MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

please naomba direction na mazingira ya Simanjiro nipo DODOMA

Simanjiro ni wilaya inayopatikana Mkoa wa Manyara imepakana na wilaya ya Meru kaskazini.na mashariki inapakana na wilaya ya kiteto,,kusini mwa simanjiro imepakana na wilaya ya Kondoa inafikika ila ni barabara ya Vumbi kama upo dodoma unaweza kuja Arusha mjini alafu ukapanda gari za moja kwamoja kutoka Arusha hadi Kiteto zinapita hapo simanjiro mda wa masaa ma4_5 Nauli ya Arusha to Kiteto ni elfu 14 hivyo ya kufika simanjiro huenda ikawa hata elfu 12 au 13 ukitokea arusha...au kama upo dodoma pia waweza panda gari zinazoenda Kondoa pale stendi unaweza kupata gari pia za simanjiro ambazo huenda hadi Kiteto.mjini (kibaya) alafu zinaunga hadi simanjiro
Gari za kule nazofahamu ni

Kimotco
Machame
Coastline
(imara zaidi)

Mazingira ya kule bhana ni barid baridi na jamiii ya kule wengi ni WAMASAI hujishughulisha na ufugaji kwa wingi,,ulinaji wa asali,,uchomaji mikaa,,na kilimo pia.

Ndio hukohuko ni karibu na mererani wanapochimba madini ya Tanzanite

Kiufupi jiandae kuishi na Maasai people wako peace sana ukijua kuishi nao....ila ni chaka kimtindo kaka....
 
Mi wilaya ya meru pia hata sijui pakojee

Meru ni wilaya inayipatikana.mashariki mwa jiji letu la Arusha barabara ya kwenda Moshi kilimanjaro wakazi wa meru hujishughulisha zaidi na.kilimo cha ndizi na mbogamboga kiufupi mboga za majani hutokea kule...
Kuna meru kaskazini ambapo ndo kuna vijiji around Mlima Meru na pia meru kusini ambapo hakuna miinuko kivile ambapo pia uwanja wa kimataifa wa ndege wa Kilimanjaro unapatikana

Mazingira ya huku ni baridi baridi andaa masweta....na blanket....

Kuna maeneo yanaitwa

Maji ya chai
Usariva
Ngarenanyuki
Kikatiti
King'ori
mbuguni (chaka)

Yanapatikana huko....

Kifupi hio ndio Meru jamii yakule kuna wamasai na wameru wenyewe korofi sana hawa watu..ukiwavuruga....
Kuna vivtutio kma

Arusha national park
Mount meru yenyewe
Ngurdoto crater
Momella lake

Karibu saana Arusha....

Kama huapataki na.unataka singida nijulishe tubadilshane....mana Arusha ndio nyumbani mimi....
 
WALIOPANGIWA MKURANGA WANIPM namba zao niwaunge group la walimu Mkuranga..watapata taarifa za kutosha.
 
Habari walimu, poleni kwa msoto wa kusubiri ajira kwa muda mrefu sana, lakini kwa nguvu za mwenyezi tamisemi wametupatia ajira japo kuna merekebisho kidogo kwa walimu wenzetu ambayo hawakupata ajira kabisa. Karibu wilaya ya ulanga mkoa wa morogoro mimi pia mwalimu mpya mwenzenu nimechaguliwa wilaya hiyo ya wilaya ambayo naifahamu kwa kina sana kozi mimesoma wilaya hiyo kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba karibuni walaya ya ulanga for more information waweza kunitafuta kwa namba 0753198577, 0789650392 na 0655669079.
 
Selina Kombani sec ndio nimepangwa hapo cjui hio shule ipo karibu na wilayani Ulanga?

Celina Kombani hiyo shule ipo tarafa ya Mwaya yani ukifika Ulanga disrtict council ambapo ni makao makuu ya wilaya ya Ulanga unapanda gari kuelekea mwaya mdau shule ipo sehemu nzuri na umeme upo na network ipo mdau ni eneo ambalo .Tarafa ya mwaya ni eneo ambalo limezungukwa na hifadhi ya mbuga ya selous mdau
 
kuna majambazi?mbona unatuogopesha jamani, Mimi huko huko naenda tena sikufahamu,

Usiogopee vitisho ..pori lipo kweli tena.kubwa tu lakini...hua kuna.escort ya askari..pia hawaruhusu kusafiri usiku sikuhizi ni mchana tu!!so.usitishikee.....
 
Wakuu...
Kwa anayeifahamu wilaya ya Rorya Mara anijuze...nimepangwa huko lakin sina ufahamu hata kidogo juu ya wilaya hiyo.

Wilaya ya Rorya iko mkoa wa Mara, nenda mpaka Mwanza. Sasa inategemea na shule uliyopangiwa lakini kama ni lazima uende wilayani nakushauri uende Tarime ulale asubuhi sana upande magari ya Utegi au Shirati uwaulize kama wanapita Wilayani uende asubuhi urudi Tarime jioni. Huko hakuna guest kwahiyo usiende jioni. Ni wilaya mpya, ukisharipoti wao watakupa direction ya shule uliyopangiwa.
 
Asanten kwa taarifa wakuu....na vipi kuhusu huduma za kijamii za kule mfano umeme na maji

Umeme ndo kwanza wanasambaza wilayani, sehemu nyingi muhimu kuna umeme, Rorya pazuri nilikuwa Mkurugenzi wa Wilaya hapo kwa siku tatu kwahiyo ninapajua vizuri kabla sijahama. Shirati ndo mji mkuu wa Rorya, makao makuu ya Wilaya yako Ingri, kuna hosiptali nyingi nzuri Kuna Shirati, Burere, Kowak, ambazo zote zinahuduma nzuri at least. Hizo sehemu zote zina umeme.
 
Heshima mbele wakuu. Kuna mtu ana taariifa kuhusu chuo cha UFUNDI PERAMIHO?. Nimejaribu kutafuta details zao mtandaoni sijazipata. NATANGULIZA SHUKURANI ZANGU ZA DHATI .
 
Niko geita ila Sio bukombe mkuu sema tutakuwa njia moja vipi safari ipo lini!!?
 
Back
Top Bottom