Mwali: Mmiliki wa DOWANS ni huyu!

Mwali: Mmiliki wa DOWANS ni huyu!

Status
Not open for further replies.
Wakati tukijadili Dowans inabidi pia tuitupie macho AGGREKO kampuni ya Kiingereza (Scotland) inayotengeneza mitambo ya kufulia umeme. Ni kitu gani kilituzuia tusiwasiliane moja kwa moja nao - instead tukawapa tenda wakala wao UAE. Kuna nini Dubai ?


Dar - Dubai connection is getting thicker and thicker !! Kwa nini option ya kununua huwa haipo kwenye hizi tenda instead tunakodisha na baadaye kulazimika kununua ?

Hayawi, hayawi, soon yatakuwa. Kwa kweli, hii nchi inatia kichefu chefu..... sijui kama tutafika kweli
 
BY the way, hawa Richmond TZ wamerudisha zile pesa za LC? Ninavyoelewa ni kwamba ili benki itoe L/C kwa jina lako, ni lazima utoe cash cover equivalent na US$ au forex unayotaka. Sasa kama LC ilitolewa kwa guarantee ya CRDB, ina maana ya kwamba hawakuwa na TShs hivyo eventually lazima Richmond warudishe hizo pesa kwa Tshs.
 
Wale nasikia wanaitwa Law Associates - kuna kaka wawili: Ringo na Cuthbert.

Hawa ni mawakili wawili tofauti na wote wanaitwa Ringo na wote (sijui ni coincidence au) wamehusika kwa namna moja au nyingine na makampuni ya kitapeli ya Rostam Aziz

Ringo & Associates waliohusika na Dowans ambao wako pale Peugeot House managing partner ni Dr. Freddy Ringo na wale waliohusika na Kagoda/Richmond na madudu mengine ya Rostam wako pale CRDB Azikiwe wanaitwa Law Associates na managing partner ni Dr. Ringo W. Tenga. Wote hawa wamewahi kfundisha UDSM kitivo cha sheria.
Though the confusion might be natural to some of you here ila ni watu wawili na kampuni mbili tofauti za kisheria but coindidentally and within a span of related periods of time under dubious circumstances they served the one and only mafia godfather in our beloved Tanzania
 
Hivi mali hizi zote Rostam kazitoa wapi kwa kipindi kifupi?
Babake Rostam alikuwa mfanya biashara ya ngozi kwa kampuni iitwayo Africa Trade Development ikiwa na makao yake Pugu Road! Leo ana Caspian, na Share Vodacom just to mention a few! Anachorigia ni ufadhiliwake kwa CCM tangu kwenye mchakato wa kupata mgombea urais hadi uchaguzi wenyewe! Huo ufadhili wa miradi jimboni kwake ni kuwafumba wananchi juu ya wizi anowabia kwenye raslimali zao! Hivi mtu akiubia Ng"ombe wako, kesho akakulaghai kwa kukupa kikombe cha maziwa utamwita MFADHILI?
 
Mimi nasubiri mwali kwa hamu kubwa maana cha kusema sina watu wanakula nchi kama wanavyotaka bila kushughulikiwa na yeyote.

Tunabaki kuwabembeleza wajiuzuru maana hawatawajibishwa hata iweje
 
Hivi mali hizi zote Rostam kazitoa wapi kwa kipindi kifupi?
Babake Rostam alikuwa mfanya biashara ya ngozi kwa kampuni iitwayo Africa Trade Development ikiwa na makao yake Pugu Road! Leo ana Caspian, na Share Vodacom just to mention a few! Anachorigia ni ufadhiliwake kwa CCM tangu kwenye mchakato wa kupata mgombea urais hadi uchaguzi wenyewe! Huo ufadhili wa miradi jimboni kwake ni kuwafumba wananchi juu ya wizi anowabia kwenye raslimali zao! Hivi mtu akiubia Ng"ombe wako, kesho akakulaghai kwa kukupa kikombe cha maziwa utamwita MFADHILI?
 
Hivi mali hizi zote Rostam kazitoa wapi kwa kipindi kifupi?
Babake Rostam alikuwa mfanya biashara ya ngozi kwa kampuni iitwayo Africa Trade Development ikiwa na makao yake Pugu Road! Leo ana Caspian, na Share Vodacom just to mention a few! Anachorigia ni ufadhiliwake kwa CCM tangu kwenye mchakato wa kupata mgombea urais hadi uchaguzi wenyewe! Huo ufadhili wa miradi jimboni kwake ni kuwafumba wananchi juu ya wizi anowabia kwenye raslimali zao! Hivi mtu akiubia Ng"ombe wako, kesho akakulaghai kwa kukupa kikombe cha maziwa utamwita MFADHILI?

