Wana bodi,
Umofia kwenu. Namwandikia ndugu yangu DR. Harrison Mwakyembe nikiwa nimetoa macho siamini kama huyu ndiye yule mwanasheria machachari wa enzi za Samuel Sitta (RIP). Kama ni yeye basi nadhani kuna tatizo kubwa kichwani kwake. Kifupi mwanasheria huyu ni mwongo hatakiwa kuaminika tena, kapoteza kila kitu kilichokuwa kinawafanya watanzania wamwamini. Kwa tathmini ya haraka, Dr. Mwakyembe amebakiza kiki moja tu ya kumfanya atengeneze headlines kwenye media nayo ni kumkamata Mange Kimambi... zingine zote kafeli kwa aibu mbaya... Nimeona andiko la Uhamiaji la kumkamata Mange pindi akitua nchini. Mwakyembe unatia aibu sana kaka. Hebu tujikumbushe
1. Wewe na marehenu Sitta (sorry marehemu hatetwi) mlituaminisha ufisadi wa fisadi papa wetu Lowasa kupitia Richmond. Mliimba wimbo huu mkamwambukiza Dr. Slaa na baadae wana Chadema. Kipindi cha uchaguzi uliopita, ukijua kuwa si kweli ulitokea Star TV ukaaminisha watanzania na hata Rais Magufuli kuwa ufisadi wa Lowasa ni kesi ya jinai inapelekwa kortini muda wowote. Rais kaingia kingi, akaanzisha mahakama ya mafisadi na mwishoe imekuwa aibu kubwa. Mwakyembe umepatwa nini kaka yangu? Ni ile sumu? Bado nawaza.
2. Ukiwa msomi mzuri, uliikana tasnifu yako ya sheria kutoka ujerumani kipindi cha uandishi wa katiba mpya. Unastahili kuendelea kuitwa PhD holder? Tasnifu yako ni ipi inayokutambulisha duniani kuhusu udaktari wako? Bado una msimamo wa kisomi uliosimamia wakati wa VIVA au msimamo wako ni huu uliouonyesha kipindi cha bunge la katiba? Au ni ile sumu kaka yangu? umekuaje wewe?
3. Wewe ni mwanasheria, mwanachama wa jumuiya ya mawakili wa Tanganyika, kwa makusudi kabisa umeamua kujitoa akili kidogo uliyobakiwa baada ya bunge la katiba na sasa unawavuruga wenzako. Ni nini kaka yangu kinakusibu? Hivi uchaguzi huu wa TLS unakusumbua nini hadi uonekane mbumbumbu kuliko kina Lusinde? Nini kinakusibu kaka yangu? Ni ile sumu au bashiteism?
4. Umekurupuka kuhusu vyeti vya kuzaliwa kutumika wakati wa kufunga ndoa. Ulilenga kuua mjadala wa TLS ulifeli matokeo yake hata Rais kaamua kukudhalilisha, nini kilichobaki ukajivunia kwa wanao na wana Kyela? Mwakyembe uko salama upstairs au unahitaji msaada kaka yangu?
5. Ukiwa waziri wa Katiba na sheria, ukiwa mwanasheria na mwanahabari, ulikuwa msitari wa mbele kutetea sheria kandamizi inayoua ustawi wa vyombo vya habari bila kujali madhara makubwa kwa jamii pana ya watanzania. Ni ile sumu kaka yangu au kuna kingine?
Mwisho, nakuona umebakiwa na silaha moja tu ili uendelee kuwa kwenye game hii. Nayo ni kujitoa kifua kwa kiki ya kumsaka na kumkamata Mange Kimambi. Hii pekee ndo wafuwasi wako watakuona bado una uwezo ambao hauna. Ila hii kiki ukiitumia ndo inakwenda kukupoteza kabisa na hatimaye nafasi yako atapewa Lusinde Kibajaji. Tunakuombea urudiwe na akili yako ya kawaida otherwise ushaanguka kaka.