Mwakyembe amechoka, apumzishwe!

Mwakyembe amechoka, apumzishwe!

Nchi yetu ilifika mahali ikawa kama haina wenyewe,Mwakyembe alikuwa sahihi kabisa kosa kubwa alilofanya alikurupuka hakujipanga kuleta hoja na hakufanyia kazi
Tunahitaji wataalam hasa wenye vichwa baridi kuokoa taifa letu wageni wanaoa kila siku hapa Tanzania
Itafutwe jinsi ya kuwabana wageni wanaotumia mgongo wa kuoa mtanzania na kupata uraia
Hakuna nchi yoyote duniani inafanya upuuzi kama huu,yaani unaoa raia na kupata uraia easy like abc
Mwakyembe jipange upya kama kweli wewe ni proffessional ili kujisafisha
Mwakyembe na Makufuli wote wamekurupuka!
 
Polonium Ina tabia ya kujirutubisha isipofanyiwa intensive neutralization.Madhara ya POLONIUM yameanza kuwa wazi kwa Mwakiembe, Raid achukue maamzi magumu ya kumpumzisha Huyu Jamaa na amrudishe INDIA haraka iwezekanavyo.
 
Kwakuwa si kosa kumchukua mwanamke na kuishi naye kinyumba haswa baada ya kukubaliana, basi kwa tangazo la Mwakyembe ndoa zingeendelea kwa jinsi ambavyo vyeti vya ndoa havitolewi
 
Huyu Jamaa mimi ni jirani yake,nataka anieleze pale ikolo kijijini kwetu wale vijana hata jina Rita hawajui maana yake,nataka aniambie office za Rita pale ikolo silikugu?badala ya kuzungumzia barabara ya Darajani -katumbasongwe ambayo muda wote shida unaleta upuuzi,

Umevimbiwa indima sasa hata akili imehama,vyama vya ushirika kyela vipo wapi,amakoko isala isi yanalanguliwa umeshindwa hata kuhoji ilikuwaje vyama vya ushirika kyela vimekufaje unaleta upuuzi ambao mtanzania wa kawaida haumsaidii hasa wanakyela ulitojofu.
 
Nchi yetu ilifika mahali ikawa kama haina wenyewe,Mwakyembe alikuwa sahihi kabisa kosa kubwa alilofanya alikurupuka hakujipanga kuleta hoja na hakufanyia kazi
Tunahitaji wataalam hasa wenye vichwa baridi kuokoa taifa letu wageni wanaoa kila siku hapa Tanzania
Itafutwe jinsi ya kuwabana wageni wanaotumia mgongo wa kuoa mtanzania na kupata uraia
Hakuna nchi yoyote duniani inafanya upuuzi kama huu,yaani unaoa raia na kupata uraia easy like abc
Mwakyembe jipange upya kama kweli wewe ni proffessional ili kujisafisha
Mwakyembe na Makufuli wote wamekurupuka!
Nchi ya wakurupukaji hata makonda alikurupuka akatangaza list kwenye TV kumbe hana ushahidi sasa anadaiwa vyeti kaamua kujitoa fahamu.
 
Nchi yetu ilifika mahali ikawa kama haina wenyewe,Mwakyembe alikuwa sahihi kabisa kosa kubwa alilofanya alikurupuka hakujipanga kuleta hoja na hakufanyia kazi
Tunahitaji wataalam hasa wenye vichwa baridi kuokoa taifa letu wageni wanaoa kila siku hapa Tanzania
Itafutwe jinsi ya kuwabana wageni wanaotumia mgongo wa kuoa mtanzania na kupata uraia
Hakuna nchi yoyote duniani inafanya upuuzi kama huu,yaani unaoa raia na kupata uraia easy like abc
Mwakyembe jipange upya kama kweli wewe ni proffessional ili kujisafisha
Mwakyembe na Makufuli wote wamekurupuka!
Umechanganya mambo humu. Nchi kibao duniani watu wanachukua uraia au resident kwa kuoa au kuolewa. Mantiki ya agizo lake ni sawa lakini utekelezaji wake haukuzingatia jiongrafia na uhalisia wa Tanzania. Utekelezaji unahitaji walau miaka mitatu ikiwa pamoja na kuweka utaratibu wa dawati la Rita katika kila dispensari nchini. Wananchi kuhamasishwa vya kutosha na ikibidi kuondoa na chaji zinazotozwa katika kipindi cha utekelezaji. Lakini vilevile serikali wakati mwingine kama haina "masterplan".
 
MWAKYEMBE AMECHOKA, APUMZIKE/APUMZISHWE.!

By Malisa Godlisten

Jana nilipoona agizo la Waziri Mwakyembe kuwa hakuna mtu ataruhusiwa kufunga ndoa bila cheti cha kuzaliwa nilimpuuza kwa sababu haikua mara yake ya kwanza kutoa kauli za kustaajabisha. Rafiki yangu mmoja alinitania kuwa natarajia kufunga ndoa, je nina cheti cha kuzaliwa?

