Mwanaume, Mungu akikupa uhai mpaka unafikisha miaka 35 hakikisha uwe na familia. Fedha si kitu

mangosongoo

JF-Expert Member
Oct 2, 2016
257
456
Ndugu zanguni, maisha yanakwenda kwa kasi sana, na hatujui ya mbele yetu ni nini, yanaweza yakawa mazuri au mabaya japo katika kanuni ya maisha hatutakiwi kujitabiria mabaya.

Katika mazuri kunakufanikiwa kimaisha, kiuchumi, kifamilia, elimu na afya njema lakini katika mabaya nayakusikitisha kwa mwanadamu kuna magonjwa pamoja na vifo na mengineo.

Tukigeukia kwa upande wa mabaya, kijana umefikisha miaka 35 au zaidi au chini kidogo uwe na fedha au usiwe nazo na huna familia, wewe bado upo upo. Ulishawahi kukaa na kutafakari siku kwa bahati mbaya umeumwa ghafla ndani umezidiwa itakuwaje?

Sawa ndugu zako wa karibu watapata taarifa na watakusaidia lakini itafika mahali wanaweza choka na kujipoteza mmoja moja, kinachobaki ni kuanza kujuliwa hali kwa njia ya simu lakini familia yako, mke na watoto watakuwa hapo na wewe usiku na mchana kukupambania, hawatachoka na wewe. Tumeshuhudia haya katika jamii zetu zinazotuzunguka.

Vile vile unaweza kuwa na fedha nyingi mwisho siku zinaweza zisikusaidie pia ukiwa kitandani. Hili ni jambo la kufikiria sana na kulipa umakini mkubwa. Sisi wanaume kuna namna tunatakiwa tufikirie sana.
 
Ndugu zangun,maisha yanakwenda kwa kasi sana,na hatujui ya mbele yetu ni nin, yanaweza yakawa mazuri au mabaya japo katika kanuni ya maisha hatutakiwi kujitabiria mabaya. Katika mazuri kunakufanikiwa kimaisha,kiuchumi,kifamilia, elimu na afya njema lakini katika mabaya nayakusikitisha kwa mwanadamu kuna magonjwa pamoja na vifo na mengineo .Tukigeukia kwa upande wa mabaya, kijana umefikisha miaka 35 au zaidi au chin kidogo uwe na fedha au usiwe nazo na huna familia ,wew bado upoupo ulishawai kukaa na kutafakari je siku kwa bahati mbaya umeumwa gafla ndani umezidiwa itakuwaje?
sawa ndugu zako wakaribu watapata taarifa na watakusaidia lakin itafika mahali wanaweza choka nakujipoteza mmoja moja, kinachobaki nikuanza kujuliwa hali kwanjia ya simu lakin
familia yako mke na watoto watakuwa hapo na wew usiku na mchana kukupambania hawatachoka na wew. Tumeshuhudia haya katika jamii zetu zinazotuzunguka
Vile vile unaweza kuwa na fedha nyingi mwisho siku zinaweza zisikusaidie pia ukiwa kitandani, Hili nijambo lakufikiria sana nakulipa umakini mkubwa sis wanaume kuna namna tunataikiwa tufikirie sana...
Mkuu kwa hiyo unataka watu wawe na familia ili familia ije kuwasaidia siyo?

Familia iwe kama bima ya kumsaidia mtu akiwa katika matatizo, siyo?
 
Hao watot wa kukusaidia wanaweza wakawa Busy na Familia zao, hku upande Mkeo nd Kabsa akawa anakuhudumia kwa manyanyaso makubwa,

Cha msingi Tafuta hela ztakusaidia uzeeni maana Ht ukiumwa utakuwa na uwezo wa kuajiri watu na watakuhudumia kwasabb nd itakuw kazi Yao Ya kuwaingizia kipato.

Tofaut na Mkeo au watt wanawez wakakuzira tu maan huwalipi chchte watafany tu kama Msaada maan hawan cha kupoteza kwako,

Point yangu ni kwamba KATAA NDOA. Tafuta Hela itakutunza uzeeni na Ujanani, pia Usitegemee Wema kwa Wanadamu.
 
Mkuu kwa hiyo unataka watu wawe na familia ili familia ije kuwasaidia siyo?

Familia iwe kama bima ya kumsaidia mtu akiwa katika matatizo, siyo?
Bima ndio ndugu yako??

Ukitaka kujua umuhimu wa familia ukizeeka au kuugua.

Tembelea vituo vya malezi ya wazee.


Tembelea siku moja nyumba za kulea mapadre na masister wazee,vndio utajua ndugu zako ni watoto wako na wazee wako.
 
Bima ndio ndugu yako??

Ukitaka kujua umuhimu wa familia ukizeeka au kuugua.

Tembelea vituo vya malezi ya wazee.


