BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Abiria 122 wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wamenusurika kifo wakiwa safarini baada ya ndege waliokuwa wamepanda kupata hitilafu kwenye moja ya injini zake.
Ilikuwa Jumamosi Februari 24, 2024, ndege ya ATCL Airbus A220-300 iliyoruka kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya iliponusurika kushika moto baada ya moja ya injini kupata hitilafu na kuanza kutoa moshi.
ATCL imesema tukio hilo limetokea dakika 25 baada ya ndege kuruka na kwamba, marubani na wahudumu walidhibiti hali hiyo na ndege kurejea na kutua salama jijini Dar es Salaam.
Abiria aliyekuwa ndani ya ndege hiyo aliyeomba jina lake lisitajwe, amesema baada ya kuruka umbali wa futi anazokadiria kuwa 12,000 walianza kuhisi harufu ya kitu kinachoungua.
MWANANCHI