MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

please naomba direction na mazingira ya Simanjiro nipo DODOMA
 
mnataka sababu tu na kupata kusema wakati unajua kua typing error kwa bahati mbaya. kama wewe hujawahi kukosea
 
Duh MURANGI nia sehemu za majita huko, kiukweli ni mbali sana kutoka mjini, mara ya mwisho nimepita huko mwaka 2011 nakumbuka hapakua na umeme sijui kwa sasa.

Wakazi wa kule wengi ni wavuvi, wengine ni wakulima.
Kiukweli watoto hawana muamko na shule zaidi ya kutafuta pesa kupitia shughuli za uvuvi.

Infact hupaswi kuogopa wala kukata tamaa, we kafanye kazi maana tangu 2011 patakua pamebadilika mkuu.
 
kwa walimu mlopangwa mkoa wa kagera wilaya ya biharamulo tukutane apa tupeane mawili matatu.
 
Tandahimba ni wilaya inayopatikana Mkoa wa Mtwara, unapotaka kwenda waweza panda mabasi ya Dar-Tandahimba mfano wa basi ni TANDAHIMBA XPRESS (Bovubovu hivi) au upande basi linaloenda Masasi kutokea Dar then shuka Mtama (Kwa Bwana Mkubwa) hapo utapata mabasi ya huko, changamoto ya huko ni barabara mbovu tu ndo maana hata mabasi yanayokwenda huko ni yale ya tripu moja Dar Tripu gereji.

Asante sanaa Mkuu
 
kwa anaefahamu wilaya ya Musoma tafadhali naomba dondoo. Musoma DC ni ile ya mini au vijijini? Mdogo wangu kapangwa Musoma DC.
 
Musoma DC ni Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (hii ni Musoma Vijijini) yenye Tarafa za Nyanja (Majita) na Kiagata. Zamani ilikuwa kubwa lakini mwaka juzi imemegwa na kuzaa Butiama DC. Hata hibyo, ofisi za Musoma DC bado ziko Musoma Mjini.
 
Duu!! Vp kuhusu hyo shule na nyumba za kupanga unaweza kupata around??
 
Asante sanaa Mkuu

Asee kuna classmate zangu ndugu wawili hapo Tandahimba na mzee wao ni diwani na mfanyabiashara maarufu sana tu. Kama utapenda wakupe sapoti contact ni PM, mmoja ni ustaz sana ila ni mkarimu sana. Mwingine msela sana na mkarimu pia (au tunaita mwana)
 
Tandahimba sio wilaya kongwe, haina hata miaka mingi iliundwa 1995 kama sikosei

Upo sahihi Mkuu. Tandahimba ni kati ya wilaya zinazokua kwa kasi na kuna biashara sana. Ni moja kati ya wilaya ambayo utaikuta bank ya CRDB kutokana mazingira ya kibiashara. Ni wilaya iliyojengwa kwa mipango mji wa hali ya juu. Nenda utapafurahia sana, ni pazuri. Ukifika tupe mrejesho Mkuu
 
Wakuu...
Kwa anayeifahamu wilaya ya Rorya Mara anijuze...nimepangwa huko lakin sina ufahamu hata kidogo juu ya wilaya hiyo.
 
panda gari mpaka arusha mjini then pale arusha stendi chukua bodaboda mpaka makao mapya ndio magari ya kwenda simanjiro waambie unashukia orkesumet hapo ndipo makao makuu ya wilaya yalipo, nauli tokea arusha ni 10000. mabasi yanaondoka SAA 5 asubuh
 
Wapendwa,,kwa neema ya Mungu ajira amazo wengi wetu tumekuwa tukizisubiri zimetoka sasa..Mimi ni mmoja wao waliopangwa kwenye wilaya hiyo inayoitwa Moshi Dc mahali ambapo sikuwaza kuwa nitaenda katika uhai wangu hata siku moja ila ndo hivyo sina jinsi..Ukiondoa taarifa ya kuwa Kilimanjaro ni mkoa wenye baridi sina taarifa yoyote ile ambayo inaweza kuwa msaada kwangu mimi..Tafadhali,mwenye kuijua vizuri hiyo sehemu anielekeze vizuri..Pamoja na hayo,wale waliopangwa Lindi Mjini au Mtwara Mjini na ungependa urudi kwenu Moshi,waweza wasiliana nami maan kwa kweli afya yangu hairuhusu kuishi sehemu yenye baridi..Niwatakie wakati mwema..
 
kama upo Dom Fanya uje hadi hapo Ranch ya kongwa ( morogoro road) then pata gari za kuja kite to ( masaa 2tu), utall kiteto na asbh utapanda gr za kuja orkersumet( lipo moja) saa tatu ushafika wilayan
 
Mdogo wangu amepangwa huko ualimu sekondari, je mazingira kwa ujumla yapoje?umbali upoje kutoka Arusha mjini? hali ya hewa pamoja na shule za karibu ni zipi?

karibuni wadau...
 
acha nyoya dogo.... .I mean kimbia tafuta shule nyingine ya kuhamia
 
Back
Top Bottom