Tembelea siku moja nyumba za kulea mapadre na masister wazee,vndio utajua ndugu zako ni watoto wako na wazee wako.
Una tabia za kijima bado.
 
binadamu ameumbiwa uwezo wa kushindwa kufanya lolote na kuweza kufanya maajabu na cha ajabu huwa anauwezo wa kukata tamaa na kujiua pale anapokumbwa na makubwa au vice versa ko ndugu mwandishi ucjal majibu tunayo
 
Sawa!

Yote kheri,lakini nadhani hadi 35 kama mwanamme lazima uwe na alama umeweka Kwenye jamii,familia ni identity muhimu sana!!

SWALA LA msaada ni kumuomba Mungu tu, HUWEZI JUA msaada utatoka wapi mkuu coz WANAUME tunahitajika Kwenye jamii HATUPENDWI MKUU,TRUST HATUPENDWI LABDA MAMA YAKO MZAZI TU!!

Ukishapoteza ushawishi Kwenye familia yaani aidha ugonjwa wa MUDA mrefu au uzee au kifungo cha maisha you are done trust me!!

Huyo mkeo sio wa kutilia maanani unapokua Katika hali ya kushindwa mkuu,watoto nao tunalea lakini WAKIKUA watasema HAKUNA KAMA MAMA yaani we shinda juani,waza sana fanya vyovyote vile lakini kuhusu upendo wa watoto KWA baba utategemea roho ya mama ilivyo kukuelekea kipindi hicho!!!

ENDELEA KUOMBA MUNGU MKUU MAMBO NI MENGI SANA!!
 
PESA NA FAMILIA havitenganishwi. Maisha ya sasa familia bila pesa ni kutafuta majanga.
Tuko nyakati ambazo pesa inapendwa kuliko MUUMBA.
 
PESA NA FAMILIA havitenganishwi. Maisha ya sasa familia bila pesa ni kutafuta majanga.
Tuko nyakati ambazo pesa inapendwa kuliko MUUMBA.
Huo ndio mtihani mkubwa katika maisha yetu
Pesa haitatuacha salama
 
Ndugu zanguni, maisha yanakwenda kwa kasi sana, na hatujui ya mbele yetu ni nini, yanaweza yakawa mazuri au mabaya japo katika kanuni ya maisha hatutakiwi kujitabiria mabaya.

Katika mazuri kunakufanikiwa kimaisha, kiuchumi, kifamilia, elimu na afya njema lakini katika mabaya nayakusikitisha kwa mwanadamu kuna magonjwa pamoja na vifo na mengineo.

Tukigeukia kwa upande wa mabaya, kijana umefikisha miaka 35 au zaidi au chini kidogo uwe na fedha au usiwe nazo na huna familia, wewe bado upo upo. Ulishawai kukaa na kutafakari siku kwa bahati mbaya umeumwa gafla ndani umezidiwa itakuwaje?

Sawa ndugu zako wakaribu watapata taarifa na watakusaidia lakini itafika mahali wanaweza choka na kujipoteza mmoja moja, kinachobaki nikuanza kujuliwa hali kwa njia ya simu lakini familia yako, mke na watoto watakuwa hapo na wewe usiku na mchana kukupambania, hawatachoka na wewe. Tumeshuhudia haya katika jamii zetu zinazotuzunguka.

Vile vile unaweza kuwa na fedha nyingi mwisho siku zinaweza zisikusaidie pia ukiwa kitandani. Hili ni jambo lakufikiria sana na kulipa umakini mkubwa. Sisi wanaume kuna namna tunataikiwa tufikirie sana.
Hata huyo mke anaweza kuchoka na kukukimbia vile vile
 
Watu Kama wewe tumeshawaona sana. Mtaishia kulelewa na mayaya wabeba box kutoka Africa huku mkikohoa na kuwatemea mahohozi ya masigara.
Mpaka hapo umesha assume wakati hunijui.

Nakwambia una mawqzo ya kijima sana.
 
Yaani kuna wanayafanya maisha kuwa magumu sana kwenye fikra zao na wanataka kuzihamisha fikra hizo kwa wenzao ili kushare nao stress......

Kwanza kabisa maisha hayana manual book... unaweza ukahitaji kufanya jambo fulani kwenye maisha kwa nyakati fulani lakini mazingira yakakuwia magumu.......

Asilimia kubwa ya maisha ambayo watu wanaishi yapo kinyume na matakwa yao sio kwa kupenda bali kuna mambo hutokea hapo kati ambayo yapo nje ya uwezo wako

Kila mtu ana maisha yake na kitabu cha maisha na jinsi mambo yanavyomtokea maishani mwake na vimetofautiana mtu na mtu.....si vyema kuweka mbele mitazamo yako kwenye maisha ya wengine
 
Back
Top Bottom