Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari awasilisha muswada wa marekebisho ya Sheria Tisa (9) Bungeni, agusa Bandari na Uhujumu Uchumi

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari awasilisha muswada wa marekebisho ya Sheria Tisa (9) Bungeni, agusa Bandari na Uhujumu Uchumi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari akiwasilisha maelezo ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2025 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2025) Juni 5, 2025 Bungeni Jijini Dodoma.

Aidha mara baada ya kuwasilisha maelezo hayo, Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Seif Gulamali aliwasilisha maoni ya Kamati hiyo kuhusu Muswada huo.

1749191316276.png
Muswada huo ambao umesomwa Mara ya Pili Bungeni unatarajiwa kujadiliwa na hatimaye kupitishwa na Waheshimiwa Wabunge.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Muswada huo unapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria Tisa (9) ambazo ni:-

(a)
Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Uhalifu wa
Kupangwa, Sura ya 200;
(b) Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa
Serikali, Sura ya 177;
(c) Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za
Viwandani na Majumbani, Sura ya 182;
(d) Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini, Sura ya 413;
(e) Sheria ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Sura ya 150;
(f) Sheria ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya
Binadamu, Sura ya 59;
(g) Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Sura ya 268;
(h) Sheria ya Bandari, Sura ya 166; na
(i) Sheria ya Leseni za Usafirishaji, Sura ya 317.
 

Attachments

Hatuwezi kuamini chochote hapo maana mkataba wa bandari aliuandaa yeye tena akiwa mamlaka tofauti. Sasa amekaa hapo kusisitiza na kuharalisha mabaya yote ya mkataba. Sijui kama wabunge wetu wataliona hilo..
Wacha wao wawe Malaika na sisi tubaki mashetani Kawa walivyosema wao jana
 
@TLS take note kuona kama kuna upuuzi wa kuongeza sheria kandamizi
 
Back
Top Bottom