Nilisema tu kwa kifupi kuwa wendawazimu pekee ndio wanaopaswa kuelewa agizo hilo. Sio kwa sababu "nimebashite" cheti cha kuzaliwa ila kwa sababu agizo hilo ni batili na halina maana. Hata kama watanzania wote wangekua na vyeti vya kuzaliwa bado ningepinga agizo hilo.

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]; agizo hilo ni kinyume cha sheria. Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kifungu cha 9 hadi 24 inaeleza kitu kinachoitwa MASHARTI ya ndoa (Preliminaries to Marriage &Restrictions on Marriage). Masharti yanayoelekezwa na sheria hiyo ni pamoja na:

-Umri (miaka 18 au zaidi, kwa mwanamke chini ya 18 apate idhini ya wazazi)
-Utimamu wa akili (asiwepo mgonjwa wa akili kati ya muoaji/muolewaji au wote)
-Hiyari (asiwepo anayelazimishwa, kila mmoja aridhie)
-Kutangaza ndoa (wanaotaka kufunga ndoa wanapaswa kuandikisha mbele ya msajili wa ndoa walau siku 21 kabla ya tarehe ya ndoa)
-Ruhusa ya kupunguza siku hizo 21 inapatikana kwa Msajili Mkuu wa Tanzania, kwa kujaza fomu ya pekee, kutoa sababu ya haraka, na kulipa ada maalumu. Wasajili wadogo hawawezi kutoa ruhusa hiyo
-Kuwa na wadhamini wawili wa ndoa.

Hayo ndio masharti ya ndoa. Ukisoma masharti hayo hakuna mahali sheria imehitaji cheti cha kuzaliwa. Sasa Mwakyembe ametoa wapi hili agizo? Ameota usiku? Ameshauriwa na mkewe? Amepata wapi? Kutoa agizo ambalo ni kinyume na sheria, ni kuvunja sheria. Na sheria inapovunjwa na Waziri wa sheria ni aibu zaidi.

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]: Kuna watu wanamtetea Mwakyembe kuwa cheti cha kuzaliwa kinapatikana kirahisi. Yani hakuna sababu ya kulalamika kwa kuwa eti ni rahisi kupata cheti cha kuzaliwa. Kiongozi mmoja wa kisiasa akawashangaa watanzania jana akasema watanzania wamezoea kulalamika badala ya kwenda RITA wakachukue vyeti. Yani yeye hakuona ubatili wa agizo la Mwakyembe, alichoona ni urahisi wa kupata cheti pale RITA.

Labda kumsaidia kiongozi huyu na wengine wenye mawazo kama yake, niwaambie tu kwamba hoja sio urahisi wa kupata cheti cha kuzaliwa, hoja ni kwamba agizo la Waziri ni batili na halina mashiko kisheria (null and void abinitio). Sheria ya ndoa haielezi cheti cha kuzaliwa kuwa moja ya requirements za kuoa/kuolewa.

Hatuwezi kuruhusu viongozi watoe matamko ya hovyohovyo ambayo ni kinyume na sheria kwa sababu tu hivyo wanavyovitolea maagizo ni rahisi kupatikana. Itafika mahali watasema watu wasio na kadi za CCM wasipate huduma za afya, na tutaunga mkono kisa tu kadi za CCM zinapatikana kirahisi. Hii sio sawa hata kidogo.!

[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG]: Logic ya cheti cha kuzaliwa ni nini? Yani kuna uhusiano gani kati ya cheti cha kuzaliwa na kufunga ndoa? Kwamba Mwakyembe alitaka kupima nini? Uraia au? Umri? Ukoo? Intention yake nini?

Kama ni uraia, je watu wasio raia hawaruhusiwi kufunga ndoa nchini? Kama wanaruhusiwa, hili agizo lina maana gani? Ninachofahamu ni kuwa kama mtu si raia hakatazwi kufunga ndoa hapa nchini, kama ambavyo watanzania wanaoishi nje ya nchi hawakatazwi kufunga ndoa huko walipo.

Mtu kufunga ndoa Tanzania hakumfanyi kuwa raia wa Tanzania. Na mtanzania aliyeko nje ya nchi kufunga ndoa huko, hakumfanyi kupoteza uraia wake. Sasa kama ndio hivyo logic ya cheti cha kuzaliwa inatoka wapi? Mwakyembe amekula maharage ya wapi?

[HASHTAG]#Mwisho[/HASHTAG]; nimpongeze Rais JPM kwa kufuta agizo hili la "kijinga" ambalo ni kinyume cha sheria. Lakini ni vizuri akampumzisha kazi Dr.Mwakyembe maana ameonesha kuchoka. Kauli zake za siku hizi zimedhihirisha kwamba he is not smart as he used to be. So ni busara ampumzishe tu.

But pia kwa kuwa Mheshimiwa Rais amedhihirisha kwamba anazisikia kelele zetu na anachukua hatua, ni vizuri asikie pia kelele za Bashite na achukue hatua. Haiwezekani kelele za siku moja za vyeti vya kuzaliwa amezisikia na kuchukua hatua, lakini kelele za mwezi mzima kuhusu Bashite hajazisikia. Tafadhali Mheshimiwa Rais chukua hatua na la Bashite pia. Hii itakujengea heshima na kufanya watu waone hauna double stsndards.!

