Mwanahalisi leo latoboa ile ya ndani kabisa ya EPA!

Hivi unafikiri kweli wale maelfu waliojazana Jangwani kwenye mkutano wa CCM hawajui ufisadi unaofanyika nchini? Really..?
Kwani maana ya magazeti ni nini, wewe unayetuletea mashairi yako na kutuimbia nyimbo kila siku unafikiri unachotuambia hatukijui, so if that keep quite don't bring us your stories, kwa sababu kila kitu tunakijua au ni kipya gani unachokijuwa wewe sisi hatukijui. Habari ni pamoja na kukumbushana.
 
This is very good answer to the gentleman yeye anadharau makala za wenzake anafikiri za kwake huwa zinatusaidia sana wakati tunajua nyimbo ni zile zile tofauti ni choirmaster tu, haa haa haaaa big up Edson.
Tatizo lenu mnakurupuka kujibu bila kuelewa yaliyoandikwa yana maana na mantiki gani! You have to learn to read between the lines. Jifunze kuiangalia sentensi ama maandishi kwa mapana na marefu yake. Sioni mahali ambapo MMKJ amekosea katika kuuliza swali alilouliza. Mnaotofautiana naye mnatakiwa kusema kwa mtazamo wenu ni vipi makala hiyo inaweza kusaidia? Wenzenu wanajibu hoja ipasavyo ninyi mnakurupuka kumrushia madogo MMKJ!
 
Hivi unafikiri kweli wale maelfu waliojazana Jangwani kwenye mkutano wa CCM hawajui ufisadi unaofanyika nchini? Really..?

Wanajua sana kwa vile wenggi wao wamenufaika kwa namna moja au nyingine.....khanga,pilau,cash.....mtuhumiwa mmoja wa ufisadi nasikia alichukua wazee kama 100 kuwapeleka Mecca kuhiji....akajenga na misikiti...anaitwa Maranda....:becky::becky:
 
Tatizo lenu mnakurupuka kujibu bila kuelewa yaliyoandikwa yana maana na mantiki gani! You have to learn to read between the lines. Jifunze kuiangalia sentensi ama maandishi kwa mapana na marefu yake. Sioni mahali ambapo MMKJ amekosea katika kuuliza swali alilouliza. Mnaotofautiana naye mnatakiwa kusema kwa mtazamo wenu ni vipi makala hiyo inaweza kusaidia? Wenzenu wanajibu hoja ipasavyo ninyi mnakurupuka kumrushia madogo MMKJ!
Wewe ndio hujui kinachozungumzwa, unakubaliana na MKJJ habari za ufisadi zinatosha sasa watu waache kuleta evidence na facts, mbona yeye anatuletea habari ambazo hata sisi tunazielewa. Wakati anatuimbia utenzi wa Loliondo unafikiri nani alikuwa hajui tukio la Loliondo basi na yeye asituletee tena habari tunazozijua imetosha simple.
 
CCM sijui kama wanadhani sasa Watanzania kwa asilimia fulani wanajua kusoma na kuyajadili mambo. Wamezoea tu kuwaburuza lakini this will not be forever! The time is coming and is approaching very fast. Change is coming to Tanzania and it will not take a generation or a decade. There is a lot desired to be changed and there is a lot desired to be questioned and correct answers provided.
 
Hivi iwapo mshitakiwa wao mmoja kanena, kwa nini CCM bado wanawafanya Watanzania wote mafala? Kwa nini jamani?
 
Nilisoma Hilo Gazeti ila pale kwa Tindu Lisu ndipo palikuwa patamu jamani JK nae mmmmmh hapa kuna Filimeeeeee inachezwa na kama hayo ni kweli si shindwi shangaaa kuona makamba kila kukicha akiongea pumba tuuuuu na CCM ndani hawasemi kitu na kuna wasomi haswaaaa walio enda vidato vya kutosha na sasa wameamua kuigeuza siasa kwa manufaaa yao na sio kwa watanzania
 
kwa kwei namshangaa sana mtu anayeona swala la EPA ni historia, yeye ndio historia, na ni vizuri na yeye pia tukamuomba anyamaze kwakuwa si mmojawetu, na hivyo ndivyo watu hawa na nduguze wa CCM wanavyotaka tuamini, tuwe wajinga na waendelee kutumia upumbavu wetu kama mtaji wao, jamani sisi wengine tumeshakataa kutumika. Napenda kumkatisha tamaa kwamba EPA bado ni moto na hautasimika wameuwasha watauzima, watapelekwa tu mahakamani hakuna kukwepa, na JK anajua hilo na ndio maana haachi kuanguka bila kuguswa, keshaguswa his innermost part. Wewe umeona wapi watu wanakula mpaka hela za barabara za kijijijini kwao, can you imagine? hiyo inatofauti gani na mkulima wa muumini mwinjuma aliyekula mbegu anataka kutuua njaa, sasa wanaua wakwere wenzao ndio maana hawaoni tabu kupeleka kodi yetu kwenye kampeni ka kupitia akaunti ya familia, hayo mabango mabaya yasiyo na concept na yenye the poorest rejected quality in a normal market, wamepeleka kazi ufaransa sijui china (tutajua tu ni wapi) na kuwadhulumu vijana wote wa kariakoo, gerezani etc biashara waliyoizoea, ya hela zao wenyewe. Waende waende, watangulie kama mwalimu, hatuwahitaji
 
Kwa kwei namshangaa sana mtu anayeona swala la EPA ni historia, yeye ndio historia, na ni vizuri na yeye pia tukamuomba anyamaze kwakuwa si mmojawetu ..... Napenda kumkatisha tamaa kwamba EPA bado ni moto na hautasimika wameuwasha watauzima, watapelekwa tu mahakamani hakuna kukwepa, na JK anajua hilo na

.... And you shall all come to agree that...EPA is the main determinant factor in the future of JKK and the final results in the coming election.... Hakuna kingine kitakacho kuwa na nguvu kama hiki... so EPA iko haiiii inapumzi kuuu!!!

