Hii ndio sababu ya baadhi ya wanafunzi wa Saint Francis na shule za seminari kupungua uwezo darasani wakienda shule nyingine form 5 ama chuo

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,080
Kufaulu kwao kunashangaza wengi na wala hawanunui mitihan bali wanafanyiwa michujo mkali sana, yani ile ininterview ya kuingia tu watoto wanaweza kuwa elf 3 ambao ni vipanga wote ila wanahitajika 100 tu, yaani mtoto kuingia tu hapo inabidi awe kipanga na bado kuna michujo mikali ya maksi za juu sana, inaendelea wakianza shule, hadi mtoto aweze kufuzu kufanya mtihani wa kidato cha nne kapambana sana.

mfumo wao wa usomaji ni tofauti, mfumo wao unamlazimu wanafunzi kujua namba ya kujibu mitihani muda mwingi tangu akiamka hadi kwenda kulala, mazingira yao ni mazuri ila ni kwajili ya kujua mtindo wa kujibu maswali sio kula upepo ama kuotea jua ama michezo, testi kibao za kuzoesha wanafunzi kuweza kujibu mtihani, nadhani hata ukifeli likizo unaweza ukabaki shule ili upigwe brashi kujifunza mtiririko mzuri wa kujibu maswali ya necta, usipofikisha wasatani wa shule umekwenda, bonasi na zawadi nono pindi matokeo yakitangazwa zinawapa walimu presha kubwa kuhakikisha wanakomaa na wanafunzi wao mpaka kieleweke .

Mpaka kufikia form 4 kwenye mwezi wa sita ule kila mwanafunzi anakuwa kama kasuku, yaani kuanzia definition, factors,advantages, feautures, n.k. wanaweza kuzijibu kama mashine ya kutoa kopi, past papers wanakuwa wameshasolve zimekuwa kama kiitikio cha muziki hakuna swali jipya mbele yao, wanachosubiri hapo huwa ni kulishangaza taifa kwa msururu wa division 1 za single digit.

Tatizo linaanza hao wanafunzi wakienda shule nyingine advance ama chuoni ukikutana nao wanarelax kwasababu hawakutani tena na heka heka za kubanwa ama mazingira ya kulazimishwa kusoma kama mwanzo.

Wanakuwa na uhuru kwa mara ya kwanza baada ya msoto mkali ndio mana wanaanza kufel, hawajazoea uhuru tofaut na wanafunzi wengine waliotoka shule za kawaida wakiwa na uhuru na bado wakatoboa, kwao uhuru ni kitu cha kawaida tofaut na wale wa saint francis ambao walikuwa wanatumia muda mwingi kusoma
 
Kufaulu kunaanzia katika mindset ikiwa ukiwa form five na ukaweka katika Akili yako kuwa utapata one ya 3 hilo jambo lazima litatokea .

Ukiachana na kusoma Sana katika mazingira mazuri bado mindset itachukua nafasi kubwa katika kufanikiwa au kutofanikiwa .

Na jambo la mwisho ni "People you hang out with" Kama wapo negative watakubomoa mapema
 
Kufaulu kwao kunashangaza wengi na wala hawanunui mitihan bali wanafanyiwa michujo mkali sana, yani ile ininterview ya kuingia tu watoto wanaweza kuwa elf 3 ambao ni vipanga wote ila wanahitajika 100 tu, yaani mtoto kuingia tu hapo
na mwafrika ana matatizo, asipobanwa hatekelezi wajibu wake.

angalia utawala huu watu walivyojiachia, ni kuiba tu feza za walipa kodi. kumbe tunahitaji kiongozi dikteta hata kama ni uchwara!
 
na mwafrika ana matatizo, asipobanwa hatekelezi wajibu wake.

angalia utawala huu watu walivyojiachia, ni kuiba tu feza za walipa kodi. kumbe tunahitaji kiongozi dikteta hata kama ni uchwara!
Hata wahindi, wachina, n.k. ndio wanaongoza kwa kuelimika zaidi mpaka marekani, nao huwa wanasoma kwa kubanwa sana hasa wahindi
 
Kwa kweli, nimekuja chuo nimekua dunya wa darasa

Kipindi hicho tengeru boys nilikua kipanga, nakumbuka interview tulifanya 8k, tukaingia 187

Tulikua tunabanwa sana, ukifeli likizo ya septemba unabaki shule, usipofikisha avg ya shule mwisho wa mwaka unafukuzwa

mda wowote mtihani inaitwa special exams

saivi niko free nazungusha tu, kuna wenzangu washapata watoto kabisa
 
Hiyo shule ni kutudhalilishia tuu watoto wetu..wakikosa intavyuu waonekane hawana akili..
Ila yote fainali chuoni...tunakutana vyuoni hakuna cha wa Feza au st francis au Kayumba yani hapo tunaaanza upyaaaaaa
Sio chuoni ni advance, nilikutana na wanafunzi km 4 class kutoka shule ya private tena walikuja na 1 ya single digit, sisi tuliotoka kayumba tuliwaburuza, m1 alihama mapema, wa3 tulimaliza nao mie mwenyewe niliwakata necta ACSSE.

huwa hawana maajabu na wanashangaza kwa kweli.
 
Sio chuoni ni advance, nilikutana na wanafunzi km 4 class kutoka shule ya private tena walikuja na 1 ya single digit, sisi tuliotoka kayumba tuliwaburuza, m1 alihama mapema, wa3 tulimaliza nao mie mwenyewe niliwakata necta ACSSE.

huwa hawana maajabu na wanashangaza kwa kweli.
Ulisoma Kayumba kuanzia primary?
 
Kwa kweli, nimekuja chuo nimekua dunya wa darasa

Kipindi hicho tengeru boys nilikua kipanga, nakumbuka interview tulifanya 8k, tukaingia 187

Tulikua tunabanwa sana, ukifeli likizo ya septemba unabaki shule, usipofikisha avg ya shule mwisho wa mwaka unafukuzwa

mda wowote mtihani inaitwa special exams

saivi niko free nazungusha tu, kuna wenzangu washapata watoto kabisa
Usijiachie san ila kama watu wangekuwa wanafuata zile sheria na taratibu za boarding chuo wangefaulu sana.
 
Sio chuoni ni advance, nilikutana na wanafunzi km 4 class kutoka shule ya private tena walikuja na 1 ya single digit, sisi tuliotoka kayumba tuliwaburuza, m1 alihama mapema, wa3 tulimaliza nao mie mwenyewe niliwakata necta ACSSE.

huwa hawana maajabu na wanashangaza kwa kweli.
Ooh hivi hapo st Francs hawana Advance...ndo wanapofeli sasa wtt wakitoka hapo wanaenda wapi na walivyo wa moto...
 
Ooh hivi hapo st Francs hawana Advance...ndo wanapofeli sasa wtt wakitoka hapo wanaenda wapi na walivyo wa moto...
Pale hakuna advance, wengi wao huwa wanaenda shule za private zenye advance, ila wanaoenda GVT ni utawakuta Tabora girls, Msalato, na kilakala.

Sasa angalia wakiwa hapo shule za GVT ni full tafrani.
 
Back
Top Bottom