Mwakyembe: Marufuku abiria Kuchimba dawa njiani

Mwakyembe: Marufuku abiria Kuchimba dawa njiani

Kwa muda huu kabla 01 Septemba 2012, serikali inapaswa kujenga sehemu maalum za kujisaidia, kama ile ambayo iko njiani kuelekea Mto wa mbu ukitokea Makuyuni (Arusha), ikifanya hivyi hiyo sheria itakuwa na nguvu.
Ingawa inasikitisha kuna sehemu za kuchimba dawa zingine zina vyoo lakini watu hawaingii chooni wamezoea pori kama ilivyo njia ya Iringa eneo la kuchimba dawa kabla ya kufika Mafinga ukitokea Makambako.
 
Heading za magazeti ya kesho na waandishi wetu uchwara"KUCHIMBA DAWA BARABARANI MARUFUKU" utadhan hcho ndio cha muhimu alichokiongelea kwny hotuba nzima
 
Big up Dr kwa uamuzi wako. Ni aibu sana na ni ufinyu wa mawazo baada ya miaka 50 ya Uhuru tunawaza mawazo ya kizamani. Kuna shida gani kila Halmashauri kujenga "rest areas" katika maeneo yao? Hebu tubadilike kifkra. Yeyote anayempinga Dr anadhihirisha uzamani. Kumbukeni sisi siyo mbwa ni wanadamu....... Big up again Dr. Kanyagia hapo hapo mpaka kieleweke.....

Hakuna anayempinga ndugu yangu isipokuwa busara ya kawaida inatutuma kwamba ilitakiwa ahakikishe hayo uliyoshauri yanafanyika kwanza kabla ya kupiga marufuku. Ngoja tu tusubirie hiyo vita itakayokuwepo kati ya makonda na hao abiria watakaokuwa wanajisaidia ndani ya mabasi, sipati picha hali itakavyokuwa! Achana na kubanwa haja ndugu yangu, ni kitu isiyokuwa na ujanja ile!
 
Walau tuwe tunatoa matamshi yenye tija, tuache uchochezi, asa hii mwananchi wa kawaida inamsaidia nini, meli za usafiri zimekushinda unadhani utatokea huku? Heshima yako inashuka
 
Vijengwe vyoo kila baada ya kilomita kadhaa au kila miji iliyopo katika barabara kuu.
 
Da sasa watu watajisaidia wapi? si wangejenga vyoo kwanza. Inaoneka haja imekuwa sio call of nature tena. So gari likiharibika inabidi msubiri lift muende al-jazeera du!
 
Hivi does he has any idea ya mkojo wa mjamzito??? Hauzuiliki jamani! Pathetic waziri!
 
Halafu tutaumwa magonjwa hayana jina! Hatuna usafi stahiki, bado sanaaaaaaaa! Kwasababu wao wanafly kila siku!
 
sipati picha pori la ushirombo mpaka nyakanazi bila kujisaidia balaa!hapo ujue kuna biashara ma bus ya mchina

Hakuna pori Ushirombo! Kuna vijiji Hadi kufika Nyakanazi Kama Kaniha, Lunzewe etc etc
 
Hana busara angejenga kwanza public toilet kwenye barabara zote ndio atoe hili tamko, kwa mfano unatokea ruvu kwenda Chalinze kama ni mgonjwa wa kisukari huwa anakojoa mara kwa mara atafanyaje hapo katikati?

Hajui alisemalo kwani ni jambo ambalo linahitaji kwanza kuandaliwa mazingira , ukiwa unasafiri tumbo likachafuka na mabasi yetu hayana vyoo itakuwaje? aseme mabasi ambayo hayana vyoo atayafunga then ndio anaweza kutekeleza hili .
 
Meli imepinduka inchini zenji sio Tanganyika na tena kama inchi ina waziri wake ambaye tayari keshabwaga manyanga
 
Anaweza asiisome hii thread kwani amesema haamini data za Jamiiforums!
 
ugonjwa wake umempa kichaa, jenga vyoo kwanza ndo useme huu ujinga daktari.

Kumbe bado anahitaji kurudi India haraka sana naona side effect za sumu bado zina msumbua Mwakyembe! Dose ilikuwa kubwa hivi? Nadhani hajawahi kubanwa na haja safarini huyu.
 
0142.jpg au kid-peeing.jpg
 
ni ujinga mtupu,
ni kiburi cha mpanda ndege,
ni uvivu wa kufikiri,
ni kupenda sifa,
ni uwezo wa kufikiri umeshuka

AKAFANYIWE SCAN YA KICHWA PENGINE BADO ANASUMBULIWA NA MARADHI
 
Heading za magazeti ya kesho na waandishi wetu uchwara"KUCHIMBA DAWA BARABARANI MARUFUKU" utadhan hcho ndio cha muhimu alichokiongelea kwny hotuba nzima
.
Kama inavyochangiwa hapa jf. Kama alivyoiongelea yeye kiudakuudaku. Kama vile watz tunavyopenda udaku udaku !
 
Vyoo vyao wanashindwa kuvimaintain vichafu na havina maji mf pale mizani kabla ya chalinze ukiwa umetoka wami aibu tupu mzani hauna hata 3 yrs tayari vyoo vibovu tunapiga hukohuko msituni kwenda kashughulikie maswala ya msingi kaa msongamano dar unaanza eti sio maadili mtu mzima hapa kijana pale! Jela je?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom