Muonekano wa moja ya ndege mpya za Air Tanzania

Waswahili hamnaga jema. Mnataka kukimbia kabla ya kutambaa. Huwezi anzia kununua Marcopollo bila kuanza na Hiace. Hutaweza kumanage. Ndiyo maana mnakopa mitaji mikubwa bank mnaitumia vibaya wanawakaba hadi viti vya majumbani kwenu. Ridhika na uliichonacho.
tulikuwa nazo tayari boeing 737 sio tunaanza na haya mapangaboi, kweli tanzania kila kitu kina rud i nyuma miaka 50
 
Za Rwanda ni Nzuri zaidi nitapanda za Jirani yetu... Ningeshangaa Jirani amshauri jamaa anunue Ndege nzuri kama zake ili ampiku la hasha kamuambia mkuu nunua mapanga boi ili tusifanane aliyekutangulia kakutangulia tu.... Miaka hii bado Ndege za Mapanga boi????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????/ ai kanti belivu ma ayis

Za Rwanda ni Nzuri zaidi nitapanda za Jirani yetu... Ningeshangaa Jirani amshauri jamaa anunue Ndege nzuri kama zake ili ampiku la hasha kamuambia mkuu nunua mapanga boi ili tusifanane aliyekutangulia kakutangulia tu.... Miaka hii bado Ndege za Mapanga boi????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????/ ai kanti belivu ma ayis
Mlaleo wacha upotoshaji...huyo jirani ana Turboprops kadhaa,alianza nazo hizo na baada ya biashara kuchanganya akanunua CRJ-900 ambazo ni Jet engines,baadae akanunua Boeing tatu,moja ni B733,B737 na B738....Na sasa ameenda mbali kanunua Airbus mbili ambazo ni A333-200 ameeita "Ubumwe"....Waha na Waangaza wanajuwa nini maana yake.
Kama huna data usijadili jambo

image.jpeg
image.jpeg
 
tulikuwa nazo tayari boeing 737 sio tunaanza na haya mapangaboi, kweli tanzania kila kitu kina rud i nyuma miaka 50
Je sasa tunayo hela ya kununua hizo Boeing ?
Tulisharudi nyuma miaka 100 kwani hatukuwa na ndege ,tumenunua hizo ndio tunaanza safari upya
 
Jamani tusiidiss sana serikali yetu kwa baadhi ya jitihada inazozifanya nimejaribu kugoogle kwenye wikipidea we andika tu hiyo brand ya ndege bomberdier Q400 taarifa zake zote zinakuja za hiyo kampuni iliyotengeneza ndege na imeweka mpaka siku serikali yetu iliweka order Canada na jamaa wameelezea series ya ndege yetu kwani mojawapo ya wateja wake WA kipindi cha karibuni hata ETHIOPIAN AIRLINES ni wateja WA hiyo kampuni kwa baadhi ya flight zao so kwa ufupi ni kuwa ni mwanzo mzuri na ndege sio mbaya na wala sio ndogo kivile nadhani ni ya abiria kama 70.
 
TTCL
Hii haikufa bali tatizo kubwa lilikiwa poor management+poor business strategy +poor customer care (Mfano TTCL walikuwa hawafanyi kazi weekend imagine service wanazotoa ilikuwa tatizo likitokea weekend inabidi usubiri hadi Jumatatu) .Licha ya kuwa na coverage karibia nchi nzima walizidiwa na private company (Tigo,Vodacom,Airtel,Zantel) pia wangeweza kutarget project nyingi za serikali ni aibu ISP wa mashirika mengi ya serikali ni kampuni binafsi

ATCL
Kwanza hii ni biashara ngumu sana kwa nchi maskini kama yetu sababu ya uchumi mdogo(domestic route) ni wachache wanaoweza kupanda ndege na international route ni ngumu sana kushindana na competitors toka Uarabuni,ni biashara ambayo ukikosea kidogo ku-recover unahitaji support kubwa zaidi

Makampuni ya serikali yalikuwa hayaendeshwi kufuata ushauri wa wataalamu (unanunua/unakodi ndege mbovu ambazo gharama zake za uendeshaji wake ni mkubwa kuliko.Kuna fitina zilifanywa na management ikasababisha ATC ife na PW ikapewa deal zote

