Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Inasikitisha sana kuona wasomi kama hawa wanaamua kuchagua kifo chao wenyewe kuliko cha chama chao, Aliombwa sana ahame akasema yuko tayari kufa akisema ukweli sasa kweli inakuwa. CCM siyo mama yao Mwalimu mwenye kadi namba moja alinena wao wanang'ang'ana tu! Si vizuri kuwacheka lakini ni wasomi wanajua CCM walivyo wauaji hebu ikumbukeni orodha hii na mazingira ya vifo vyao:

HORACE KOLIMBA
IMRAN KOMBE
GIBONCE MWAIKAMBO
NZUGILE JIDULAMABAMBASI
SAMSON KIPEPE
OMARY MBANO
PAULIN MPUYA
SALOME MBATIA N.K

Nashukuru mungu hata rafiki yangu Dr Masumbuko Lamwai alibadili tabia yake ya kuusema ukweli kama ulivyo baada ya kuhamia CCM naye angekuwa marehemu kweli ingawa sasa hivi ni marehemu kisiasa lakini kimwili tunaye, kama hamwajui ni WABAYA HASWA
N

hivi samson kipepe ilikuwaje members?nakumbuka alikuwa naibu katibu mkuu uvccm na mkuu wa utawala na fedha
 
I want to believe that these cowards will pay for their sins here on earth. We wish Dr. Mwakyembe and all other victims of evil strengh and quick recovery.
 
DR alikua lazima adhurike ingebidi achukue tajadhari zaidi sema aliwadharau mafisadi na nguvu zao na nia yao ya kutawala nchi na kuficha maovu yao...anyway tunawajua hili kundi na ipo siku watalipa kama si wao basi vizazi vyao vijavyo
 
I want to believe that these cowards will pay for their sins here on earth. We wish Dr. Mwakyembe and all other victims of evil strengh and quick recovery.

Yah, Those that belongs to CCM will definitely pay
 
Du, mamvi nomaaaaa, kumfanya hivi magamba mwenzake ndiyo nini?

Mnamwonwa EL bure jamani! ipo siku ukweli utadhihiri ndo mtajua! wote tunajua nani mbaya hapa! Kumbukeni Nguza na wanae wote akiwamo na Papii walifungwa maisha kwa kesi ya kutunga tu kisa kisasi sababu ya dem.

Huyu ndiye muuaji kama hamju basi kinachoomuondoa Mwakyembe ni ile siri aliyoacha kutueleza kwenye sakata la Richmons/symbion mwenye richmond anaogopa ipo siku Mwake anaweza kusema!

lakini inasikitisha sana! Prof. Mwakyusa aliuwawa, Prof Mwandosa hoi taabani sasa Mwakyembe yani jamaa muuaji sana huyu daah!
 
Ndio maana wengine mambo ya imani tulishayashtukia haya make sense long time ago. Mungu angekuwa ana nguvu ya kuponya mtu basi angekuwa na nguvu ya kuzuia mtu asiteseke in the first place. Na kwa nini mpaka aombwe? Hivi wewe ukiona mtoto wako anaumwa utasubiri jirani na ma stranger wengine waje wakuombe na kubembeleza ndio umsaidie? Sisi si tunaambiwa ni watoto wa Mungu? Mungu gani hana huruma kuliko baba wa kibinadamu?


Ha! ha! ha! Kwenye shari kuna kheri ndugu! Sifa kubwa ya Mungu wetu mkuu huwa asemi yeye hutenda si kama kikwete yeye anasema tu! Sasa huileta shari kwetu ili katika shari hiyo ipatikane kheri mara mbili! kuugua mpaka kufa kwa Mwake labda!!(maana kufa lazima mtu ufe) itapatikana kheri kubwa tusubiri!
 
haya sasa ni kama mambo ya KEnya ambapo akina Tom Mboya, Ronald Ngala, JM Kariuki, Gama Pinto, nk waliuliwa na kundi lenye ulafi na uroho wa madaraka la serikali ya KEnyatta na haswa wale kiambu mafia (watu kama akina Mbiyu Koinange, Charles Njonjo, Dr Njoroge Mungai, James GIchuru, Gitahi Kariuki, Ben HInga etc) na baadae Moi na washamba wake wa kikalenjin wakaja kuwaua akina Masinde Muliro, Bishop Muge, Robert Ouko kwa sababu zile zile kuwaona kuwa ni wanahatarisha ustawi wao binafsi unaoletwa na madaraka ya serikali...

similarities kubwa za haya niliyoyaonyesha hapo Kenya na hapa kwetu Tz ni kwamba mantiki ni ile ile kuna kundi lililopata utajiri kwa njia chafu likiwa kwenye madaraka na linapigana kwa nguvu zote kung'ang'ania hayo madaraka ili kulinda mkate wao na maovu yao..wakikuona unatishia hilo wanakumaliza kwa njia zozote-kisiasa au kimwili na kiroho kama kamanda wetu Mwakyembe

Hili kundi ni hatari sana na katu halitatamani kuachia madaraka wataendelea kupandikiza viongozi ili walindwe, wataendelea kuingiza nguvu mpya na damu mpya kwenye kundi lao ili nguvu yao iendelee..wakiona vipi watapandikiza watu wao hata vyama vya upinzani ili kujinusuru na hata mpinzani wa kweli akiingia watawanunua washirika wake ili awe isolated mwenyewe na kazi isifanyike....



