Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,508
- 911,249
- Thread starter
-
- #61
Nshomile Ruta nimekubali shairi lako. Imebidi niandike kwani nilihisi kitufe cha "like" kisingeyatendea haki mawazo yangu. Ila unaonaje ukijikita kwenye umalenga ikiwezekana uandike vitabu kwa ajili ya hiki kizazi kipya cha SMS.
[MENTION]Unatafuta ugomvi na Madameb.
Unaposema mfumo dume una maana gani?
kama una maana mwanamke kuwa 100% responsible kwa mambo ya kike na mengine ambayo itabidi apambane nayo kwenye mazingira yake, na mwanaume kuwa 100% responsible kwa majukumu ya kiume na mengine ambayo life itamtupia then naomba niku 'like'
lakini kama una maana mwanamke kuacha majukumu yake kukimbilia mengine na kutaka watu wengine ndio watake cover ya alioacha, au mwanaume kukumbia majukumu yake na kukimbilia mengine ili akiacha watu wahangaikie na majukumu asilia ya kwake then HAPANA.
hivi mfumo dume hasa uwa ni upi? mimi hua nasikia wanautaja wakati wanazungumzia kupiwga kina mama, kuachiwa kazi ngumu etc kwa upande huu siwezi kuongea sana ila sipendi familia ya hivi.
Nilimaanisha kuwa, mwanaume kwa maumbile, ni lazima atumike na awe mwangalizi. kama atanunua mikuki na kulinda sungusungu, au ataweka walinzi, au atasimamia uwepo wa security alarms, inabidi imkae kichwani, ukiona mama ndio anahangaika na kama alarms, walinzi kama wamekuja, kama mbwa ni wakali, wamekula au kucheki milango imefungwa usiku, inabidi ujue significance yako inapotea
pia ukiona familia watoto wanakula usichojua, wanafunga na kufungua shule bila kuulizwa, wanaugua nakupona bila wewe kujuuliza, mama na watoto wanavaa mwaka mzima h ujihusishi lazima tukushangae
[MENTION]mwanaume kusimama, miguu yote mitatu,
mmoja wa kwake mamaa, miwili ni ya viatu,
kwake usikae hama, mpende kwa wote utu,
mwanaume kusimama, heshima kujiletea.
Shair zuri, ila litume BBC watakupa pesa, jf kuna fan nyingine.:becky::becky::becky::becky::becky:Mwanaumme bila kazi hapendeki
Shida akililiwa visingizio kibao
Kumgalagaza mwenzie kitandani haoni kero
Lakini matunda yake kamwe hayali
Mwanaumme ni nini haswa?
Binti alijipanga bila ya zengwe
Yalikuwa matunda ya ushauri nasaha
Mwenzie alimpasha amalizane naye
Naye aliafiki na sasa matunda yapo hadharani
Mwanaumme ni nini haswa?
Rafikiye alimwuuma sikio naye akaafiki
Kisa mkomoe na uja wepesi
Mengineyo yatajipa sasa ni kilio
Kijana kaingia mitini na hataki tena
Mwanaumme ni nini haswa?
[MENTION]Mwanaume ni onja onja....
wabohaki,kaka Ruta
Nawasalimu wa kunyumba
uanamume ndio utata
mengineyo ni viambata.
sio gari unalobuluta
wala ghorofa yako nyumba
au wangapi umewapata