Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Ivi hao waliompa sumu wanadhani wataishi daima?
Wote tutauonja umauti!
Ole wenu mkifika mbele ya mola sijui mtajibu nini juu ya huu ufukunyuku mlioufanya
 
Nataka kujua huyu mnafiki Sitta kaenda kwa nauli yake au kodi zetu? Hawa jamaa wanatunyonya sana, hawajui hata bei ya ticket ya ndege kudadeki. Pole Mwakyembe, ndio madhara ya unafiki, ungemaliza kazi siku nyingi lakini ukaficha vielelezo wabaya wako wakanusurika na sasa wamekukuta kwenye anga zao. Ukitoka Mungu mkubwa, tunakuombea lakini tunajua Pollonium ni kitu nyingine kabisa
 
Hii ni DHAMBI ambayo katu WANYAKYUSA hawatoisamehe CCM na JK kama chochote kitawatokea MWAKYEMBE na RAIS wa Wanyakyusa Prof.MWANDOSYA.Mungu awapiganie warudi salama.
 
Nimepata hofu kuu, na kijasho chembamba kinanitoka wakati nasoma ripoti ya Jason Bourne, kama ni kweli basi naamini Tanzania sio sehemu salama kuishi..Aisee inatisha sana.
 
Sasa Magamba Wanataka Kuuwa WATU Woote wenye akili na uelewa!! Wanataka Nani aongoze Hii Nchi? Wanataka watu Design ya Lusinde? Duh Huruma hadi Aibu Kwa Taifa!!

Hata Mwakyembe naye ni gamba pia. Siungi mkono kitendo alichofanyiwa kuwekewa sumu ili kuondoa roho bali sikubaliani na tabia ya Mwakyembe ya kukaa na siri moyoni kuhusu Richmond kwa sababu ya manufaa yake.

Aliamua kunyamaza na kutosema siri iliyofichika nyuma ya pazia, kwa sababu hiyo akapewa Unaibu Waziri. Kibaya zaidi, ni watu hao hao unaweza kukuta ndiyo wako kwenye mpango wa kumuondoa.

Ni bora atoe hiyo siri kuliko kunyamaza huku watanzania wakiendelea kutaabika na giza totoro na ufisadi.
 
Nimetokwa machozi nilipoona picha ya Mh Mwakyembe gazeti la mwananchi ya leo akizungumza na Sitta akiwa bado hosipitalini. Mwli wake umekuwa kama nyoka. Kama ni watu walimpa sumu ili watu wapate madaraka walaaniwe

Dah! Tumwombeeni apone!
 
POLONIUM-210 not possible

sijaandika hiyo kishabiki najua wengi hapa hawajui kwani inaitwa POLONIUM-210. Rejea somo la kemia ukiwa form two, atomic number for polonium is 84 while its mass number is 210 and as long as polonium is unstable element its is written as POLONIUM-210.
 
Kweli inauma sana, ila kama kuna wanafamilia wa Mwakyembe anasoma hii comment naomba muwe mnasoma zaburi 35 kila siku mpaka atakapopona, zaburi ya 46, na 109, hii ni kwa ajili ya mgonjwa na pia ni njia nzuri ya kuwashughulikia maadui zenu.

Ingekuwa vizuri kama mke wake angekuwa anasoma. Mgonjwa mwenyewe awe anasema haya maneno kila siku Maombolezo 3:22-23, Yakobo 5:15-16, Zaburi 20 yote.

Awe na moyo wa kusamehe yote, hakika Mungu atauokoa uhai wake na kaburi. Maana imeandikwa katika Marko 16:18b hata wakinywa kitu cha kufisha hakitawadhuru kabisa.

I hope anybody who is closer to this family will take this very seriouse. Hulituma neno lake lipate kutuponya na kututoa katika maangamizi. I will keep praying for him
 
Ivi hao waliompa sumu wanadhani wataishi daima?
Wote tutauonja umauti!
Ole wenu mkifika mbele ya mola sijui mtajibu nini juu ya huu ufukunyuku mlioufanya
Ni kweli kabisa halafu wanajifanya wancha Mungu na kwenda makanisani kusali nakuchangia fedha. Mwakyembe na Mwandosya watakufa Mungu akiamua kazi yao hapa duniani imekwisha na nyie wauaji mtaenda wapi ?
 
Napendekeza lowassa na rostam wakamatwe kuisaidia polisi,ushahidi wa kimazingira unatosha kuwatia hatiani kwenye hii issue ya mwakyembe!wauaji wakubwa hawa,na huyo lowassa na kansa yake mungu atamuumbua itamtesa kweli kweli hata akiingia ikulu!
 
Back
Top Bottom