Mwanaume, unachopaswa kufanya ukiwa kwenye Mgogoro wa ulezi wa Watoto na Mwanamke

Mpasuaji wa Manesi

JF-Expert Member
Mar 13, 2016
299
1,372
Mwanaume,

NDOA ikishafeli, na Wakati tu mgogoro wa kugombania watoto utapoanza na wewe ukakomaa nao, hapo kaa ukijua tayari umeshindwa kabla hujaanza. Yaani hapo Mwanamke tayari anakuwa amekushinda.

Mkienda Mahakamani, utashindwa.

Ukienda Kanisani, huko pia utashindwa.

Ukienda Ustawi wa jamii, utashindwa pia.

Na hata ukija Jamiiforums pia, bado utashindwa (members watakukaanga).

Hivyo nisikilize Mpasuaji wa Manesi,

Tenganisha Hisia zako na watoto wako, mambo ya hisia achia Wanawake, hao tayari ni watoto wako na jamii inalifahamu hilo. Na hata watoto wako pia wanafahamu kuwa wewe ni Baba yao, hivyo huna sababu ya kuleta visirani.

Kama Mama yao anahitaji kubakia na watoto, ni sawa. Muache abaki nao. Huna sababu ya kuchukua wanao kinguvu na kuwapitisha watoto kwenye migogoro itakayoharibu fikra zao na kuwaachia kumbukumbu mbaya.

Kama kweli unajali watoto wako, basi jiepushe na migogoro na malumbano isiyo vya lazima. IKIWEZEKANA, Jitahidi kuwafanya hata watoto wako wasijue nini kinaendelea.

Wewe Ondoka kwa amani na fanya majukumu yako inavyopaswa.

  • Wafungulie watoto account ya Bank.
  • Weka pesa humo kila mwezi.
  • Weka kiwango maalumu kinachoweza kutoka kwa mwezi mtu atakapotoa.
  • Lipa ada moja kwa moja kwenye Shule husika.

Watoto sio wajinga, wanaona kila kitu na watafahamu kinachoendelea. Wakati wao utakapofika watakutafuta.

LAKINI ukiendelea kuwa wa migogoro, mara uibe mtoto, mara ugomvi, mara vikao kila siku, hata watoto wako nao watakuona wewe ni PUMBAVU na hawatakuheshimu.

"Mimi siwezi kuacha damu yangu", "Lazima niwapambanie wanangu", Hizi ni kauli za Wanaume wajinga. Mitazamo yao kuhusu ndoa ni ile ya kwenye drama na kwenye Movie.

Be a Man, Stay taliban.

EDITED, Tar 4 August 2023:
Nimesoma Comment za wale wale mnaoendeshwa na hisia, "My child is my everything", "nipo tayari kwa lolote kwa ajili yao", "I love them and they love me so much and other bla bla bla."

Mpo SAHIHI pia, endeleeni kupambana na hio migogoro huko Ustawi wa jamii, vikao kila siku na Mahakamani, hakuna aliyewazuia.

Mtu isipomfaa akili yake, basi utamdhuru ujinga wake.
 
Uko sahihi Ila unaweza kuta mke wako kajificha kwenye ulokole kumbe anafanya umalaya wa kimya kimya unapogundua umalaya wake Anza tangaza umpi matuzimizi kwa ndugu na majiran baana na kukana ndoa yake wakati umezaa nae hataki huduma yoyote toka kwako kwa walikuwa wanampa kichwa na wanabwaga.

Tena anakumbuka anataka matumizi yako na kujificha kupitia kwa watoto anahitaji matumi aliyokuwa napata kila ayamishie huko kusikojulikana na hii shauri ya makanisa uchwara yanayonzishwa.

Sasa Kuna majambazi wazizi, wauaji wamefanya madhabi mikoa wakifika wanajifanya waokoka waongo.iko haja kwa wizara Mambo ya ndani kupeleka muswada bugeni kuwa namna nzuri ya kusajili hizi tasisi za kidin na waomba usajili wanakiwango gani Cha elimu sio watu walishindwa maisha mtaani.kukupanda kuwafanya wengine wajinga kuwapiga pesa na kuwafanya mazezeta
 
Uko sahihi Ila unaweza kuta mke wako kajificha kwenye ulokole kumbe anafanya umalaya wa kimya kimya unapogundua umalaya wake Anza tangaza umpi matuzimizi ...
Duuh mkuu pole sana kwa yaliyo kukuta japo sijaelewa kilichokusibu,nilichoelewa ni kua umeamua kuanzisha uzi ndani ya uzi wa mtu,pole sana ndio maisha tuendelee kupambana tu...pole mkuu

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Bado akili za kitoto na mnaendeshwa na mambo ya kijinga.

Kama mlikuwa na ndoa ni kitu rahisi hata kutatua hilo suala,Kwa vile automatically wewe ndo unajulikana ndo baba wa watoto Kwa hiyo utabaki kama mzazi wa asili kama utahudumia sawa kama utaacha juu lako.

Kama ni hawara ni kutafuta matatizo zaidi na pia wengi hukosa Ile nguvu ya kuhudumia ,wengine wanafika mbali kabisa kuwa na wasiwasi juu ya nasaba ya mtoto.

