Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,348
- 23,757
Ndugu zangu Watanzania,
Kama leo hii Kungetokea muujiza Wa Hayati Baba Wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kufufuka kutoka Kaburini Butiama alikofumba macho na alikolala Usingizi wa Milele na kurejea hapa Nchini na kutazama yale yanayofanywa Na Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Kwa Hakika Baba wa Taifa angekaa chini na kububujikwa na machozi ya Furaha kubwa sana na kumshukuru sana Rais Samia kwa kazi kubwa aliyoifanya na anayoendelea kuifanya kutimiza ndoto alizokuwa nazo pale Taifa letu lilipokuwa linajipatia uhuru wake. Ambapo yeye mpaka anaaachia uongozi na kufariki Dunia alikuwa bado kutimiza Ndoto hizo ambazo kwa sasa Rais Samia amezitimiza.
Ikumbukwe ya kuwa kiu kubwa na ndoto ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ilikuwa ni kupigana vita kali sana na maadui watatu ambao ni Umaskini ,Ujinga pamoja na Maradhi. Ambapo Mama yetu Mpendwa kwa Sasa amepigana kikomandoo na kihodari saba kutokomeza maadui hao. Ambapo ameweza kuwekeza vya kutosha katika secta ya kilimo inayogusa Maisha ya watanzania wengi. Ambapo mpaka sasa Bajeti ya kilimo ni Trilioni moja point tisa. Anatoa mabilioni ya ruzuku katika pembejeo za kilimo, amevutia wawekezaji katika secta ya kilimo, ameongeza pesa za utafiti wa mbegu bora ,afya ya udongo,mafisa kilimo kwa ajili ya kutoa Elimu kwa wakulima na kuongeza tija na kipato kwa mkulima mmoja mmoja.
Rais Samia ameimarisha masoko kwa mazao ya wakulima kwa kauli mbiu yake ya kilimo ni Biashara. Jambo lililowatoa mamilioni kwa mamilioni ya watanzania katika dimbwi la umaskini na njaa hapa nchini na kuwainua kiuchumi. Ndio maana kwa sasa ukienda vijijini unaona watu wamepiga bati za msauzi,wamesakafia vizuri na kupaka rangi nyumba zao. Utaona Wananchi wakiwa na usafiri wa pikipiki wamepaki majumbani mwao na wengine wakiwa na magari mazuri kabisa ya kutembelea na kubebea mizigo yao kutoka waliko kwenda sokoni.
Leo ni kawaida kuona wakulima wakisomesha watoto wao katika shule nzuri na kula milo mitatu mizuri na yenye virutubisho . Rais Samia pia amepeleka umeme hadi vitongoji na kuweka mwanga muda wote . Jambo lililopelekea kuchochea shughuli za kijasirimali na kiuchumi. Ndio maana ukienda vijijini utakuta shughuli za uchomeleaji,saluni za kike kwa kiume ,mashine za kukamua mafuta ,kusaga na kukoboa sembe ,friji kwa ajili ya vinywaji,samaki ,nyama ,matunda n.k.
Lakini pia Rais Samia amewekeza katika Elimu katika juhudi za kutokomeza adui ujinga hapa Nchini. Amejenga shule kila kona ya Nchi,amejenga na kuongeza vyumba vya madarasa zaidi ya elfu 20 na kufanya sasa habari za wanafunzi kwenda awamu ya pili kubakia historia. Kwa kuwa wanafunzi wote wanaofaulu wanapata nafasi ya kuripoti kwa pamoja na kusoma katika mazingira rafiki kabisa. Anatoa Elimu bure ambapo zaidi ya Billion 33 zinatolewa kila mwezi. Ameongeza bajeti ya Elimu ya juu kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi kufikia Bilioni mia saba 80 .
