Mwana FA v/s Lady Jay Dee....!!!

Mwana FA v/s Lady Jay Dee....!!!

... Mimi nauza nyanya, kwanini na wewe uje kuuza nyanya karibu yangu?...
Unauzia wapi nyanya zako mkuu? Kwa hakika sio kariakoo! Mbona baishara ndio zilivo hivyo kwa clusters?

Ni suala la ushindani tu kama katika biashara nyingine. Actually, msingi wa sheria ya ushindani wa biashara ni kumnufaisha mlaji. Uwepo wa show hizo mbili (mimi naamini zitakuwa zaidi ya mbili siku hiyo) kwa siku moja unawapa "walaji" choice na pia inapunguza bei kwa sababu hakuna mmoja ambaye atakuwa na nguvu ya kuhodhi (monopolistic) na hivyo kujipangia bei atakayo.

Btw, Jide ni mmoja wapo ya wanamuziki ninaopenda miziki yao. Napenda pia mashairi/mistari ya MwanaFA.
 
kuna wakati unaweza kumshangaa mtu sana,ukajaribu kufikiria akili yake imewaza nn,ukabaki huna jibu,kwa elimu yake,na heshima yake FA amefanya kitu cha ajabu sana,hatutamuelewa wala hataeleweka,wacheni kutetea upuuzi! Vitu vilivyotakiwa kuwaunganisha,ndio vinawafanya watengane!mbona bongo movies wako poa tu?
 
Ni kweli sijafuatilia. Ni kweli kuna bifu kati ya JD na Clouds.

Je ni kweli kuna bifu kati ya MwanaFA na Jide? Kuna kosa gani kwa Jide kufanya biashara siku ambayo MwanaFA pia anafanya biashara? Ni kwa nini Jide akifanya show yake, MwanaFA "hatakiwi" kufanya show yake?Je ni kweli kuwa siku hiyo wanamuziki wote hawatafanya show zao isipokuwa Jide na MwanaFA? Labda mtueleweshe vizuri eneo hili sisi ambao hatufuatilii haya mambo ya wanamuziki kila siku.

1. Ni kweli kwamba Jide haba bifu na MwanaFA, na MwanaFA anaweza kufanya show yake any day hata kama inagongana na ya Jide.

2. Ni kweli kwamba MwanaFA ni mmoja wa wakurugenzi kwenye taasisi ya THT (solely owned by Clouds FM owners), hope hili unalifahamu.

3. Kwa namba 2 hapo juu, kwa sababu ya uhusiano uliopo kati ya MwanaFA na Clouds FM unaweza ku-impair maamuzi ya MwanaFA juu ya upande upi awe kwenye hii bifu ya Clouds FM na Jide.

4. Moja ya mbinu Clouds FM wanazozitumia ni kumshindanisha Jide na wasanii wenzake au na bendi zingine, na hivyo ndivyo imekuwa kwa MwanaFA this time, hii show ya FA promoters wake ni Clouds FM kuanzia tarehe, matangazo, wasanii waandamizi, ukumbi mpaka kiingilio.

5. Last time Ruge alisema Skylite Band imepokea kijiti cha kuwa bendi pendwa kwao Coluds FM badala ya Machozi Band, so hii ni bendi nyingine inatumika kupambana na Jide (Mmiliki wa bendi ni Sebastian Ndenge kwa mujibu wa Ruge) na wameschedule ratiba y sawa sawa na Machozi Band.

NOTE: Ukisoma namba 4 hapo juu utakumbuka mbinu hii ilitumika pia kupambana na Vinega kipindi kile cha nyuma, tar 26/11/2012 Vinega waliplan show na Clouds wakapanga show yao pia tena kwa kuahidi kuwaleta wasanii wa nje DMX na Fabulous, ilikuwa vita hevi sana ile na kina MwanaFA walitumika pia kwenye ile vita.

Conclusion: Transitively, MwanaFA ana bifu na Jide, ie Kama Jide ana bifu na Clouds FM wakati Clouds FM na MwanaFA ni wamoja, then MwanaFA ana bifu na Jide.
 
clouds ni kama hitler,walijikusanyia nguvu mbele ya macho ya watu huku wakipigiwa makofi na hata waliokuja kuwapinga badae..tulikuwa wapi hadi wanajenga hiyo evil empire?
 
Sikoseli na ni njiti pia, labda nyinyi ndio mnamshangaa, mimi namuelewa bado nisikie tu analiwa kama mboga.
 
Tusimlaumu FA, kwan ye ni mwanamzik na anatafuta pesa
So hapo wa kumlaumu ni aliyempa mkataba
 
Not necessarily. Kwa nini JD asingesogeza wiki moja mbele ya show yake?

JD ndiye alieanza kutangaza show, then hao wengine wakatangaza later. At least they have shown themselves who they are
 
Ni zamu kwa zamu, JD alinjoy coverage ya Clouds FM, na sasa ni wenzake kama Ruge alivyosema. Siku MwanaFA naye atakuja kuwa replaced tutamsikia.