Dubai/Oman conection..... soon tutajua tu, tumewashika pabaya
 
Mag3
View Post

Wakati tukijadili Dowans inabidi pia tuitupie macho AGGREKO kampuni ya Kiingereza (Scotland) inayotengeneza mitambo ya kufulia umeme. Ni kitu gani kilituzuia tusiwasiliane moja kwa moja nao - instead tukawapa tenda wakala wao UAE. Kuna nini Dubai ?


Dar - Dubai connection is getting thicker and thicker !! Kwa nini option ya kununua huwa haipo kwenye hizi tenda instead tunakodisha na baadaye kulazimika kununua ?

Naona umenusa..... Hivi jiulize, kila kitu Dubai, kila kitu Dubai..... hata kampuni ya kutengeneza fedha G&D ni Dubai, G&D ya vitambulisho ni Dubai na hakuna anayekohoa kusema kitu, KULIKONI? Soon tutajua tu!!!!
 
Mwali... ataanza kutolewa; DPP, DCI, TISS don't worry we will do your work for you! Tutawapikia, kuwapakulia, na kuwawekea mezani.. mkipenda hata kuwawekea mdomoni... Tutakachowaomba mfanye ni vitu viwili tu...
 
Na Saed Kubenea, Mwana Halisi.

KELELE za sasa ndani ya serikali kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans ni jitihada zinazolenga "kukidhi maslahi binafsi," MwanaHALISI limegundua.

Vyanzo mbalimbali jijini Dar es Salaam na mikoani vimeonyesha kuwa hakuna tatizo la umeme hivi sasa nchini; wala hakuna upungufu wa maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme.

Uchunguzi wa gazeti hili sasa unathibitisha kuwa madai ya serikali, kwamba nchi karibu itaingia gizani kutokana na ukosefu wa umeme, hayana msingi wowote.

Kwa wiki nzima sasa serikali, ikishirikiana na Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) wamekuwa wakitoa tahadhari kuwa iwapo mitambo ya umeme ya kampuni ya Dowans haitanunuliwa mara moja, taifa litaingia gizani wakati wowote kuanzia sasa.

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja amesema serikali ina nia ya kununua mitambo ya Dowans ili kukabiliana na tishio la uhaba mkubwa wa umeme kutokana na mabwawa kukauka.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dk. Idris Rashid amesema kwamba mahitaji ya umeme yameongezeka nchini na kwamba kinachohitajika ni serikali kununua mitambo yote ya Dowans pamoja na vifaa vyote vya kuunganishia kwenye gridi ya taifa.

Hata hivyo, taarifa ndani ya TANESCO zinasema vyanzo muhimu vya nishati hiyo, ambavyo ni mabwawa ya maji, bado viko imara na maji yako kwenye viwango thabiti vya kuzalisha umeme.

Kwa mfano, hadi juzi Jumatatu, bwawa la Mtera mkoani Dodoma lilikuwa na maji ya kutosha ya kuzalishia umeme.

Kima cha juu cha ujazo katika bwawa la Mtera ni mita 698.50 na kina cha chini kwa ajili ya uzalishaji umeme ni mita 690.00. Lakini hivi sasa Mtera ina ujazo wa mita 695.91.

Hii ina maana kwamba kile kinachoitwa, "tishio la mabwawa kukauka," hakipo katika bwawa hilo. Kinachoonekana kuwa upungufu, wataalam wamesema, hakiwezi kuleta athari yoyote kubwa katika miezi ya karibuni.

Hali kama hiyo ipo katika bwawa la Kidatu mkoani Morogoro. Hadi juzi Jumatatu, maji katika bwawa hilo yalikuwa mita 449.37. Kima cha juu cha maji kwa Kidatu ni mita 451.00 huku kima cha chini ni mita 441.00.

"Kwa maana hiyo, mpaka sasa, na kutokana na takwimu hizi, hakuna ushahidi wa mabwawa hayo kukauka au kuwa hatarini kukauka," amefafanua injinia mmoja wa TANESCO makao makuu, Dar es Salaam.

Aidha, Mamlaka ya Hali ya Hewa imetangaza kuwa mvua kubwa zimeanza kunyesha katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga.

Wataalamu wa TANESCO wanasema ni mvua hizo ambazo zitajaza mabwawa ya Mtera, Kihansi, Nyumba ya Mungu, Kidatu na Hale kabla ya mwezi Machi na Aprili mwaka huu.

