Kwa vile Mwakyembe ameamua kuchimba dawa iwe marufuku, tujaribu kumsaidia na Economics za such a scheme. Yafuatayo ni mawazo yangu tu, they are open to criticisms; nia yangu ni kuja na kitu cha kuanzisha mjadala towards hii solution. Nitatumia route ya Arusha – Dar-es-salaam. Tuanze na assumptions kuu kama ifuatavyo:
1. Moja, kwa wastani, binadamu huenda chooni kati ya mara tano na saba kwa siku. Ili kupata namba iliyokamilika, tutumie namba 6 (sita) kama idadi ya trips za mtu kwenda chooni in a day.
2. Mbili, umbali wa Arusha to DSM ni kama kilometa 600.
3. Tatu, safari ya Arusha – DSM kwa wastani huchukua masaa (10) kumi.
4. Nne, idadi ya mabasi kwa siku (kwenda na kutoka Dar/Arusha) sio chini ya mabasi 50. Kila basi linabeba wastani wa abiria 55. Hii ina maana kwa siku, njia ya DSM – Arusha inatumiwa na abiria at least 2,700 (elf mbili na mia saba).
5. Tano, iwapo safari ya Arusha – DSM inachukua wastani wa masaa kumi na iwapo kwa wastani mtu anajisaidia mara sita kwa siku, then katika masaa kumi ya safari ya Dar-Arusha/Arusha-Dar, mtu atahitaji kujisaidia 1.6 times. Lakini ili tupate namba rahisi kuitumia, lets round it up iwe mbili (2) na ku assume kwamba katika muda wa masaa kumi, wastaniwa idadi ya matumizi ya choo kwa mtu ni mara mbili (2).
6. Sita, katika mazingira ya safari, haja ndogo huchukua wastani wa dakika mbili (2), na haja kubwa wastani wa dakika tano (5). Hivyo wastani wa mahitaji ya abiria kujisaidia katika kila kituo ni dakika 3.5 (average ya haja kumba na ndogo). Tutumie dakika tatu (3) for simplicity reasons.
Tumeona kwamba kuna jumla ya mabasi 50 yanayosafiri dar- Arusha na Arusha – dar kwa siku, hivyo kwa wastani, kila route ina mabasi 25 kwa wastani. Mabasi haya huondoka kwa awamu nne kama ifuatavyo: 6AM, 7AM, 8AM, na 9AM. Tukigawanya awamu hizi nne kwenye jumla ya mabasi 25, tunapata idadi ya mabasi 6; na haya mabasi sita yatakuwa yanafika after every hour kwenye kituo cha kwanza kwa kujisitiri. Kila basi lina abiria 50 kwa wastani, Kwahiyo kila baada ya ONE HOUR, kutakuwa na jumla ya mabasi 6 yenye jumla ya abiria 300 katika vituo hivi vipya. Sasa ili kila abiria apate dakika tatu za kujisaidia, kama kuna choo kimoja (one passanger at a time), ina maana muda utakaotumika kuhudumia mabasi haya sita yenye abiria 300 ni dakika 900 (sawa na masaa 15) iwapo kutakuwa na choo kimoja. Sasa ili ili tuweze ku spare only ONE HOUR kwenye kituo, ina maana serikali inatakiwa kujenga jumla ya vyoo kumi na tano (15) ili abiria 300 wanaoshushwa na mabasi sita kila baada ya saa (jumla ya abiria 300 per hour) wasikae zaidi ya ONE HOUR katika kituo cha kwanza cha kujisaidia kwa kujisitiri.
Tukumbuke kwamba hii ni kwa mabasi 25 ya route ya DSM – ARUSHA, Kwahiyo kwa mabasi ya route ya ARUSHA – DSM, serikali pia itabidi kujenga vyoo vingine kumi na tano (15) to serve abiria wa upande ule mwingine ambao pia watakuwa abiria 300 after every one hour.
But this is where it gets trickier:
Tumeona kwamba abiria atahitaji kutumia choo mara mbili ndani ya muda wa safari ya masaa kumi yenye umbali wa kilomita 600 KM. Hii ina maana kwamba inabidi serikali ijenge vyoo kumi na tano Kilometa 180-200 kutokea DSM kwenda Arusha (kabla ya kufika njia panda ambako kuna vyoo tayari kwenye ile sehemu ya mapumziko na vyakula inayomilikiwa na mwenye mabasi ya Dar Express) ili abiria wa DSM – ARUSHA waweze kutumia vyoo kwa mara ya kwanza tangia waanze safari ya Dar – Arusha, halafu matumizi ya pili ya choo ndio yawe pale kwenye vyoo vya njia panda vya Dar Express. Baada ya ya hapa, abiria wa DSM – Arusha hawatakuwa na fursa nyingine tena ya kujisaidia mpaka mwisho wa safari – yani Arusha. Same principle will also apply kwa abiria wanaotokea Arusha kwenda ambapo pia kutahitajika ujenzi wa vyoo vingine kumi na tano (15) kilometa kati ya 180 – 200 kutokea Arusha kwenda Dar, halafu hawa pia watapata fursa ya kutumia choo kwa mara ya pili pale kwenye vyoo na restaurant ya dar express, na na baada ya hapo hapatakuwa na fursa tena ya kutumia choo mpaka mwisho wa safari – yani Dar-es-sa;aam (ubungo).
I have not taken into account ya gharama za ujenzi wa vyoo hivi jumla ya at least 30, pia gharama za usafi, ulinzi ili watu wasiibe vitu kama mbao na mabati, na pia gharama za maintenance (mfano repairs za hapa na pale, kukata nyasi nyoka wasiingie n.k). Nadhani vyoo vya shimo would be more suitable. Vile vile masuala ya tissues na maji ya kunawa, my assumption ni kwamba abiria watajihudumia wenyewe katika haya.
Haya ni mawazo yangu tu ya haraka haraka ambayo kuna uwezekano nikawa way off, lakini angalau tupate sehemu ya kuanzia na mjadala, hasa kubadilishana mawazo kuhusu the best way forward.