Nimepapenda hapo. Jd sasa apunguze kulalamika. Jd kama promo kapewa sana na Clouds akatae akubali, kama ilifikia kipindi wakam favor kila tangazo analolipia Clouds fm, wanali double. Kama tangazo lilikuwa la tsh 100 wanamuongezea linakuwa la tsh 200, lakini hili hata siku moja hajawahi kulikanusha wala kulizungumzia.
 
JD ndiye alieanza kutangaza show, then hao wengine wakatangaza later. At least they have shown themselves who they are

Mkuu unadhani kibiashara kuna tatizo, kama unaona utaweza kutengeneza pesa nzuri kupitia kwa kutengeneza beef na mwenzako?
Ile show ni ya Clouds Mwana FA amelipwa kwa ajili ya ku perform, yeye kosa lake lipo wapi kama waajiri wake ndio wanaopanga hizo tarehe za show?!
 
kwani unafikiria huyo jamaa ni mzima,hizi ni tabia za watoto wakiume wasio ridhiki,hebu kumbuka walivyojitoa ECT alivyoanza majungu na vijembe.AY naona kamkacha kiana sababu ya hiz tabia zakutumika na kutumiwa kama kopo la msalani,huyu jamaa kama sio msomi sijui wengine mnaenda darasani kuongeza vyeti ila busara na hekima hakuna kitu ,mmnazidiwa mpaka na sisi form four division IV... ass hoe
 
Hapo mbona mm naona yapo sawa maana huyu ana mashabiki wake na Jide ana mashabiki wake

Suala si hilo Lubengo. Kinachowashangaza wengi nikiwamo mimi nikwamba Mara ya kwanza Jide ndiye alianza kutangaza kwamba show yake itakuwa tar 31,Mwana Fa nae akatangaza tarehe hiyohiyo! Alipoulizwa na baadhi ya wanahabari mbona show yake ipo siku ambayo jide ana show akasema amepanga tar hiyo sababu itakuwa ni mwisho wa mwezi hivyo watu wengi watakuwa na pesa. Mimi nilikubaliana wakati ule na idea ya Mwana FA nikijua kijana ana nia ya kutafuta PESA. Baada ya kifo cha Ngwea Jide alisema atatangaza tar mpya ya show yake. Mwana FA nae alisema atatangaza tar mpya. Watu wengi walisubiri waone Jide atasema tar gani na FA atasema tar gani. Cha ajabu FA hakutangaza tar yake mapema mpaka Jide alipo tangaza ndipo FA nae akatangaza tar ile ile aliyotangaza Jide!. Jide ameweka wazi sababu ya kuweka show yake tar hiyo kwamba ni siku ambayo ni birthday yake.FA angetuambia kachagua siku hiyo kwa sababu zipi wakati alishasema mwanzoni kwamba show yake alichagua iwe mwisho wa mwezi sababu watu watakuwa na pesa,si angeifanya tar 29June ambayo niJumamosi na mwisho wa mwezi!. Nachokiona ni kwamba FA anatumika. Na hii ni baada ya kuona anaishiwa kipaji hivyo anatafuta watu wa kumbeba. Ingawa ni marafiki AY ana busara na anaheshimika zaidi kuliko huyu kijana. Na ndio maana AY ana maendeleo zaidi kimaisha na katika medani ya muziki ndani na nje ya TZ kuliko huyu kijana!. Mi nilidhani kuwa show zingetofautiana tar,FA angeweza kwenda kwenye show ya Jide na kuimba nyimbo walizowahi imba pamoja ns the same could have been done by Jide!?. Wakati huu wasanii wote walitakiwa kuweka njaa pembeni na kupigania maslai yao zaidi. Bila hivyo ndio haya yanatokea msanii anakufa hata kibanda cha kuuza vocha tu hana. Sijui lini mtakuwa na akili nyie wasanii mnaotumiwa!
 
kwani unafikiria huyo jamaa ni mzima,hizi ni tabia za watoto wakiume wasio ridhiki,hebu kumbuka walivyojitoa ECT alivyoanza majungu na vijembe.AY naona kamkacha kiana sababu ya hiz tabia zakutumika na kutumiwa kama kopo la msalani,huyu jamaa kama sio msomi sijui wengine mnaenda darasani kuongeza vyeti ila busara na hekima hakuna kitu ,mmnazidiwa mpaka na sisi form four division IV... ass hoe

mkuu, siku hizi MwanaFA na AY hawako karibu tena?
 
Mkuu unadhani kibiashara kuna tatizo, kama unaona utaweza kutengeneza pesa nzuri kupitia kwa kutengeneza beef na mwenzako?
Ile show ni ya Clouds Mwana FA amelipwa kwa ajili ya ku perform, yeye kosa lake lipo wapi kama waajiri wake ndio wanaopanga hizo tarehe za show?!

There is a point in that bold
 
Back
Top Bottom