Mwenyekiti wa State Oil (T) Ltd Nilesh Suchak kupitia kampuni ya Uwakili ya Prime Attorneys amemtumia barua Mkurugenzi Mtendaji wa Jamvi la Habari Habib Mchange akimtaka kuomba radhi na kufuta mara moja kauli za kashfa zilizochapishwa na kurushwa kupitia vyombo mbalimbali vya Habari na Mitandao...
Asiyejua alikotoka, hakika hawezi jua anakoenda!
Moja ya urithi ambao awamu ya tano ilituachia ni somo la hatma ya aliyekuwa akijitambulisha kuwa mwanaharakati binafsi wa Rais Magufuli, ndugu Musiba.
Nani hakumjua Musiba enzi za JPM? Musiba kwa matendo na maneno yake, ni kama alikuwa ndiye...
Ninakumbuka Musiba aliwahi kusema baada ya Lissu na Hche kuchaguliwa na Mkutano mkuu wa Chadema kuwa CCM wajiandae na siasa ngumu kutokana na haiba ya hawa watu.
Ni kweli tumeyaona utabili wake ulikuwa sahihi. wacha tuone
Mwanaharakati na Mwanasiasa Cyprian Majura Musiba, ametangaza rasmi kurejea katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia Januari Mosi, 2026, akisema amefanya uamuzi huo kwa hiari yake bila kushawishiwa na mtu yeyote.
Katika barua ambayo imenaswa na Royal TV ikionesha uamuzi huo tangu mapema Januari...
Nimekutana na hii taarifa ya maamuzi ya rufaa ya kesi ya Bernard Membe dhidi ya Cyprian Musiba.
Kwanza ikumbukwe kesi ilipokuwa inasikilizwa Mahakama Kuu, upande wa washitakiwa, yaani upande wa Musiba, hawakutokea Mahakamani kwa hiyo kesi ilisikilizwa upande mmoja na mdai yaani Membe kupewa...
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mwibara kupitia ACT Wazalendo Cyprian Musiba ameahidi kuzilinda kura zote atakazopigiwa na wananchi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Musiba amesema hayo Agosti 31, 2025 akizungumza na waandishi wa habari wilayani Bunda akiwaomba wananchi kumpigia kura kwa wingi na...
Kwa wafuatiliaji wa siasa Polepole si mzalendo wala hawezi kuwa mwanaharakati.
Anayosema leo yameanza leo? Kutekwa watu, kupotezwa ndio mara ya kwanza?
Mbona kipindi cha Magufuli hakuongea haya? Eti Musiba Junior nae anaungana nae kweli?!! Mbona Watanzania tunakuwa watu wa kujisahau sana...
Wakuu,
Inaonekana kama Musiba baada ya kukatwa na CCM akili zimeanza kumrudi.
Leo akiwa anaongea na waandishi wa habari ameomba radhi watu wote ambao aliwakosea kipindi hicho na akaongeza kuwa kipindi kile alikuwa kijana tu.
Nadhani msamaha huu unawahusu sana wakina Fatma Karume na wengineo...
Akizungumza na wanahabari Julai 31, 2025 Kada wa Chama cha Mapinduzi Cyprian Musiba ameeleza kuwa mchakato wa kuchagua watia nia ubunge unafanywa hasa kwa kujuana ndani ya chama hicho akidai ili uchaguliwe ni lazima uwe unajuana na mtu au uwe mtoto wa waziri ndipo uchaguliwe
Pia amehusia baadhi...
Mwnaharakati machachari na mzalendo wa Chama cha Mapinduzi, aliyependa na kupendwa sana na hayati Magufuli Cyprian Musiba amesema hajaelewa sababu walizotumia viongozi wa chama kukata jina lake pamoja na majina ya watu wengine
Musiba amesema yeye amechukua fomu kwa mara ya nne mwaka huu na...
Cyprian Musiba akipata kuwa mshirika mkubwa wa propaganda za Magufuli akimiliki vyombo vya habari kama vile magazeti vilivyokuwa vikimpigia debe Magufuli.
Leo Musiba amegeuka kuwa mwiba kwa serkali ya CCM. Asema CCM wanategemea wasanii lakini hata hivyo watu wanawapuuzia na kufuatilia mambo ya...
Mwanaharakati huru Cyprian Musiba amedai kuwa viongozi wengi wa vyama vya upinzani nchini si wa kweli na wanatumia nafasi zao kama chanzo cha kipato badala ya kutetea maslahi ya wananchi.
Akizungumza wakati wa mahojiano na Jambo TV, Musiba amesema vyama vya upinzani vimegeuka kuwa ajira kwa...
Mwanaharakati huru Cyprian Musiba akitoa maoni yake kuhusiana na uchaguzi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
"Freeman Mbowe sio tough (mgumu) vile, sababu Mbowe mnaweza mkazungumza, Wenje mnaweza mkazungumza na mambo yakaenda na mkapeleka nchi yenu mbele."
"Lakini wale jamaa...
Kuna mabadiliko kidogo ya kiuongozi yatafanyika hivi Karibuni.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kuwa Sabaya na Musiba kuwa mkuu wa Mkoa wa Mara huku Paul Makonda akitazamiwa kuwa katibu mkuu mpya CCM, na Polepole Humphrey atakuwa Waziri wa Tamisemi.
Dr Bashiru Ally kuwa waziri wa Mambo ya ndani na...
Mwanaharakati huru kama anavyojiita, Cyprian Musiba amesema kama mtanzania ameumia sana na matukio ya utekaji na kupotezwa kwa watu hususan tukio la hivi karibuni la kuuawa kwa Ali Mohammed Kibao. Hata hivyo, amesema kama mtanzania anapinga kutumia matukio kama haya kuanza kushambulia watu...
Musiba aliowatuhumu woote kwamba wanamhujumu Magufuli kwa kutaka kumpindua Magufuli na serikali yake alitwezwa na kubagazwa Sana lkn list yote aliyoitaja sasa iko nje ya Mfumo
January Makamba
Benard Membe (marehemu)
Nape Nnauye
Dulaa kinana
hongera Sana Musiba yametikis
January
Sio masikhara kuhusu hili swali. Inawezekana mwanaharakati huru Cprin Musiba ni mtu anayehusudiwa (role model) na vijana wa chama cha Mbowe (CCM B). Kwanini natamka hivi? Kwanza ikumbukwe mwanaharakati huru alikuwa akitukana yeyote aliyehisi ni kikwazo kwenye utawala wa awamu ya 5. Tumeona...
Kama mada ilivyo hapo juu kwa kuwa inadaiwa kuna 4R (Reconciliation, Resilience, Reforms and Rebuilding)
kwamba zinatibu vidonda vya kuumizwa kiakili, kimwili, kiuchumi na kijamii basi nafasi hiyo ifunguliwe kwa mwandishi mkongwe Cyprian Musiba ili kuchangamsha zaidi myambuliko wa siasa za...
Katika hali ya kushangaza kumetoka aidha mgomo au chama kimekosa Mvuto kabisa.
Wengine wanadai aaah wapi sio kukosa mvuto bali chama hakitoi maokoto kama zamani hivyo watu wanaovutwa na mafumba wamekikacha.
Enzi za huko nyuma tulishuhudia social media zilizobamba kwenye anga la Tanzania...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.