Hata Hadithi pia ni masimulizi, yaani hapa ni sawa umeandika hivi "Quraan ni masimulizi na masimulizi"(Elimu ya maana za maneno inahitajika sana kwenu).
Chukulia mfano sasa baada ya hizo "Findings" kupatikana aidha iwe michori au mfano wake, maana ya hiyo michoro unairejea wapi kwenye masimulizi au michoro yenyewe unajielezea ? Sasa usiandike mambo kwa mihemko, bali fikiria kisha jenga hoja.
Unapo sema Quraan haina uhalisia bila kuonyesha hilo, hii ni ishara ya kuwa wewe ni muongo, na mpaka unakufa huwezi kuonyesha kutokuwa na uhalisia kwa Qur'aan (Hapa, nacheka sana), ngoja nikupe uhalisia tu mmoja wapo katika Qur'aan,nanukuu :
Anasema Allah mtukufu
34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini. (at - Tur : 34 - 36 )
Sasa ukija tena uje na ushahidi wa kuonyesha ya kuwa Qur'aan haina uhalisia hata kidogo.