Mwana JF share weakness yako

Mwana JF share weakness yako

TIME MANAGEMENT: wenzangu huwa wanalalamika kuwa: hivi wewe ukoje tukisema mkutano saa kumi kamili wewe unakuja kweli hiyo saa kumi, sisi tulimaanisha saa kumi ya Kiswahili, na wewe umezidi kuzingatia muda,uwe unachelewa bwana!😉 kwa hiyo mie naichukulia kama weakness kwa jamii, lakini kwa upande mwingine kwangu ni strength
 
Mtoto teketeke yan mlaini kila sehem panatingishika huwa cjiwez hata akiwa na sura kama bablevo.

Then upole
 
udhaifu wangu ni moyo wa kusaidia pamoja kuamini mtu kwa haraka, ingawaje mda mwingine inanigharimu sana
 
Bwana Yesu asifiwe wapendwa,

Kama tunavyojua kwamba kila binadamu anaeishi chini ya jua ana mapungufu (No one is perfect under the sun). Mapungufu yetu au weakness zetu zinatusababishia hasara nyingi kuliko faida

Kwa upande wangu weakness inayonitesa zaidi ni Haya. Imenikosesha marafiki na fursa mbalimbali za maendeleo.

Mwana JF share weakness yako na madhara yake.
Mie kila mwanamke mzuri nataka awe wangu!sijui hata nifanyeje...
 
udhaifu wangu ni moyo wa kusaidia pamoja kuamini mtu kwa haraka, ingawaje mda mwingine inanigharimu sana
tunafanana udhaifu na huwa nashindwa mtu kila mara namfuatilia anilipe deni,
 
1.Mimi napenda kweli na siwezagi kumfichia hisia mwanamke ambaye she keeping it 1 hunnit. I do turn to be super romantic and they always take it as an advantage.

2.Sipendi uswahili hasa kwa mtu asieweza kutimiza ahadi zake, excuses zisizo na mwisho. Mtu asie na msimamo na mzito kuelewa ni ngumu sana mi kuivana nae.

3.Nina short temper, yani kukuchenjia ni dakika 0 mazee ila ni mwepesi sana kusamehe na huwa siwezagi kuweka kinyongo moyoni.Nakupa kavu na hasira ikiisha tu hapo hapo maisha yanaendelea.

4.Sijawahi na sina guts za kumpiga mwanamke licha ya kuwa nina hasira za karibu mno pindi nikikwazika.
Wewe mtu una tabia zangu 100%. Hio short temper imeni-cost sana.
 
Pole kuwa na roho mbaya japo kidogo lakini angalia nayo isikugharimu kama inavyokugharimu huruma. Kama unaweza kufafanua huruma kwenye mambo yapi?

Huruma, inanicost sana.
 
Pole kuwa na roho mbaya japo kidogo lakini angalia nayo isikugharimu kama inavyokugharimu huruma. Kama unaweza kufafanua huruma kwenye mambo yapi?
Hahaaaaa!!! Hivi kumbe unaweza kujifunza kuwa na roho mbaya!! Hebu nipe hints.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Opposite ya huruma atoto, pale unapotaka kufanya kitu kwa huruma zako geuza kibao na uweke roho mbaya lol!

Hahaaaaa!!! Hivi kumbe unaweza kujifunza kuwa na roho mbaya!! Hebu nipe hints.
 
Opposite ya huruma atoto, pale unapotaka kufanya kitu kwa huruma zako geuza kibao na uweke roho mbaya lol!
Najiapizaga kabisa, ila ndio najikuta huruma ishaniingia na ndio basi tena.

Nishawahi kumlipia mwanafunzi anayeishi katika mazingira magumu ada baada ya kurudishwa akawa analia sana, kipindi hicho ndio nimeajiriwa alafu ndio ilikuwa pesa pekee niliyobakiwa nayo na sina means nyingine yoyote ya kupata pesa na siwezi kuomba. Huo ni mfano mmoja tu.
 
Back
Top Bottom