Ukija katika adui maradhi unaona namna Rais Samia alivyo wekeza katika secta ya afya. Ambapo katika Makka mitatu ya uongozi wake alikuwa amewekeza zaidi ya Trilioni sita ambapo kufika sasa mabilioni ya pesa yameongezeka katika secta ya Afya. Ambapo vituo vya afya zaidi ya mia tatu vimejengwa nchini kwote , hospitali za wilaya,mkoa ,rufaa mpaka kanda zimejengwa na kuboreshwa sana. Vifaa tiba bora na vya kisasa vimenunuliwa na kuwekwa Mahospitalini. Ndio maana vifo vya mama na mtoto vimepungua kabisa hapa Nchini. Hata wagonjwa waliokuwa wanapelekwa nje ya Nchi wamepungua sana badala yake wagonjwa wanaotoka nje ya nchi kuja kutibiwa hapa Nchini wameongezeka kufikia karibu Elfu kumi na mbili.
Ikumbukwe ya kuwa afya ndio mtaji na moja wa mwanadamu. Hivyo uwekezaji huu wa Rais Samia unamaanisha katoa mtaji wa bure kabisa kwa watanzania wote. Haitoshi ilifikia wakati Rais Samia akaanza kuwafuata wagonjwa majumbani na mahali popote walipo. Hii ni katika kampeni yake ya kusambaza madaktari bingwa na bobezi katika magonjwa mbalimbali ambao walikuwa wakiweka kambi maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwatibu wagonjwa bure kabisa na kuokoa maisha ya watu.hii yote ikiwa ni dhamira njema ya Mama yetu kipenzi ya kuona watanzania wakiwa na afya njema na kupata hudumu za kimatibabu kwa urahisi na kufikiwa mahali walipo. Jambo ambalo ni nadra sana kufanywa na viongozi wa kiafrika.
Yamewezekana haya yote kwa sababu ya ujasiri alionao Rais Samia katika kufanya maamuzi na kuchukua hatua za kijasiri na yenye kuleta matokeo chanya kwa watu. Nimeandika kwa ufupi tu kati ya mengi sana ambayo ningeweza kuwaeleza juu ya kazi tukuka iliyofanywa na Rais wetu Mpendwa. Itoshe kusema Rais Samia ni Zawadi kwa Taifa letu tunayopaswa kuitunza na kuilinda kwa wivu mkubwa sana. Watu na viongozi aina yake huwa hawazaliwi kila siku na hawapatikani kila sehemu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa zawadi hii adimu ya kuwa na Mama Nchini.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kama leo hii Kungetokea muujiza Wa Hayati Baba Wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kufufuka kutoka Kaburini Butiama alikofumba macho na alikolala Usingizi wa Milele na kurejea hapa Nchini na kutazama yale yanayofanywa Na Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Kwa Hakika Baba wa Taifa angekaa chini na kububujikwa na machozi ya Furaha kubwa sana na kumshukuru sana Rais Samia kwa kazi kubwa aliyoifanya na anayoendelea kuifanya kutimiza ndoto alizokuwa nazo pale Taifa letu lilipokuwa linajipatia uhuru wake. Ambapo yeye mpaka anaaachia uongozi na kufariki Dunia alikuwa bado kutimiza Ndoto hizo ambazo kwa sasa Rais Samia amezitimiza.
Ikumbukwe ya kuwa kiu kubwa na ndoto ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ilikuwa ni kupigana vita kali sana na maadui watatu ambao ni Umaskini ,Ujinga pamoja na Maradhi. Ambapo Mama yetu Mpendwa kwa Sasa amepigana kikomandoo na kihodari saba kutokomeza maadui hao. Ambapo ameweza kuwekeza vya kutosha katika secta ya kilimo inayogusa Maisha ya watanzania wengi. Ambapo mpaka sasa Bajeti ya kilimo ni Trilioni moja point tisa. Anatoa mabilioni ya ruzuku katika pembejeo za kilimo, amevutia wawekezaji katika secta ya kilimo, ameongeza pesa za utafiti wa mbegu bora ,afya ya udongo,mafisa kilimo kwa ajili ya kutoa Elimu kwa wakulima na kuongeza tija na kipato kwa mkulima mmoja mmoja.
Rais Samia ameimarisha masoko kwa mazao ya wakulima kwa kauli mbiu yake ya kilimo ni Biashara. Jambo lililowatoa mamilioni kwa mamilioni ya watanzania katika dimbwi la umaskini na njaa hapa nchini na kuwainua kiuchumi. Ndio maana kwa sasa ukienda vijijini unaona watu wamepiga bati za msauzi,wamesakafia vizuri na kupaka rangi nyumba zao. Utaona Wananchi wakiwa na usafiri wa pikipiki wamepaki majumbani mwao na wengine wakiwa na magari mazuri kabisa ya kutembelea na kubebea mizigo yao kutoka waliko kwenda sokoni.
