribu kuwatetea ndugu zangu wa Tanga japo itakuwa ngumu kwao kutetewa.. Sema lile bomba litawainua sana Tanga..
 
Mleta mada unakosea kulinganisha kati ya hizi miji miwili. Arusha ni sababu ya utalii, ndo maana unaona hotels na baadhi ya makampuni HQ zao zipo hapo, ila Individual Mwanza ipo juu sana!! Mwanza maeneo mengi sana watu wameweka nyumba za maana ambapo kwa miaka 4 ya nyuma yalikuwa ni mapori!! Kiukweli Mwanza inakuwa kwa kasi sana upande wa makazi tofauti na Arusha ambapo ni Njiro tu!!! Mi mwenyewe kila baada ya miezi miwili naenda Mwanza, lakini nakuta baadhi ya maeneo yamebadilika kuliko nilivyopaacha!!
 
Acheni kuifananisha Mwanza na upuuzi,Arusha bado ni Manispaa tu...hakuna cha maana japo taasisi kubwa za kiserikali Kama TANAPA,TAEC,AICC zina makao Makuu...ila Mwanza inajengwa na wanamwanza wenyewe...Kutoka Igoma mpaka Buhongwa ni Route ndeefu ila.bado uko ndani ya jiji na hamna uswahili...Mwanza ni kubwa imepanuka na huduma kubwa kubwa za kibiashara na si Arusha...
Niko Arusha mwaka wa Sita sasa ila nikifika Mwanza najisikia raha...hasa nikiwa Kenyatta road kuelekea Airport ukiona mwambao wa Victoria ni Raha hasa...Huku Arusha ni viroba na bangi tu...sehem ambayo iko vzuri ndo inaendelea kwa sasa ni Njiro,tena Mwisho ni hapa Njiro kwa Msola...ila maeneo mangi ni uswahili afu kamji ni kadogo mno.
Mwanza ndo jiji la pili kwa ukubwa,wingi wa watu na kiuchumi...Jamani mnapoandika vitu mfikrie vzuri.MWANZA ipo Top five ya majiji Afrika Mashariki..na si Manispaa ya Arusha
kweli kuelewa nalo ni tatizo
jamaa anamaanisha ukuwaji wa Mwanza umepungua Arusha inakuja kwa kasi sana wewe unajua kwa Msola tu kuna Ngaramtoni ya chini kuna UZUNGUNI
 
Acheni kuifananisha Mwanza na upuuzi,Arusha bado ni Manispaa tu...hakuna cha maana japo taasisi kubwa za kiserikali Kama TANAPA,TAEC,AICC zina makao Makuu...ila Mwanza inajengwa na wanamwanza wenyewe...Kutoka Igoma mpaka Buhongwa ni Route ndeefu ila.bado uko ndani ya jiji na hamna uswahili...Mwanza ni kubwa imepanuka na huduma kubwa kubwa za kibiashara na si Arusha...
Niko Arusha mwaka wa Sita sasa ila nikifika Mwanza najisikia raha...hasa nikiwa Kenyatta road kuelekea Airport ukiona mwambao wa Victoria ni Raha hasa...Huku Arusha ni viroba na bangi tu...sehem ambayo iko vzuri ndo inaendelea kwa sasa ni Njiro,tena Mwisho ni hapa Njiro kwa Msola...ila maeneo mangi ni uswahili afu kamji ni kadogo mno.
Mwanza ndo jiji la pili kwa ukubwa,wingi wa watu na kiuchumi...Jamani mnapoandika vitu mfikrie vzuri.MWANZA ipo Top five ya majiji Afrika Mashariki..na si Manispaa ya Arusha
Kweli arusha n ndogo sana, ukijenga viwanja vya mpira 3 unamaluza mji mzima
 
Wana JF

Sina lengo laku pambanisha Mwanza Vs Arusha ila kiukweli nashindwa kuelewa nini kimeisibu Mwanza.

Mwaka 2002 Nikiwa shuleni Mwanza nilijiona kama nipo Dar ndogo.Mwanza ilikuwa motoMambo yalikwenda faster mji ulikua unakua kwa kasi sana

Nilikuwa nikiamini kufikia 2015 jiji la Mwanza litakuwa la mfano kwa ukuaji wake cha ajabu na kushangaza Arusha ndio inakuja faster huku Mwanza ikidorola kama mtoto mwenye utapia mlo kulikoni.

Tatizo nini Mwanza?Kama kuongozwa imeongozwa na CDM muda mzuri tu kwanini Haipai kwa kasi ilee!?

Nashindwa hata kulinganisha Mwanza VS Arusha maana Arusha kwasasa ipo moto vibaya kama hali itaendelea kuwa hivi tutegemee Arusha kuwa ndio jiji la pili kwa ukubwa Mwanza inakuja kupitwa na Dodoma itanikera sana.
We mimi nikiwa dar mwezi mmja tu nataka kurudi rock town city je nikiwa arusha ni wiki 1 tu narudi huko city kwetu achana na mwanza baba zamani iliitwa nyanza komaa bro sasa ni mza aka ROCKCITY
 
ni ukosefu wa adabu kulinganisha jiji la mwanza na arusha, linganisha manispaa ya ilemela na arusha hapo ndo itamake sense
 
Mwanza ongezeni juhudi ya kiuchumi na mpunguze kuzaa maana kuna consume capital for investment,la sivyo mtaanza kuburuzwa na dodoma na mtwara soon,mmeshindwa kujustify uhalali wa kua jiji la pili badala ya kuleta vivid examples mnaleta picha za kwenye office shelves..
 
Kwa wale mnaoponda mbeya kwa kusikia ni vyema mkaja kutembea,anzia igawa,mbeya hadi Tunduma utakua umepita sehemu kubwa ya wilaya zake alafu rudi safiri kuanzia karatu arusha moshi hadi korogwe then rudi hapa Jf unambie eye surveying yako inakupa picha gani ya maendeleo general exclude hang over ya magorofa
 
Kama mzunguko wa pesa mkubwa kwanini kodi inayokusanywa Arusha ni mara mbili ya Mwanza wakati Mwanza ina idadi ya watu mara mbili ya Arusha??? Huko shule mlienda kusomea ujinga au kitu gani??

Uanze kutumia akili na ww kumbuka hizi ni takwimu za mkoa mzima wa arusha ambako kumejaa mbuga za wanyama na vivutio vya utalii, weka hapa takwimu za Arusha City vs Mwanza City tujadiliane
 
Back
Top Bottom