"Kwa mvua hizi zinazonyesha," kimeeleza chanzo chetu cha habari, "huenda zikalazimu TANESCO kuachia kingo za mabwawa na kuachia maji yatoke ili kuzuia yasibomoke."

Hadi Jumapili iliyopita, Waziri Ngeleja alikuwa ameanza kampeni kubwa akidai kuwa kununua mitambo ya kuzalisha umeme ya Dowans "siyo kufanya ufisadi" bali ni kuweka maslahi ya taifa kwanza.

Katika wimbo huo, Ngeleja aliungwa mkono na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe ambaye alisema anaweka mbele "maslahi ya taifa."

Lakini ni Ngeleja aliyeliambia bunge, zaidi ya miezi mitatu iliyopita, kuwa serikali haiwezi kununua mitambo hiyo kwa kuwa imetumika na kwamba kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Ununuzi wa Vifaa na Huduma serikalini ya mwaka 2004.

Katika haraka isiyo ya kawaida, serikali na TANESCO wametupilia mbali ushauri wa Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge na kudandia Kamati ya Zitto wakidai wanatafuta bunge liwaruhusu kununua mitambo ya Dowans.

Kamati ya Nishati na Madini ilishauri TANESCO kufanya kile ambacho wanaona kimo katika uwezo na uamuzi wao. Dowans ni sehemu ya sakata la Richmond ambalo maazimio ya Bunge juu yake hayajatekelezwa na serikali.

Hata hivyo, bado serikali inakabiliwa na mgogoro wa nani hasa wajadiliane naye katika kununua mitambo ya Dowans iliyoko Ubungo, Dar es Salaam.

MwanaHALISI imebaini kuwa wakati kampuni ya Dowans ilikuwa inaweka mitambo yake na baada ya kuanza uzalishaji, haikuwa na ofisi nchini na wala mmiliki wake halisi alikuwa hajulikani.

Hadi sasa, Bunge ambalo liliunda Kamati Teule kuchunguza mkataba wa kampuni ya Richmond iliyokabidhi shughuli zake kwa Dowans, halifahamu mmiliki wa Dowans.

MwanaHALISI imegundua kuwa kuna kampuni inayoitwa Dowans Holdings SA (DH-SA) iliyosajiliwa nchini Costa Rica, Amerika ya Kusini, tarehe 1 Julai 2005 na kwamba ndiyo yenye uhusiano na Dowans iliyoko Ubungo.

Kampuni ya DH-SA ilianzishwa na mtu mmoja aitwaye Bernal Zamora Alce. Taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ambazo gazeti hili limeona, zinaonyesha Zamora alisajili Dowans na makampuni mengine 99 yanayoishia na herufi "SA," kwa siku moja.

Taarifa zinasema kati ya makampuni hayo 100, Zamora alijitangaza kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi katika makampuni 52.

Hata hivyo, pamoja na utitili huo wa makampuni, imefahamika kuwa Zamora hana simu ya mkononi, hana sanduku la barua wala hajulikani mtaa anakoishi.

Uchunguzi uliofanywa na waandishi wa habari wa kimataifa na wanasheria mashuhuri nchini Costa Rica umegundua kwamba kampuni ya Dowans haikuwa na ofisi nchini humo haikuwa na simu wala gari.

Si nchini Costa Rica tu, bali kampuni ya Dowans yenye mitambo Ubungo, kwa mujibu wa taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza Richmond, haikuwa na namba za simu wala ofisi; wafanyakazi wake walikuwa wanatumia ofisi za kampuni ya Caspian Limited hapa nchini.

Kampuni ya Caspian inamilikiwa na mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz. Ni Rostam aliyethibitishia Bunge kuwa Dowans ilikuwa inatumia anuani zake.

Katika andishi lililotumwa serikalini na Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Costa Rica, kuitahadharisha serikali ya Tanzania kuhusu Dowans anasema, "Dowans ni kampuni ya mfukoni iliyoanzishwa mahususi kwa ajili ya kufanya kazi maalum."

Katika mazingira haya, Dk. Rashid alipoulizwa TANESCO inajadili na nani kuhusu ununuzi wa mitambo, alijibu haraka kuwa wao hawafanyi majadiliano bali wamepeleka mapendekezo serikalini. Alisema ni serikali yenye jukumu la kununua au kutonunua mitambo hiyo.

