Kuna siku nilikuwa ninapitia posts humu JF nikakuta umemwambia mtu akatafute kitabu kinachoitwa "The Lost Books of the Bible", nilikitafuta na kukisoma na nikagundua ni ukweli usiopingika kwamba biblia tunayoisoma "imechezewa" kwa makusudi kwa sababu wanazozijua hao walioichezea biblia.
Katika kusoma kwangu kile kitabu "The Lost Books of the Bible" nikagundua kwamba mwandishi anayakubali yale maneno yaliyoandikwa kwenye biblia ila anacholalamikia yeye ni kwa baadhi ya watu wa kanisa wa kipindi hicho kuamua ni kipi kiwepo na kipi kisiwepo kwenye biblia kwa sababu walizozijua wao wenyewe.
Mimi ilifikia kipindi nilikuwa ninajiuliza kama yale yaliyoandikwa kwenye biblia yaliandikwa na manabii kweli au ni usanii ila baada ya kuona mwandishi amekubali yale maneno ya kwenye biblia yaliandikwa na manabii/mitume na ni genuine (kitu ambacho kilinipa moyo kusadiki kwamba Mungu yupo) basi mwandishi anasadiki kwamba Mungu yupo.
Unaonaje hili swala la mwandishi wa hiko kitabu kuona kwamba maandiko ya biblia ni genuine na tatizo la mwandishi lipo kwenye uchakachuaji wa biblia tu? Huoni kwamba mwandishi kuyaamini kwake maandiko ya biblia kunaonyesha kwamba Mungu yupo?
Uliorodhesha vitabu zaidi ya hiki na hivyo vingine nilivipitia japo ni juu-juu lakini sikuona hata kimoja kikisema kwamba maandiko ya biblia ni mambo ya kutungwa. Vitabu vyote vimekubali biblia ni genuine.
Hauoni kwamba uGenuine wa maandiko ya biblia unadhihirisha uwepo wa Mungu?
Nashukuru kwa kupitia kile kitabu. Kwanza kabisa kile kitabu ni basic sana na cha zamani sana, version yangu ilikuwa first printed ni ya 1926.
Process ya kupata realization si ya kuipata kwenye kitabu kimoja. Ni ya ngazi kwa ngazi, layer kwa layer kama layers za kitunguu kimoja kikubwa.
Layer ya kwanza ni hiyo ya kujua kwamba biblia hii ya sasa inayotumiwa na wengi imekuwa edited na watu, chiefly Constantine na maaskofu wake katika "Council of Nicea". Wakaamua nini kibaki na nini kiondoke, mara nyingine kwa sababu za kisiasa ili kuendeleza nguvu za utawala wa Roma.
Muandishi kukubali kwamba vitabu vimeandikwa na manabii ni layer nyingine. Kwa sababu nabii ni nani? Nabii si mtu? Sasa hawa watu si Wayahudi? Kama walikuwa na political reasons za kutaka kufanya world domination kwa nini wasitumie dini? Kwa nini wasiseme kwamba wana wa Israel ni taifa teule la mungu? Dini imetumiwa kama sehemu ya siasa iliyopewa utakatifu tu.
Ukizama zaidi katika historia ya dini utaona jinsi gani watu walivyotumia dini kutaka kuleta order kwanza. Bila ya woga wa mungu watu wangeuana sana kwa hiyo wazee ikabidi waanze kutisha watu kwa kuhadithia mizimu na mungu.
Ilipoonekana kuwa hili linawezekana, na watu kwa ujinga wa kutoelewa nature (radi, kupatwa kwa jua etc) waliogopa mungu, wazee hawa wakakaa na kuorganize dini, amri kumi za mungu na makanisa, wakateua wafalme waliobarikiwa na mungu, wafalme wakawa wana protect dini na dini ina protect wafalme. Ukiangalia Babeli,China, Misri, Wayahudi hadithi ni hiyo hiyo.
Mpaka George W. Bush kapigana vita ya Iraq kwa kutumia support kubwa ya the evangelicals.Alivyoanza actually aliiita "Crusade".
Kwa hiyo ukizama sana, ukisoma the canonical arguments for the existence of god.Utaona kwamba wanaosema mungu yupo hawana hoja, na wanaosema hakuna uthibitisho kwamba mungu yupo maswali yao hayajibiki.
Hata hapa JF tu maswali yangu kibao hayajibiki.
Habari za dini na mungu ziliweza kuwachota watu enzi za ujinga, za kuambiwa "fanya" ukafanya bila uchunguzi wala uthibitisho.
Hizi enzi zetu za uthibitisho na habari, mungu kaanguka.
Kwa sababu watu washasema sana kwamba radi ni sauti ya mungu anapokasirika. Wanasayansi wakachunguza wakaielewa radi kisayansi bila kuhitaji "the god hypothesis". So on and so forth.
Kila tunavyozidisha maarifa ya kisayansi, ndivyo tunavyozidi kuona hizi habari za mungu ni kamba tu.
Na hata ile argument ya kusema mungu anahitajika kama "boogey man" ili kuwa keep watu in line inakosa nguvu, kwa sababu kuna ma Buddhist huko hawaamini mungu lakini wana a higher moral standard kuliko hata wanaoamini mungu wengine.