Mwakyembe: Marufuku abiria Kuchimba dawa njiani

Mwakyembe: Marufuku abiria Kuchimba dawa njiani

Mtu mwenye afya ambaye haumwi, kunya au kukojoa porini sio kuchafua mazingira kwani Kinyesi cha mtu mwenye afya ni mbolea.

Na hivi ni watu wangapi huko vijijini wasiokuwa na vyoo wanaokunya huko porini? Mazingira barabarani yanachafuliwa na utupaji wa taka dirishani kutoka kwenye magari.

Ukisafiri barabara zetu kuu utaona mita tano kando kando ya barabara zimejaa makopo, chupa za plastiki, mifuko ya rambo na takataka nyingi sana zisizooza.

Tukiendelea kwa mwendo huu kwa kulifumbia macho tatizo hili litakuja kuwa janga la taifa huko mbeleni. Hichi ndicho Mwakyembe angefaa akivalie njuga.

Hakuna ubishi huyu waziri kajilewesha sifa za kiCCM make kakurupuka bila hata kufikiri kidogo.
Ila kuhusu post yako kinyeshi cha ninadamu sio shwari kutupwa ovyo kwani kina mabaki ya ya chakula (especially elements of life) na kemikali zilizohusika katika mmengeny'o tumboni ambayo kwa pamoja vinaweza kusababisha ukuaji wa vijidudu (microorganism) flani ambavyo vinaweza kuleta madhara kwa binadamu, wanyama na mazingira kwa ujumla.

Ila kwa vile huwa uchimbaji dawa hufanyika sehemu isolated na mabali na makazi ya binadamu nafikiri hii practice inaweza kuendelea mpaka pale vitapojengwa vyoo katika maeneo husika ili kulinda mazingira.
 
Kwa kweli huu huwa ni msaada tu wa madereva wa mabasi kwani ukiangalia economics zake, hauna faida yoyote kwa mwenye basi kwani muda hupotea; kwahiyo ni vyema tusiwaangalie madereva wa mabasi kama vile hawajali utamaduni wa watanzania; hili suala ni demand-driven na ni abiria ndio uendekeza, vinginevyo sheria mpya itafaidisha zaidi wenye mabasi kuliko inavyodhaniwa.

Sio msaada, wanafanya hivi kusudi ili kutopoteza muda- kama gari likisimama katika kijiji au mji. Kwa mfano basi linapotoka Mbeya likifika Makambako dereva anaingia stendi na kutoka (ni lazima kulipa ushuru) halafu anakwenda kusimamisha basi baada ya km. 5 hivi na kuwaambia abiria wakachimbe dawa.

Anajua wakiwaambia abiria wakajisaidie wakiwa katika stendi watafanya na mambo mengine km kula, kununua vocha, au kufanya manunuzi mengine. Kwa hiyo muda wa kusubiriana utakuwa mrefu, isipokuwa porini hakuna atakaekwenda mbali kwa kuogopa kuachwa au kudhuriwa na wanyama.

Siku hizi miji midogomidogo ni mingi katika barabara kuu zote, ni swala la uamuzi tu, wananchi wanaweza kujenga vyoo.Kujisaidia porini kubaki kama dharura tu. Jamani tutunze mazingira, msitetee uchafu na ujinga.

Tutofautishe binadamu na mnyama, unaposafiri na mkwe wako, au mtoto wako wa jinsia tofauti kwa nini iwe taabu? WATANZANIA TUJIREKEBISHE KAMA NCHI NYINGINE INAWEZEKANA KWA NINI SISI TUSHINDWE? Hata la vyoo tusubiri wafadhili?
 
Back
Top Bottom