Leo ni kawaida kuona wakulima wakisomesha watoto wao katika shule nzuri na kula milo mitatu mizuri na yenye virutubisho . Rais Samia pia amepeleka umeme hadi vitongoji na kuweka mwanga muda wote . Jambo lililopelekea kuchochea shughuli za kijasirimali na kiuchumi. Ndio maana ukienda vijijini utakuta shughuli za uchomeleaji,saluni za kike kwa kiume ,mashine za kukamua mafuta ,kusaga na kukoboa sembe ,friji kwa ajili ya vinywaji,samaki ,nyama ,matunda n.k.
Lakini pia Rais Samia amewekeza katika Elimu katika juhudi za kutokomeza adui ujinga hapa Nchini. Amejenga shule kila kona ya Nchi,amejenga na kuongeza vyumba vya madarasa zaidi ya elfu 20 na kufanya sasa habari za wanafunzi kwenda awamu ya pili kubakia historia. Kwa kuwa wanafunzi wote wanaofaulu wanapata nafasi ya kuripoti kwa pamoja na kusoma katika mazingira rafiki kabisa. Anatoa Elimu bure ambapo zaidi ya Billion 33 zinatolewa kila mwezi. Ameongeza bajeti ya Elimu ya juu kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi kufikia Bilioni mia saba 80 .
Ukija katika adui maradhi unaona namna Rais Samia alivyo wekeza katika secta ya afya. Ambapo katika Makka mitatu ya uongozi wake alikuwa amewekeza zaidi ya Trilioni sita ambapo kufika sasa mabilioni ya pesa yameongezeka katika secta ya Afya. Ambapo vituo vya afya zaidi ya mia tatu vimejengwa nchini kwote , hospitali za wilaya,mkoa ,rufaa mpaka kanda zimejengwa na kuboreshwa sana. Vifaa tiba bora na vya kisasa vimenunuliwa na kuwekwa Mahospitalini. Ndio maana vifo vya mama na mtoto vimepungua kabisa hapa Nchini. Hata wagonjwa waliokuwa wanapelekwa nje ya Nchi wamepungua sana badala yake wagonjwa wanaotoka nje ya nchi kuja kutibiwa hapa Nchini wameongezeka kufikia karibu Elfu kumi na mbili.
Ikumbukwe ya kuwa afya ndio mtaji na moja wa mwanadamu. Hivyo uwekezaji huu wa Rais Samia unamaanisha katoa mtaji wa bure kabisa kwa watanzania wote. Haitoshi ilifikia wakati Rais Samia akaanza kuwafuata wagonjwa majumbani na mahali popote walipo. Hii ni katika kampeni yake ya kusambaza madaktari bingwa na bobezi katika magonjwa mbalimbali ambao walikuwa wakiweka kambi maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuwatibu wagonjwa bure kabisa na kuokoa maisha ya watu.hii yote ikiwa ni dhamira njema ya Mama yetu kipenzi ya kuona watanzania wakiwa na afya njema na kupata hudumu za kimatibabu kwa urahisi na kufikiwa mahali walipo. Jambo ambalo ni nadra sana kufanywa na viongozi wa kiafrika.
Yamewezekana haya yote kwa sababu ya ujasiri alionao Rais Samia katika kufanya maamuzi na kuchukua hatua za kijasiri na yenye kuleta matokeo chanya kwa watu. Nimeandika kwa ufupi tu kati ya mengi sana ambayo ningeweza kuwaeleza juu ya kazi tukuka iliyofanywa na Rais wetu Mpendwa. Itoshe kusema Rais Samia ni Zawadi kwa Taifa letu tunayopaswa kuitunza na kuilinda kwa wivu mkubwa sana. Watu na viongozi aina yake huwa hawazaliwi kila siku na hawapatikani kila sehemu. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa zawadi hii adimu ya kuwa na Mama Nchini.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.