Kikwajuni one,
Mwenyezi Mungu ni mwingi wa rehema ameumba binadamu na wanyama halafu wanyama hakwafanya mahayawani bindamu akatupa akili ndiyo hizo tunazozitumia sasa hivi kupingana na mwongozo ndani ya maumbile na kuona kama Mungu hayupo ni stori tu.
Kabla ya kusema mwenyezi mungu kaumba binadamu na wanyama, kwanza prove kwamba yupo. Hujaprove kwamba yupo usharukia kwamba kaumba?
Wapo wapi kina firauni waliokuwa wanajifanya ndiyo Mungu.
Kina Firauni wamekongolewa na entropy per the second law of thermodynamics, kama ambavyo kila kitu kitakongoroka.
Sasa unataka kusema entropy na the second law of thermodynamics ndiyo mungu?
Hivi mwili wa binadamu mfano kwenye tumbo, Ini, Figo, Bandama, Moyo, Mapafu, vimejitengeza venyewe, au vimezuka,
Hata nikisema sijui jibu la swali hili, hilo halina maana jibu lake ni mungu.
Ukiniuliza square root ya mbili ni nini? Nikasema sijui, hilo halina maana jibu lake ni nane. Why should it be nane, show me how.
Kwa nini binadamu awe kaumbwa na mungu? Nioneshe.
Kama unasema complexity ni lazima iwe na muumba, ultimately kwa principle hiyo hiyo itabidi mungu naye awe na muumba, na muumba wake awe na muumba, ad infinitum.
lakini anakubali injini, computer, imetengenezwa na binadamu.
Cha kushangaza hapa ni wewe unayekubali kwamba complexity ndogo kama injini inatengenezwa na binadamu, lakini complexity kubwa kama mungu haitengenezwi.
Ni kama kukubali kwamba mkokoteni ni lazima utengenezwe na binadamu, hauwezi kutokea wenyewe, lakini Jumbo Jet linaweza kujitengeneza lenyewe tu.
Kama binadamu (low complexity) ni lazima awe ameumbwa na mungu, na complexity ni alama ya intelligent design, then mungu (high complexity) naye ni lazima awe ameumbwa, na muumba wake lazima awe ameumbwa.
This god falls on his face.
Tatizo binadamu wanataka kufikiri mpaka nje ya uwezo wao.
Wakiweza kufikiri maana yake hapo si nje ya uwezo wao, by definition binadamu hawezi kufikiri nje ya uwezo wake.
Usiogope kufikiri kwa kuogopa kufikiri nje ya uwezo wako.Utakuwa kama mtu anayeogopa kutembea kwa kuogopa kufika mwisho wa dunia na kudondoka.