So TTCL now wamebadilisha baadhi ya vitu tayari na capital wanayohitaji ni ndogo ukilinganisha na wanayohitaji ATCL (hawa ingewezekana shirika livunjwe waanze upya +ndege mpya).Ingawa investment ya TTCL ingesaidia sana maendeleo ya nchi na impact yake ingeonekana mapema kuliko ya ATCL but kuchelewa kufufua ATCL ilikuwa ni advantage kwa competitor wetu hasa Kenya kabla ya Fastjet PW ndio walikuwa wametawala route za TZ na KQ wanamiliki PW hisa 40%.2012 Fastjet walipoanza operation walinyimwa kibali kuoperate Kenya wamepewa mwaka huu baada ya JPM kuingia madarakani
Nashukuru sana kiongozi na nimekuelewa vizuri sana,nadhan tatizo kubwa ni kwamba haya mashirika yamekuwa yakijiendesha kwa hasara lkn yana uwezo wa kujiendesha kwa faida,lkn shirika ambalo impact yake ingeonekana mapema zaid kama serekali ingeamua kutilia mkazo kati ya ttcl na atcl,nadhan ni ttcl kama ulivyoeleza hapo juu
 
Terms and conditions hizo za ajira ya mkataba.. sijui kabisa kama watapata marubani au engineers, hawatawapata, i bit, umwajiri kwa contract mwaka mmoja au mitatu, kisha huko mbeleni hana uhakika wa kurenew contract, hapo watapata cabin crew tu, pilots and engineers wasahau, i can see that, huwezi mpa engineer mkataba wa mwaka mmoja, alafu mwakani akikosa mkataba..!? Sbb wengi sasa hv wameajiriwa labda Fastjet, Precision, Coastal, Tropical, Safari plus, etc, sasa mtu professional aache kazi huko aje umpe mkataba wa mwaka mmoja au 5 na ATCL ndio kama inafufuka vile, hapo hawatawapata, nawajua..
halafu na mishahara mpaka muandamane
 
image.jpeg
image.jpeg
WEwe unajua maana YA jet engine kweli? Kwani ile ndege YA rais haijawahi kutua Mwanza znz Nk? Acha kudandia vitu usivyojua. Hujui zile ndege zao walizoua mwanzo zilikuwa jet engine?
Unajadiliana na maamuma.....anafikiri ukisema Jet engines basi ndio ile midege ambayo utotoni tulikuwa tunasema inatuwa Misri na S.Afrika tu.Hajui hata Fast Jet ndege zao zote ni za "Jet Engines"...Katika ndege tatu z Raisi...Mbili ni za Jet engines!!ambazo moja ile Fokker inatuwa mpaka uwanja wa Iringa.
Tazama kwa mifano...Hiyo ndege ndogo ya mzungu wa Iringa anaitwa Fox ni "Private Jet" inabeba watu watano tu na ni jet,wakati hiyo kubwa ya Rais na inabeba watu zaidi ya 20 si Jet na ni turboprop....Anashangaa Jet itatuwa kiwanja gani cha mkoa?Sasa mbona hiyo Jet hapo ni uwanja wa Mkoani??Hana elimu ya mambo ya aviation anajadili tu kishabiki.
 
View attachment 386629 View attachment 386630
Unajadiliana na maamuma.....anafikiri ukisema Jet engines basi ndio ile midege ambayo utotoni tulikuwa tunasema inatuwa Misri na S.Afrika tu.Hajui hata Fast Jet ndege zao zote ni za "Jet Engines"...Katika ndege tatu z Raisi...Mbili ni za Jet engines!!ambazo moja ile Fokker inatuwa mpaka uwanja wa Iringa.
Tazama kwa mifano...Hiyo ndege ndogo ya mzungu wa Iringa anaitwa Fox ni "Private Jet" inabeba watu watano tu na ni jet,wakati hiyo kubwa ya Rais na inabeba watu zaidi ya 20 si Jet na ni turboprop....Anashangaa Jet itatuwa kiwanja gani cha mkoa?Sasa mbona hiyo Jet hapo ni uwanja wa Mkoani??Hana elimu ya mambo ya aviation anajadili tu kishabiki.
Hii ndo Tz inayohitajika au cio ndg zang
 
Nashukuru sana kiongozi na nimekuelewa vizuri sana,nadhan tatizo kubwa ni kwamba haya mashirika yamekuwa yakijiendesha kwa hasara lkn yana uwezo wa kujiendesha kwa faida,lkn shirika ambalo impact yake ingeonekana mapema zaid kama serekali ingeamua kutilia mkazo kati ya ttcl na atcl,nadhan ni ttcl kama ulivyoeleza hapo juu
Biashara ya Airline ni ngumu mno kwa Africa only Ethiopian ndio wameweza.Kushindana na waarabu wenye mafuta (Oman Air,Emirates,Etihad,Qatar,Turkish ,Fly Dubai) ni kazi nzito sana hata wazungu wanapata tabu
 
image.jpeg
Huo ni uongo
Hiyo ndege inayoonekana hapo ni caravan
Ni hujuma tu za watu wachache wanaotaka kuchafua jitihada za Rais
Hivi kwanini mnapenda kupotosha?Mnafikiri humu JF watu wote ni wajinga wajinga?Unaijuwa Caravan wewe au unaisikia?Umewahi kuona Caravan yenye double Turboprop?....Caravan ni single engine!!Kama hiyo ya ATCL unaiita Caravan....Hii hapa utaiiitaje?Wacha kupotosha wewe alaaaa
 