Alipoulizwa sasa serikali itajadiliana na nani wakati mmiliki wa Dowans hajajulikana, Dk. Rashid alisema, "Hayo si yangu. Ni mambo ya wanasiasa. Sisi tumetoa ushauri kwa serikali kwamba tunataka mashine za kuzalisha umeme…"

Alipoulizwa kwa nini TANESCO isishauri serikali kutaifisha mitambo ya Dowans, kwa hoja kwamba kampuni hiyo ilitapeli serikali kwa kurithi mkataba wa Richmond kienyeji alisema, "Hilo siwezi kulizungumzia."

Waziri Ngeleja hakupatikana kujibu swali kwa nini TANESCO inataka serikali kufanya mazungumzo na Dowans badala ya kuingia katika mchakato wa zabuni.


Utapeli juu ya utapeli - UFISADI ULIOKUBUHU.​
 
na hivi majuzi nimesoma mahali (sikumbuki gazeti) kwamba makamu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mahesabu akisema kamati haijawahi kufikia azimio kwamba mitambo ya dowan inunuliwe. makamu mwenyekiti huyo amedai wanamgoja zitto kwenye kamati wamkaange. kama hili ni kweli ni vyema kumuuliza mheshimiwa zitto "kulikoni?"
 
Halisi,

Vipi Mkuu bado unasubiri kupewa mji?.......hebu weka mavitu Mkuu tuanza kumkoma Nyani hapa hapa...kabla hatujaanza kupoa
 
Jamani huyu mwali mbona kakawia hivi? watu tumenawa hadi mikono imekauka pilao halionekani; MMkjj, Halisi, msijabadili mawazo mawazo dakika za mwishomwisho? siku hizi hatumwamini mtu hadi tuone!!
 
Hivi kweli kuna siku tutaamka asubuhi tukute breaking news RA kapelekwa kisutu halafu katupwa keko? What a wonderful day in the history of mother Tanzania! Siku hiyo ndio itakuwa ni siku ya uhuru wa kweli wa Tanzania! Sio wa bendera tena! Na ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa genge la mafia kuitawala TZ! Nchi itarudi mikononi mwa wananchi!!!!

Inapaswa kuwa Public Holiday!
 
The bottom line here is that in the higher levels Dowans aka Richmond is known who it belongs to. Critically looking at it, it seems all the lot smells this scam! Remember what happened to the first culprits? Nothing. They are enjoying the loot and even using it now against the establishment to be able to topple it and come back to loot more. Why action was not taken against them like confiscating angalau the 'visentis'? Walitengeneza kampuni hewa hapa na kutafuta wazungu wa kwa Mandela ili ionekane ni ya nje! The whole thing is so clear. The problem is that the whole house needs cleaning but who to take the broom and start. If the cleaning is not done now, we are doomed. Guys and gals what do we do? Any suggestion?
 
Men, do we need to identify who is Dowans?
The intimacy that exists between Edward Lowassa and Rostam Aziz cannot be mistaken for something else apart from being the matsermind of Richmond and Dowans! We want them at the Kisutu Magistrate Court and later Keko! Fullstop.
 
Men, do we need to identify who is Dowans?
The intimacy that exists between Edward Lowassa and Rostam Aziz cannot be mistaken for something else apart from being the matsermind of Richmond and Dowans! We want them at the Kisutu Magistrate Court and later Keko! Fullstop.


Unataka watangaze au?

Maana tayari tunajua ni RA, Manji na EL na ndio maana walikutana Dubai last weekend kujaribu kunegotiate madeni yasiyolipika ya Dowans
 
Kichekesho ni kwamba tulifikiria kutaifisha mitambo ya Dowans (as an option) bila kufahamu kwamba mitambo hiyo imewekwa kama dhamana kwa mikopo waliyochota benki..Fedha ambazo haijulikani zimetumika au zimekwenda wapi..
Sasa wanabodi pigeni mahesabu kwanza hela wanazochota toka kwetu kisha jumlisha na zile walizochota benki......
Ehhh Mungu weee tumeliwa vibaya jamani!
 
Utamu wa hadithi unaanza hivi
Paukwa Pakawa paliondokea...............halafu mwisho wa hadithi itakuwa utamu kolea.
This is more than interesting. Kagoda ni mdudu mtu, ukweli upo wazi lakini longalonga nyiiingiiii mpaka 2010 mdudu mtu anakuwa ametoweka au amefariki ghafla bin vuu jalada lime limefungwa wadanganyika wenzangu tuanze na kesi za uchaguzi hizo mpaka 2015 halafu linakuja lingine sijui wanajua wao wenye mamlaka halafu mnasema turudi nyumbani maisha bora kwa wachache wengine tufe njaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom