Mwanaume kuzirazira sababu yake nini?

Mwanaume kuzirazira sababu yake nini?

mbona umehamia kwenye topic sasa !!??
kwahiyo haya leti amani tena now umehamia kwenye nguvu ""??
kuhusu swala la uwepo wa amani ulipaswa kusema yanaleta amani 50% ..then 50% nikaraha maana kuna watu wameshakufa na wengine kupata vilema kupitia hayo hayo mapenzi

kuhusu swali lako la uwepo wa jukwaa la MMU JF jukwaa hilo limewekwa kwa mantik pana ya watu kushare experience za mahusiano wanayopitia ama waliyowahi kupitia ..inaweza kuwa ni experiance nzuri ama mbaya ...na kwa uzoefu wangu nilioupata humu sehemu kubwa ya thread zilizopo MMU zimejaa malalamiko na kukuta tamaa kwa watu juu ya mapenzi "waweza kuon amani uliyokuwa unaizungumzia wewe ikiwatesa watu kwa kiasi kikubwa ..na hkunaga amani yenye mateso amani inapaswa kuwa na raha "
kama wewe huu uzi wako uliouleta hapa nao pia umejaa lawama kwa jamaa yko "'mpka umekaa na kuamua kuuleta huku ili kupewa ushauri means nijambo linalo kunyima amani flna furaha na kupelekea kuubabua moyo wako kama vile umelishwa tindikali "" so amani uliyokuwa unaizungumzia iko wapi hapo ..."" wanawake wengi wamezalishwa na kukimbiwa ..wengine wanatunza familia zao ..wengine wameshindwa na kuwa machokoraa wao na watoto wao "" kwahayo matukio bado hujanishawishi kuwa mapenzi huwa yanaleta amani kwa 100℅..mpak ukafikia hatua yakusema hakuna maisha bila mapenzi """wakati kina Nicola Tesla walikuwa hawana wake wala ma gf
great thinker
 
Kuwa na uwezo wa kujivalisha nguo mbili tatu
kununua smartfon na
kuweza kununua vocha
kulipa kakodi ka chumba haikufanyi wewe kujiona sasa umekomaa kiakili.

Japo vitabun wanasema mtoto ni mtu yeyote mwenye miaka chin ya 18.
Bas hiyo sentence ya mwisho ndo inayomatter
 
kununanuna tabia za kike. labda ni kitinda mimba huyo..

suala la kuwa na wivu sana yawezekana ni sababu anaamini sana maneno ya mtaani kuwa hakuna binti mwenye mpenzi mmoja tu.

ila la kutokuwa na stori jameni sio kila mtu muongeaji... japo kwa mpenzi wapaswa kujitahidi kidogo walau
 
kununanuna tabia za kike. labda ni kitinda mimba huyo..

suala la kuwa na wivu sana yawezekana ni sababu anaamini sana maneno ya mtaani kuwa hakuna binti mwenye mpenzi mmoja tu.

ila la kutokuwa na stori jameni sio kila mtu muongeaji... japo kwa mpenzi wapaswa kujitahidi kidogo walau
Kuongea na mpenzi wako kunaleta ukaribu hata kama sio muongeaji lkn mm naamini kwa MTU unaempenda utajikuta tu unaongea automatically
 
Kuongea na mpenzi wako kunaleta ukaribu hata kama sio muongeaji lkn mm naamini kwa MTU unaempenda utajikuta tu unaongea automatically
ni kweli.
ndiyo maana nikasema hata kama sio muongeaji ila kwa mpenzi wako utajitahidi tu...tena waweza kujishangaa au hata yeye akakushangaa jinsi unavyoweza ongea
 
(A)Anazirazira:

1.Ashakusoma unamtetemekea sana, akinuna tu unabembeleza mpaka anajisikia raha.Hakuna asiyependa raha, lazima anune kila siku.
2.Anatafuta upenyo wa kukuacha. Siku akizira usipobembeleza ndo hutomuona tena. Kuhakikisha hili, ebu siku moja akizira nawewe chuna umuone kama atatafuta namna ya kujirudi au atachuna.

(B)UKIMYA:

(i)Ni mtu wa kukaa kimya hadi umuongeleshe =ni tabia/haiba yake(personality), siyo muongeaji.Hii ndiyo sababu hata akipiga simu haongei sana.Hebu jaribu kuchunguza kama ni tabia yake au la kwa kuangalia anapokuwa na watu wengine either wanaume au wanawake kama pia huwa wanaanza kumuongelesha tu!

(ii)Anakupigia simu baada ya muda mrefu kupita = Anahitaji umuanze, hauko akilini mwake muda mwingi, anakukumbuka kwa nadra.


(C)"Umetoka kwa bwanako?".... Huku akichekacheka:

1.Hana wivu juu yako, yaani kwake ni kwamba mwanamme yeyote akupitie yeye sawa tu ilimradi na yeye anapata.
2.Hakuamini, kama ulivyokwisha ona.
3.Hatanii, anawasilisha ujumbe wake na hisia zake(vile anavyokufikiria) pasipo kutaka kusababisha ugomvi.

(D)Hakuamini kwa sababu:

1.Unatabia ambazo zinamtia shaka
2.Umewahi muonesha kuwa wewe siyo wa kuaminika, alikuamini lakini aliwahi kukuona ktk hali ambayo hakutegemea.
3.Hajiamini(Inferiority complex), anahisi wewe siyo level yake.

HITIMISHO:
(1)Mapenzi pasipo wivu, Hamna mapenzi hapo ni kusogeza tu siku....ukitaka utolewe roho mguse mke wa mwanamme(utashangaa kwanini nasema mwanamme) ndiyo, mwanamme yeyote hawezi vumilia aone mpenzi wake aliyenaye malengo na anayempenda anatumiwa na mwingine hawezi hata thubutu kukutania upuuzi huo asiopenda kuuona na akiongea "umetoka kwa bwanako" atakuwa ktk hasira na sio ktk kicheko. So, huyo in short hana malengo na wewe!

(2)Mawasiliano ni muhimu sana ktk mahusiano yoyote hasa ya kimapenzi! Ukiona haoni umuhimu wa kuzungumza na wewe basi haoni umuhimu wa kuyajenga na kuyadumisha mapenzi yenu.

(3)Ukimpenda mtu, muda mwingi anakuwa akilini mwako na ukim-miss unatamani hata usikie sauti yake tu....utapiga simu mara kwa mara, hasa mnapokuwa hampo pamoja!

Nimeongea si kama mwenye experience ktk mapenzi tu lakini pia kama psychologist!
 
kuna wakati mtu unakela anaamua kukaa kimya wewe una tafsiri kasusa.ama kutaka uanzwe wewe tu kupigiwa/kutumiwa msg jamaa akiuchuna unatafsiri kasusa.

ama mko kwenye mabishano akaamua kukupa ushindi kwa kukaa kimya tayar kasusa.kuna watu huwa hawapendi malumbano ana amua kukupa ushindi mapema
 
kuna wakati mtu unakela anaamua kukaa kimya wewe una tafsiri kasusa.ama kutaka uanzwe wewe tu kupigiwa/kutumiwa msg jamaa akiuchuna unatafsiri kasusa.

ama mko kwenye mabishano akaamua kukupa ushindi kwa kukaa kimya tayar kasusa.kuna watu huwa hawapendi malumbano ana amua kukupa ushindi mapema
Mkuu na kama kosa lake sasa pale mnaamua kuwekana sawa ye hataki kukubali kosa bas hapo atasusa na kuondoka hiyo imekaaje
 
Back
Top Bottom