Kuna ombwe la hekima na busara katika vichwa vya watu waotutawala.Sio bure!
Hivi kuweza kujua kipi cha kuongea, kwa namna gani,mahali gani, kwa nini na kwa matokeo gani kunahitaji ''Semina Elekezi'' ama kuyaelewa maudhui ya kitabu cha Azimio la Arushwa kuhusu ''Maadili ya Uongozi''?
Kwa nini nchi hii haiachi kuzalisha walevi waliokubuhu wa madaraka?
Ufahamu kidogo tu juu ya dhana ya ''utawala wa sheria'' na ''utawala bora'' ungemwelekeza Ndugu DC,ikiwa kweli ana madai ya msingi, kwenda mahakamani na/au katika vyombo vya Kitaaluma kuhoji Elimu ya mhusika na yeye angeisaidia mahakama kuthibisha madai yake hayo.(Ingawa ni wazi angepata tabu sana kuweka ushahidi usioacha shaka).
Pole sana dada Mwanasheria!Hatupendi kabisa unyanyasaji.