GE2025 Musiba: Kama kuna mtu yeyote nilimkosea, naomba anisamehe. Ule ulikuwa ni ujana

GE2025 Musiba: Kama kuna mtu yeyote nilimkosea, naomba anisamehe. Ule ulikuwa ni ujana

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
889
Reaction score
2,863
Wakuu,

Inaonekana kama Musiba baada ya kukatwa na CCM akili zimeanza kumrudi.

Leo akiwa anaongea na waandishi wa habari ameomba radhi watu wote ambao aliwakosea kipindi hicho na akaongeza kuwa kipindi kile alikuwa kijana tu.

Nadhani msamaha huu unawahusu sana wakina Fatma Karume na wengineo ambao walichafuliwa sana na huyu baba kipindi cha mwendazake




View: https://www.youtube.com/watch?v=FEkeO7yPjdc

Mwanaharakati huru Cyprian Musiba amechutama na kuwaomba radhi wote aliowakosea na kuwafanyia mabaya siku za nyuma akidai kuwa yote aliyoyafanya ulikuwa ni ujana huku akiwasisitiza waafrika kutokuwa na visasi na kuacha kuweka vitu moyoni.

"Watu wananisema eti wewe ulikuwa unawaombea wenzako mabaya. Inawezekana nilikuwa kijana sana. Sasa hivi nimekuwa mtu mzima - akili zinakua, unabadilika, unakuwa na busara. Unajua kadri unavyozidi kukua, ndivyo unavyopata hekima, busara na utu. Wakati mwingine ujana sio mchezo.

"Kwahiyo waafrika tuna tatizo la visasi na sijui tutaacha lini, visasi sio vizuri, visasi pia vinasababisha nchi haiendi mbele inarudi nyuma tu, sasa msipende kuweka kitu moyoni, ni kitu kibaya sana kwasababu nchi hii ni yetu sote, mtu akikukosea kasirika hapo hapo mmalizane tu msameheane maisha yaendelee," amesema Cyprian Musiba.
 
Nanukuu kauli ya musiba "Nimekubali yaishe nimeamua kurudi kijijini" baada ya Muda Mzee wa niguse ninuke akaaga dunia..😀


Mimi nilikusamehe tangu mzee wa niguse ninuke alipofariki..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom