Mwanasheria wa Wizara afichua siri nzito mkataba wa bandari

juma30

Senior Member
Jun 25, 2022
149
421
Mwanasheria wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mohamed Salum amesema mkataba baada ya kusainiwa Oktoba 25, 2022 ulipelekwa Bungeni Februari 2023 kwa ajili ya hatua za uridhiwaji ambapo alisisitiza kuwa kabla ya Azimio halijapelekwa Bungeni lilipitiwa na Mfumo mzima wa Serikali ambao ni Wakurugenzi wote wa Sera na Mipango (DPP) kutoka Wizara zote, Makatibu Wakuu wote wa wizara zote chini ya mwenyekiti wao Katibu Mkuu Kiongozi (CS) na Baraza la Mawaziri ambapo Rais ndiye Mwenyekiti ambapo wote kwa pamoja waliridhia mkataba huo kwenda Bungeni.



Mwanasheria wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mohamed Salum
 
Daah ila hawa jamaa 😪😪😪!! Halafu kwann baadhi ya machawa humu wanasema huo c mkataba while wahusika wanasema mkataba?

Sina baya na nyie lkn tuelezen nan aliwaambia mje mseme sio mkataba au ni posho ndio uliwatoa ubongo wote? Naomba mtoe maelezo nyie... Cc Lord denning Faizafoxy covax HIMARS choiceVariable
 
Mmmh🥺🥺🥺

Jamaa kavimba balaa. Sijui ni mazoezi kunyayua vyuma huko Gym au mazoezi ya kunyanyua magunia ya pesa za hongo za DP World..!!

By the way, amesemea wapi haya? Mahakamani huko Mbeya kama shahidi upande wa utetezi au?

Na hivi huo ni makataba au makubaliano?
 
26 July 2023

Wakili wa serikali wakiwa na waandishi wa habari wakihojiwa nje ya mahakama kuu kuhusu mwenendo wa kesi

Mawakili wa serikali wadokeza njia ya suluhisho la kisiasa yaani muafaka - political solution kwa sakata la bandari, waomba wananchi warudi mezani kuongea na mheshimiwa rais kwani Mheshimiwa Rais ameonesha nia kusikiliza maoni

1690477864420.png


Chonde chonde kuna njia ( option) ya kurudi mezani, mawakili wa serikali wasema
 
Mwanasheria wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mohamed Salum amesema mkataba baada ya kusainiwa Oktoba 25, 2022 ulipelekwa Bungeni Februari 2023 kwa ajili ya hatua za uridhiwaji ambapo alisisitiza kuwa kabla ya Azimio halijapelekwa Bungeni lilipitiwa na Mfumo mzima wa Serikali ambao ni Wakurugenzi wote wa Sera na Mipango (DPP) kutoka Wizara zote, Makatibu Wakuu wote wa wizara zote chini ya mwenyekiti wao Katibu Mkuu Kiongozi (CS) na Baraza la Mawaziri ambapo Rais ndiye Mwenyekiti ambapo wote kwa pamoja waliridhia mkataba huo kwenda Bungeni.

View attachment 2700695
Mwanasheria wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mohamed Salum
Mbona kavimbiwa? Huyu atakuwa mmojawapo wa matapeli wameokotwa huko mitaani tu. Hakuna mwanasheria anayetumia akili yake halafu akawa na mwili uliotuna hivyo.
 
Nukta zinaanza taratibu kutengeneza mstari. Kutumbuliwa kwa Eric Hamis kwenye nafasi ya ukurugenzi wa bandari inawekana kuwa adhabu kwa kosa la kuwazungusha wawekezaji wa DPW....

w.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/rais-samia-atengua-uteuzi-wa-mkurugenzi-mkuu-tpa--3868580
 
Back
Top Bottom