sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,034
Maana nashangaa nashindwa kuelewa watu wanawaitaje hawa watu magenius na utawalinganisha vipi na wale ambao wanaweza kujifunza haraka bila kurudia rudia na wana msaada mdogo wa material na walimu.
Unakuta mwanafunzi topic 1 tu anaiwekea nguvu kubwa mnooo! Yaani anairudia rudia sana ili iwe kama chorus, muda huo kuna vitabu vingi vya yeye kuelewa zaidi, hapo kuna walimu wapo muda wowote na tena wamejikita kuwafundisha namna ya kujibu maswali ya kwenye mtihani. Kwa huyu mwanafunzi hadi anakaribia mitihani yake kuna kipya kipi hapa zaidi ya kwenda kurudia kiitikio?
Hapo sasa upande mwengine unakuta kuna mwanafunzi ambae kitabu alichonacho ni cha kuazima, walimu wanafundisha tu darasani hakuna msaada baada ya hapo, ni yeye kuamua asome au apuuzie hakuna wa kumcontroll, mwanafunzi huyu unakuta uwezo wake wa kujifunza haraka ndio unambeba na pia uwezo wa kutatua maswali mapya unamsaidia kujibu maswali ambayo anakutana nayo kwa mara ya kwanza.
Hapo yupi ni genius, kasuku wa kurudia kiitikio ama huyo anaeweza freestyle kutoka kichwani papo hapo?
Unakuta mwanafunzi topic 1 tu anaiwekea nguvu kubwa mnooo! Yaani anairudia rudia sana ili iwe kama chorus, muda huo kuna vitabu vingi vya yeye kuelewa zaidi, hapo kuna walimu wapo muda wowote na tena wamejikita kuwafundisha namna ya kujibu maswali ya kwenye mtihani. Kwa huyu mwanafunzi hadi anakaribia mitihani yake kuna kipya kipi hapa zaidi ya kwenda kurudia kiitikio?
Hapo sasa upande mwengine unakuta kuna mwanafunzi ambae kitabu alichonacho ni cha kuazima, walimu wanafundisha tu darasani hakuna msaada baada ya hapo, ni yeye kuamua asome au apuuzie hakuna wa kumcontroll, mwanafunzi huyu unakuta uwezo wake wa kujifunza haraka ndio unambeba na pia uwezo wa kutatua maswali mapya unamsaidia kujibu maswali ambayo anakutana nayo kwa mara ya kwanza.
Hapo yupi ni genius, kasuku wa kurudia kiitikio ama huyo anaeweza freestyle kutoka kichwani papo hapo?