Biashara ya Airline ni ngumu mno kwa Africa only Ethiopian ndio wameweza.Kushindana na waarabu wenye mafuta (Oman Air,Emirates,Etihad,Qatar,Turkish ,Fly Dubai) ni kazi nzito sana hata wazungu wanapata tabu
Kweli kiongozi ni bora tungeanza na ttcl kuliko kuanza kuingia magharama ya kununua mandege ambayo nadhan bado tutashindwa kutengeneza faida kama ambavyo tungekazia kwenye ttcl
 
wenzetu kenya walinunua dreamliner 380 ndege 6 bila kelele wala matangazo kama sisi ,vindege vyenyewe na mapanga boi kama za enzi ya hitler ww2,mshamba akiona jua ndio utajua sauti yake
Kiongozi, fafanua hapo, Dreamliner 380 zinatengenezwa na kampuni gani? Wa Tanzania tupo vizuri kuongea hakyanani...!!
 
Aibu utafikiri TPY
mbona ndege imeumbwa km likatuni
hata Rwanda wanatushinda!!!!!!!!!11
Hivi we Ukwaju mbona mnakuwa waongo sana?Rwanda wanatuahinda kwa lipi wakati na wao wana Dash8-Q400 na ndio inakuja Dsm mara kwa mara toka Kigali?
Umewahi kusafiri na ndege ya Ethiopia ya usiku toka Bole kuja Dsm wakati wa Low-Season?Wao pia huleta Dash8.Na kwa Ethiopia hizi Dash8 ndio zinatumika kutoa abiria mikoani kuleta Addis Ababa kwa ajili ya connection....Eti likatuni??Hizi ni Canadian Turboprop ndugu....Usidharau mambo usiyoyajuwa
Kama hujui vitu kaa kimya,sio lazima uchangie ili uonekane na wewe umechangia
image.jpeg
image.jpeg
 
image.jpeg

Kiongozi, fafanua hapo, Dreamliner 380 zinatengenezwa na kampuni gani? Wa Tanzania tupo vizuri kuongea hakyanani...!!
Yaani nimeufuatilia huu uzi mwanzo mwenga!!Watu hawajui kabisa mambo ya ndege lakin wanaropoka ropika kweli.Ona huyo nae eti anasema "Dreamliner 380".... Hakuna kitu kama hicho!!Dreamliner ni BOEING 787 ambayo kwa Afrika wa kwanza kununa alikuwa ni Ethiopian Airways...Na moja akaipa jina la "Abebe Bikila" yule mwanariadha maarufu wa Ethipia miaka ya 50 to 60 na moja akaiita "QUUEN OF SHEBA" kwa heshima ya Mke wa Suleiman ambao ni uzao wa Mfalme Suleiman Ethiopia!!Sasa huyu Dreamliner 380 kaijambia wapi mkuu Eli79 ?.....Watu vil..aza halafu wanajidai wanajuwa mambo
 
Kweli kiongozi ni bora tungeanza na ttcl kuliko kuanza kuingia magharama ya kununua mandege ambayo nadhan bado tutashindwa kutengeneza faida kama ambavyo tungekazia kwenye ttcl
uploadfromtaptalk1471984296122.jpg

Angalia financial report ya RwandaAir for last 5 years.Ukienda Kenya Airways nao wako hoi
 
Uwanja wa mwanza una tofsuti gani na wa Mtwara au kigoma?
Kuna tofauti kubwa tu mkuu...Kwanza ni urefu wa Runway ya Mwanza si sawa na ile ya Kigoma na Mtwara.Pia "Maximum Take Off Weight" ya Runway wa Kigoma haiwezi kulinga na ile ya Mwanza.Ndio maana uwanja wa Kigoma mwisho ukubwa wa ndege aina ya ATR72 kutuwa,maana uzito zaidi ya hiyo runway inatitia...Wakati Mwanza MTOW ni mpaka A320 hadi Boeing767.
KIGOMA hakuna taa za runway na navigation instruments nyingine na ndio maana uwanja unafanya kazi "From Sun rise to Sun set" wakati ule wa Mwanza ni 24/7....Hizo ni sabab chache kuonyesha huo utofauti mkuu lusungo
 
Back
Top Bottom