Wengi mnafeli hapa👉 Mshaaanza kuwaita majina watoto "we ndo muokozi wangu" sijui "we ndo baba" ,tambua suala la kuja kusaidiwa na huyo mtoto ni hisani ila sio lazima na hakuna guarantee atakuja kuwa na maisha mzuri unless otherwise uwe na maisha mazuri ya kumsomesha au kumfungulia biashara.

Kupata mtoto ni vyema ukatambua kwenye majukumu yako ambayo hakuna ulazima wa kuja kunufaika baadae na mtoto huyo ,sababu haukulazimishwa kuzaa mtoto.

Usije ukawa mtu mzima hovyo wa kutoa laana Kwa watoto ,jipambanie nafsi yako.!!
 
Uko sahihi Ila unaweza kuta mke wako kajificha kwenye ulokole kumbe anafanya umalaya wa kimya kimya unapogundua umalaya wake Anza tangaza umpi...
Kuwa makini sana hapa kuna mawili kama mwanamke akibaki na mtoto.

Mosi,anaweza kumtumia mtoto kama sehemu ya kupata kipato yaani anataka matumizi ambayo baadhi ya pesa atatumia yeye kama yeye.

Pili,wanawake wanakomoa ex wao Kwa kumjazia mambo mfano mtoto haumwi ila anasema anaumwa hapo anajua labda wewe una kipato Cha kiasi gani..Ila chuki ni real anaweza akaona wivu juu ya maendeleo yako.


Mi tambua maisha haya ukishazaa hovyo kama mwanaume na kipacho Cha kusuasua na watoto wakibaki Kwa mama zao basi umejimaliza..
 
kumbuka tu, matoto mengi ya wanaojiita superwoman ni mapapai...

Tunapambambania watoto kwa ajili ya malezi bora na si vinginevyo,... mwanamke atachukua mtoto atambwaga kwa bibi yake,yeye bize na kudanga haelewi lolote kuhusu kula, kusoma, michezo na afya ya mtoto, kazi yake yeye ni kupiga simu tu na kudai hela ya mtoto kila siku na inaishia kwenye vicoba,...

sababu kubwa ya wanawake kudai watoto sio uchungu, ni kudai tu hela za visingizio,...kifupi kama naachana na mwanamke,mimi binafsi na namna nilivyo hawezi hata kuthubutu kuwataka aende nao, sijui nyie ndugu zangu munavyoishi na wanawake wenu huko..

watoto wanabaki na sio kwa kuomba, huko sijui mahakamani,ustawi wa jamii,kanisani na hata misikitini ataenda yeye na sio mimi,maana sina muda wa Kupoteza kiasi hicho na hata sitishiki kwa lolote juu ya wanangu...

masuala ya KUCHUKIWA na watoto kwa wanaume sisi ni kawaida tu, ila wakishakuwa watu wazima wataelewa kwa nn baba alifanya hivi,.. hata sisi katika malezi yetu kuna wakati tuliwachukia sana Wazazi wetu, hasa sisi wenye Wazazi (wakoloni), lakini leo tunaelewa kwa nn wazazi walikuwa vile, na tunawapenda sana tu pamoja na kuwa na makovu ya bakora walizotupa utotoni... kifupi MWANAUME kuogopa kuchukiwa na watoto ni UPUMBAVU na uzwazwa wa hali juu mno (sifundishwi na mtoto namna ya kumlea, najua mimi nini nafanya) ikiwa tu unatenda haki na ni kwa faida yao wenyewe....

wewe mpe mkeo watoto wako wakalelewe na baba wa kambo aendelee kuwala mama na watoto, matoto yawe mapapai,majeuri na majizi eti kisa kuogopa kuchukiwa....

kwenye familia mwanaume ni kiongozi na si mwanamke
hata angekuwa na pesa au elimu kiasi gani(bado atabaki kuwa mwanamke)

ukishindwa kuthibitisha uanaume wako matokeo yake ndo hayo mwanamke anapata hata nguvu ya kudai watoto, mimi mwanamke mwenyewe hawezi hata kunitamkia huo UPUUZI maana anajua what's next,...

nakutakia kila lakheri katika kukabidhi watoto wako kwa mume mwenza, aendelee kujilia vinono....
 
My brother most women tunaozaa nao hawawezi kuhudumia wala kulea watoto katika busara,hekima na mazingira mazuri so kabla maji hayajamwagika mtoto kuwa na tabia mbovu bora nimchukue.
Kwanini mnazaa na wanawake wa hivo? shida ni ya nani ya kwako mzalishaji uaeona kabisa huyo mwanamke hawezi kulea watoto kwa busara na hekima na bado ukazaa nae au? Wanaume tunawalaumu sana wanawake lakini naona kuna mahali tunafeli.
 
I always tell my wife yaani tukiachana watoto atawaacha nitafanya kazi nitawalea by any means haya mambo ya watoto wakutafute baada ya kufeli maisha, shule au baada ya kuathirika na madawa BIG NO.
Ww kweli umeoa na nahakika hata ndoa yako haitavunjika.aliposema huyu ndugu yetu neno "toa hisia na wanao nimetumbua macho" sisi wengine kwa ajili ya mwanangu yoyote swala la kuweka uhai wangu Mezani juu ya maslahi yake si mjadala
 
Back
Top Bottom