Jumatano ya tar.12 nilikuwa safarini kuekekea Mara kwa shughuli fulani ya ofisi. Nilipofika maeneo ya mji mdogo wa Tinde Shinyanga nikawasiliana na ndugu yangu aliyepo chuo cha sayansi ya tiba Bugando.
Akanitaarifu kuwa atakuwa kwny kongamano na naibu waziri wa viwanda na biashara Lazaro Nyalandu kuanzia saa 8 mchana pale Nyanza club.
It was within my schedule kupumzika Mwanza then the day after nielekee Sirari, so haikuwa big deal mimi kujongea pale Nyanza Club kumsikiliza bro.Nyalandu.
Kongamano lilihusisha wanafunzi wa vyuo vinne vya elimu ya juu Mwanza, kikiwemo SAUT, CBE,Bugando na OUT.
Mr.Nyalandu alichelewa kidogo kufika bt baada ya kuhutubia ukafuata utaratibu wa maswali, na Bro.Nyalandu alionekana kuyamudu vema.
Ilipokaribia saa 6:00pm mkuu wa chuo cha CBE ambaye ndiye aliyekuwa anaongoza mjadala akatangaza kuwa huo ndo mwisho wa maswali na akamkaribisha Nyalandu kufunga kongamano.
But badala ya kuaga Nyalandu akatoa nafasi moja ya upendeleo kwa mtu mmoja. Fursa hiyo ikamwangukia kijana mmoja wa SAUT aliyeonekana ana morali kubwa ya kuuliza.
Huku akishangiliwa na ukumbi mzima, na akiongea kwa hisia kijana huyo akamwuliza Nyalandu swali lifuatalo ambalo sina hakika kama nimemnukuu ipasavyo.
Alisema "wewe kama waziri wa viwanda na biashara ni wazi kuwa ofisi ya msajili wa makampuni (BRELA) iko chini yako, na kwa kuwa BRELA ndiye msajili wa makampuni yote nchini, it means ofisi yako pia ina taarifa zote za makampuni yaliyosajiliwa nchini. Kwa mantiki hiyo naomba utueleze leo kuwa ni nani mmiliki wa Dowans, na ilisajiliwa lini nchini?"
swali hilo lilibadili hali ya hewa ya kule ukumbini kutokana na watu wengi kushangilia na kupiga kelele huku wengine wakimbeba muuliza swali.
Baadae Nyalandu akajibu akijaribu kkwepa hoja. Wanafunzi wakapiga keleke "MAJIBUUU",
Then Nyalandu kwa kujitahidi sana akasema "kwa kuwa issue ya Dowans ina wazungumzaji wengine, mimi naomba nisiizungumzie kwa leo, but mniruhusu nijibu maswali mengine. Nitaifuatilia maana kwa sasa sina taarifa za kina."