.mungu ibariki Tanzania
 
If it all, Mwakyembe was poisoned then we need justice done. We also want to know Oct 14, 1999 full report. What had happened to founding father of the nation of Tanzania>
 
Eeh Mungu, Mungu wa Isaka,Mungu was Ibrahimu uko wapi utusaidie Watanzania maana TUNAANGAMIA!!!
Yale maneno ya Rais KIWETE aliyosema kuwa kwa sasa CCM watu wana windana mtu hawezi akaacha glasi ya maji au wisk mezani akiwa na wenzake maana wanaweza KUMFANYANYIZIA sasa YAMETIMIA.

Watu tunasema kila siku kuwa CCM hakika ni Chama Cha Majambazi na Mafisadi lakini kwa vile watu wamerogwa na ri-CCM wanaendelea kulipigia debe na kushangilia, sasa haya ndiyo matokeo yake. CCM ni WAUAJI wanaotisha sana!

Kinachoonekana hapa kwa sasa ni CCM OPERATION KILLING OF PRESIDENTIAL CANDIDATES 2015!!!!
 
Inasikitisha sana, mtu mwenye afya njema, asiye na rekodi yoyote ya magonjwa yenye utata zaidi ya magonjwa ya kawaida kwa wanadamu, anabadilika ghafla kuwa katika hali hii ya kusikitisha.

Hata hiyo, kwa Neema zake Mwenyezi MUNGU Dr Mwakyembe atapona na kurudi nyumbani akiwa mzima wa afya. Na hapo ndipo walafi hao wachache, wenye roho mbaya kwa Watanzania wenzao watakapouona Ukuu wake Mungu pale atapojinyanyua kwenye ugonjwa wa ndugu yetu Dr Mwakyembe.

Pole sana ndugu yetu, simama katika yeye Yesu Kristo, aliye Mkuu kuliko wote.
 
hivi samson kipepe ilikuwaje members?nakumbuka alikuwa naibu katibu mkuu uvccm na mkuu wa utawala na fedha

Umemsahau Marehemu Stephen Kibona aliyeuawa akiwa Waziri wa Fedha, taarifa ya kifo chake hadi leo hii ni siri!!!
 
Hata Mwakyembe naye ni gamba pia. Siungi mkono kitendo alichofanyiwa kuwekewa sumu ili kuondoa roho bali sikubaliani na tabia ya Mwakyembe ya kukaa na siri moyoni kuhusu Richmond kwa sababu ya manufaa yake.

Aliamua kunyamaza na kutosema siri iliyofichika nyuma ya pazia, kwa sababu hiyo akapewa Unaibu Waziri. Kibaya zaidi, ni watu hao hao unaweza kukuta ndiyo wako kwenye mpango wa kumuondoa.

Ni bora atoe hiyo siri kuliko kunyamaza huku watanzania wakiendelea kutaabika na giza totoro na ufisadi.

Hebu acheni unafiki wenu, baada ya ripoti kutoka na kusababisha kuvunjwa kwa serikali mlifanya nini, kwa nini nanyi hamkusimama na kuanzisha harakti kumtoa huyo JK mnayetaka ang'olewe na Mwakyembe!!!

Tatizo lenu mnasubiri watu wengine ndio wawaletee neema, wakati nyinyi mkichificha nyuma ya kuta, acheni upuuzi wenu huo.

Kazi aliyoifanya na wajumbe wa kamati yake ilikuwa ya mfano, ilivunja serikali, mkalemaa jamaa wakaendelea kutawala wakati ilitakiwa kufanyika uchaguzi mwingine, leo mmebaki oh atoe siri, siri gani itayowaondoa waoga na wanafiki nyie huko mafichoni na kudai haki zenu!!!
 
Yote yawezekana kwake anayeamini,Tuamini kwamba mwakyembe atapona In JESUS NAME.Umayesoma sema Amini!!
 
wakuu tuchange tumpeleke nigeria kwa t b joshua

Ni wazo zuri.
Nasikia Lowassa alishawahi tayari kwa TB Joshua na akapewa unabii wa Urais mwaka 2015! Bila shaka Mwakyembe akienda ataambiwa na prophet Joshua tatizo na chanzo cha ugonjwa wake. Kama Lowassa ndiye aliyehusika na mkakati wa kumpa sumu yote yatawekwa wazi maana Mungu huwa hasemi uongo!

Kama itatokea huyu bwana akaenda huko surely it will be a very interesting news.
 
inasikitisha sana..halafu ukifuatilia na kufanikiwa kupata ukweli wa kwanini wanataka kunyamazisha utakuta ni kwa manufaa ya kuihujumu nchi na walalahoi wake,wivu, kuoneshana ubabe na sababu nyingine zisizo na msingi..!! we should respect and value life bana,we are not GOD to end another one's life!
 
DR alikua lazima adhurike ingebidi achukue tajadhari zaidi sema aliwadharau mafisadi na nguvu zao na nia yao ya kutawala nchi na kuficha maovu yao...anyway tunawajua hili kundi na ipo siku watalipa kama si wao basi vizazi vyao vijavyo


Hivi kwenye hiyo tume alikuwa peke yake mpaka aandamwe yeye tu?? Binafsi cant buy that unless kuna kitu kingine ambacho hakisemwi. Yeye alikuwa Mwenyekiti tu wa hiyo kamati ambayo ilikuwa na wajumbe wengine. Sasa inakuwaje wajumbe wengine hawajui kile anachokijua Mwakyembe?? Labda mseme kuna uchunguzi aliokuwa anafanya bila kuwashirikisha wenzake!!
 
Back
Top Bottom