MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

MWALIMU: Uliza kuhusu kituo ulichopangiwa

Ni chuo kizuri cha Mission kipo Songea Jimbo la Peramiho.
 
Napajua sana Bukombe, Maporini kiasi hamna umeme sehemu kubwa Ila maji siyo shida saana. Visima vipo
 
ofisi za halmashaur zpo maeneo gani mkuu. zipo mbali na barabara ya nyakanaz kahama.
 
Aliyepangwa uyui mm MKUU hapa Kata ya wilayani Nina hitaj walim 4 ke2 me 2 jama nitafuten mbaki mjini 0762080829
 
Uyui-Tabora pakoje wadau? Nitajieni shule zilizo chaka na zilizo wilayani.
 
Ungepita tabora ndo karibu..maana tabora to mpanda ni 7 hours.shemeji ako ndo anakofanyia kazi huko.ila network inayoshika huko ni airtel tu mkuu.

hii wiki yote niko mpanda, simu mitandao yote iko vizuri. Njia ya Tabora tatizo ni mbaya sana yani tope tu.
 
jamani naombeni ushauri nimepangiwa ruvuma mbinga shule inaitwa nanswea now nipo feza boys naombeni mnisaidie mazingra kwa aneye fahamu
 
wakuu naomba kujuzwa kuhusiana wilaya ya babati hususa ni shule ya gidasi kuhusu huduma za kijamii mfano maji,umeme na kama kuna nyumba za walimu n.k
 
Wameru ni wajuaji na watata! Kukupasua ni dakika sifuri sehemu almost ni nzuri na uwezo wa kufika mainroad ni mkubwa na si mbali. Maji sehemu nyingi wamechimba visima. Na umeme si vijiji vyote na shule nyingi ziko kwenye vicentre


asante kwa taarifa mkuu
 
nauliza wakuu h/w bukombe zipo maeneo gani au umbali gani kutoka kahama? nauli bei gani kutoka kahama?
 
kama kichwa kinavyojieleza, naomba kwa yule anaye ifahamu wilaya ya Nachingwea mkoa wa Lindi anijuze kwani nimepata kazi ya kufundisha huko.
 
Meru ni wilaya inayipatikana.mashariki mwa jiji letu la Arusha barabara ya kwenda Moshi kilimanjaro wakazi wa meru hujishughulisha zaidi na.kilimo cha ndizi na mbogamboga kiufupi mboga za majani hutokea kule...
Kuna meru kaskazini ambapo ndo kuna vijiji around Mlima Meru na pia meru kusini ambapo hakuna miinuko kivile ambapo pia uwanja wa kimataifa wa ndege wa Kilimanjaro unapatikana

Mazingira ya huku ni baridi baridi andaa masweta....na blanket....

Kuna maeneo yanaitwa

Maji ya chai
Usariva
Ngarenanyuki
Kikatiti
King'ori
mbuguni (chaka)

Yanapatikana huko....

Kifupi hio ndio Meru jamii yakule kuna wamasai na wameru wenyewe korofi sana hawa watu..ukiwavuruga....
Kuna vivtutio kma

Arusha national park
Mount meru yenyewe
Ngurdoto crater
Momella lake

Karibu saana Arusha....

Kama huapataki na.unataka singida nijulishe tubadilshane....mana Arusha ndio nyumbani mimi....


asante kwa taarifa vp vijiji vya meru huduma za umene na maji zipo?
 
nauliza wakuu h/w bukombe zipo maeneo gani au umbali gani kutoka kahama? nauli bei gani kutoka kahama?

Kutokea kahama nauli haijazidi 5 elfu, sina hakika kuhusu umbali ingawa haijazidi kilometers 90.
Wilaya inatwa Bukombe, lakini kabla ya ufika wilayani kunasehem panaitwa kijiji kinaitwa Bukombe.
Kua na tahadhari usije shukia kijijini kabala ya kufika wilayani.
Au itakua rahisi ukesema unakwenda Ushirombo.
Ukishuka Pale Bukombe ( ushirombo) wilayani nivema ukachukua usafiri wa bodaboda na watakupeleka Halmashauri kwa 1000
 
Back
Top Bottom