 
Nimesoma hiyo stori, naona wameandika yale aliyosemaMarando pale Jangwani na sioni kama Mwanahalisi wamefanya uchunguzi mpya; kama kuna tofauti na yale tunayoyajua basi yaleteni hapa jamvini.
Vinginevyo wataalamu wa propaganda wanasema habari ukiirudia sana ndio watu polepole wataikubali. Hivi Chadema wana uwezo wa kutosha kununua media ya Bongo? hii itakuwa kungojea Mwanahalisi mara moja kwa wiki na nonavyo mimi gazeti hili linashabikia zaidi habari za upande mmoja na kunyamazia mapungufu ya upande mwingine.
 
Wewe ndio hujui kinachozungumzwa, unakubaliana na MKJJ habari za ufisadi zinatosha sasa watu waache kuleta evidence na facts, mbona yeye anatuletea habari ambazo hata sisi tunazielewa. Wakati anatuimbia utenzi wa Loliondo unafikiri nani alikuwa hajui tukio la Loliondo basi na yeye asituletee tena habari tunazozijua imetosha simple.

Mr Quinine..naona hukumwelewa vizuri MMKJJ. Hakuwa na maana uliyoipokea wewe. Wnajamii wengine wamemwelewa vyema na kwahiyo wanajaribu kutoa majibu yanayolenga shabaha ya swali lake.

Wakati mwingine kuelewa ujumbe huwa si rahisi na hili ndio chanzo cha tofauti zetu nyingi. Mfano watu wanasoma na kunukuu msahafu wa Kuran moja lakini bado kuna wa-Suni, wa-Hamadiya na wa-Shiya nk, na wale wanaonukuu msahafu wa Biblia ileile lakini wanatofautiana kuelewa matokeo yake ni tofauti za imani mf. wa-Ltheri, wa-Anglikan, wa_catholic nk.

Tuoneshe uvumilivu wetu, tuchange mawazo yetu kwa ajili ya nchi yetu.
Sungura
 
thats exactly my point.. ndio maana sikuhizi kwa kweli sihangaiki kufichua ufisadi zaidi kwa sababu tumeshapigwa ganzi.. sasa hivi ni kujipanga kuushughulikia tu.. Tangu Loliondo hadi leo bado tupo hapo hapo.. kashfa kashfa kashfa..

Hizi ni dalili za kukata tamaa na nasikia hakuna dhambi kubwa kama kukataa tamaa - ni kujiua!
 
Nimesoma hiyo stori, naona wameandika yale aliyosemaMarando pale Jangwani na sioni kama Mwanahalisi wamefanya uchunguzi mpya; kama kuna tofauti na yale tunayoyajua basi yaleteni hapa jamvini.
Vinginevyo wataalamu wa propaganda wanasema habari ukiirudia sana ndio watu polepole wataikubali. Hivi Chadema wana uwezo wa kutosha kununua media ya Bongo? hii itakuwa kungojea Mwanahalisi mara moja kwa wiki na nonavyo mimi gazeti hili linashabikia zaidi habari za upande mmoja na kunyamazia mapungufu ya upande mwingine.


Ukiisoma vizuri stori utakuta kwamba yaliyoandikwa ni zaiodi ya yale Marando aliyosema jangwani. haya ya Jeetu Patel kukataa kurudisha hela za EPA kwa kuwa alishawapa CCM asilimia 60 ya jumla alizokwapua ni habari mpya, pamoja. Pia Mwanahalisi inatuambia kuwa maelezo haya ya Jeetu yamo katyyika hati yake ya kiapo aliyotoa kwa kamati ya Rais iliyopewa jukumu kuchunguza suala la EPA baada ya yeye Rais kukabidhiwa ripoti ya wakaguzi wa nje katika BoT -- Ernst & Young.
 
CCM sijui kama wanadhani sasa Watanzania kwa asilimia fulani wanajua kusoma na kuyajadili mambo. Wamezoea tu kuwaburuza lakini this will not be forever! The time is coming and is approaching very fast. Change is coming to Tanzania and it will not take a generation or a decade. There is a lot desired to be changed and there is a lot desired to be questioned and correct answers provided.
Wanasema "You can fool some people all the time. But you can not fool all the people all the time".

Let's wait and see if Tanzanians are not ready to be fooled all the time. October 31 is not that far.
 
kama Mungu angetufunua vichwa na kuiweka ndani
akili ya uelewa wa ndani dhidi ya kitu kinaitwa ccm? hili lingetusaidia
kutoa adhabu juu ya hii kitu ccm, maana imeyafanyia conspiracy sana
maisha ya wanyonge wa tanganyika, Mungu awalaani woote,
waundao hii kitu.
 
Back
Top Bottom