Malisa Godlisten
Naamini Ana mtu standby aliyempa ubunge hivi karibuni. Binafsi nili doubt credibility yake kuhusu Lowassa wakati kamati haikumhoji, sio kwamba nilikuwa nampenda Lowassa, la hasha ni masuala tu ya kuzingatia haki sawa kwa wote.
 
Ueledi wa masuala ya sheria unatia shaka na kuacha maswali mengi ya kujiuliza dhidi ya waziri wa katiba na sheria Dk Harison Mwakyembe!
Uteuzi wake ulipofanyika wengi waliona kuwa wizara imepata mtu sahihi lakini ni kama vile wizara inaendeshwa kwa mihemko na sifa na siyo kwa kutumia ueledi wa taaluma!
Hivi majuzi alitangaza ni marufuku kufunga ndoa kwa mtanzania yeyote kama hana cheti cha kuzaliwa, deadline akasema tarehe 1/5/2017, lakini mapema tu Rais akajibu mapigo kuwa hilo suala alikuwa halijui na limemshtua, Rais akatengua kauli yake!
Sipingani na suala la kuwa na cheti cha kuzaliwa maana hilo ni suala tu ambalo mtu anaweza akalishughulikia kadri ya utaratibu ulivyo na kupatiwa!
Ila mkurupuko wa kusema watu wasifunge ndoa huku hata mkuu wako hukumshirikisha inaonyesha ni jinsi gani Mwakyembe anavyofanya kazi bila kutumia ueledi!
Jambo lingine ni hili alilotamka kuifuta TLS, kwa matamko hayo ni dhahiri kuwa ueledi wake katika taaluma yake ni wa mashaka hasa ikizingatiwa TLS si taasisi ya serikali ila yeye akaingiza matamko yake ya hovyo kabisa!
Sasa wanasheria wanaojua jinsi ya kutumia ueledi wao wamemuonyesha jinsi wasivyobabaishwa kwenye huu uchaguzi wa TLS.
Kama alivyosema Masha naunga mkono Mwakyembe afutiwe uanachama TLS..
 
Anajitahidi labda atamfurahisha aliye juu matokeo take mtu mzima anaumbuka.
 
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wachache tuliolaumiwa kwa KUMKOSESHA UWAZIRI MKUU MWAKYEMBE pale nilipoamua kumtukuza Mungu kwa kupinga wizi wa kura za ubunge Kyela .

Nina majina ya watu waliokuja inbox kunilaumu , lakini najipongeza sana , hivi huyu kama angekuwa PM angekuwaje ?
 
Ashapumzishwa akapige blablah habari maelezo arudi nyumbani mambo ya Sheria hayawezi
 
Huyu Mwaki-embe sijui Mwaki-chungwa nilikuwa namuheshimu sana wakati aliposimamia ile kamati ya Richmond hadi kuiangusha serikali kwa kuonesha wazi kuwa W/Mkuu wa enzi zile alihusika kwenye uchafu ule. But with time, nimetokea kumdharau sana na kuona kumbe hata issue ile ilikuwa ni dili lililopangwa purposely na kikundi fulani kwa maslahi yao. Nasema hivi kwa kuwa mtuhumiwa alipojitokeza na kusema kuwa "wenye ushahidi wa yeye kuwa fisadi waende mahakamani" nilishangaa kuona kimyaaaaa! Na, ndio maana sasa naelewa ni kwa nini mtuhumiwa mkuu wa richmond kabla hajajiuzulu alisema "tatizo ni Uwaziri Mkuu"! Hii inamaanisha kuwa huyu Mwaki-nani sijui amejaa unafiki wa hali ya juu, mtu wa kimaslahi zaidi na anapenda sana kujifunika na kanisa ili aonekane yupo sahihi, hapana, Mungu anakuona.

Haiwezekani mwenzio aondelewe kwenye nafasi yake ya uwaziri kwa kusimamia kile anachokiamini na ambacho kwa mujibu wa wengi alikuwa sahihi halafu uwekwe wewe uliye "safi kiroho", ukubali nafasi hiyo (kwa mshangao wa wengi) na sasa unajaribu ku-justify kuwa mtumbuliwa alikosea! Eti, "Wewe kama mwanasheria ni mwiko na hutapeleka kitu ambacho unaona hakijakamilika kwani kwa taarifa ulizonazo kupitia vyombo vya habari ni kuwa taarifa yote inatokana na ushahidi wa mlalamikaji ambae ni Clouds". Kama wewe ni mwanasheria tena MZAMIVU, jibu swali hili: Ni kwa nini mahakama huwa inaamua kesi kwa kukubaliana na upande mmoja wa mlalamikaji ikiwa mlalamikiwa hakutokea mahakamani baada ya jitihada kadhaa za kumtaka kufika mahakamani kugonga mwamba? Please, give us a break!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom