Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

ushauri wa KISHETANI kabisa. unashauri kuua kiumbe kisichokuwa na hatia? muuaji mkubwa!
Who exactly do u think u are??? Acha kutokwa povu ovyo, hii ni open forum na kila mtu ana haki ya kutoa mawazo
 
Pole naona hadithi ya leah imekugusa sana...

Ni yangu matumaini hautasema shule kwanza
Hahaha me sitoenda shule, ila ntakaa mwaka bila kuzaa[emoji133] [emoji133] [emoji133] [emoji133] [emoji133]
 
Heaven Sent;
Were yu realy sent from heaven?? Acha hasira dada, sio miye nilikuumba ati. Dah! Hasira mpaka unasahau mantiki yangu? Sijasema na sintasema ati wanaume tumeruhusiwa kuchepuka. No, no, noo. Kuchepuka sio dili. Mke mmoja na mme mmoja ndiyo dili. Lakini, sivyo siku hizi. Wenyewe mmeshindwa wajibu wenyu.
Weye mama mpaka uchepuke na dereva wangu niliyemtuma aje akuchukue uende sokoni huoni una shida kubwa? Haya, umechepuka na huyo dereva wangu, kakupa mimba, inakaa tumboni mwa nani?? Jione kwanza kabla hujapiga yowe.
Hicho ki band chako atakilelea nani? Jamani, si haki hata kidogo. Raha zako ziwe karaha hata kwa familia mzima? Hata jumuia haita kuelewa
Hapo pa "mke mmoja, mume mmoja" nafikiri pamefunga mjadala wetu. Cheers....
 
Hahaha me sitoenda shule, ila ntakaa mwaka bila kuzaa[emoji133] [emoji133] [emoji133] [emoji133] [emoji133]

Hahahah....mwaka?!

wifi zako waswahili sana watavumilia miezi sita tuuu[emoji1]
 
Kutokana na maumivu ya haya mambo ya mahusiano, nilishaamua na kuomba Mungu anisaidie na kuniwezesha nisichepuke, sio tu kwa sababu kwa imani yangu ni dhambi, ila sitaki mie wangu apate maumivu ya kusalitiwa. Ni kitu kigumu na kibaya sana maishani
Ninasadifu hekima yako kiongozi. Ni kuomba Mungu ili atuonyeshe kwa nini tulikubali kuitwa waume kwa wake zetu, kuwaheshimu na kuwapenda ni pamoja na kujiheshimu mbele za kila mtu.
 
Some men are heartless. Hivi nyie mnaona mkichepuka ni haki kabisa, ila kwa wake zenu ni kosa lisilosameheka? Afu mnaona wake zenu wapumbavu sana, hawana mioyo, wana dhiki sana na ndoa kwamba mtaenda tu nje mlale na michepuko yenu, afu ikileta matunda (nimecheka kwa masikitiko), wanawake zenu wanaipokea happily, eti eeh? Huyo mtoto unayemleta mkeo akulelee ni damu ya mkeo hadi achekelee? Mnawaumiza sana wake zenu, kuendekeza kwenu uzinzi afu nyie mnaona kawaida tu, kuna mwanamke anayependa aletewe watoto wa nje?. Msiwatendee wake zenu msiyotaka kutendewa. Yani mmewafanya wake zenu kama nannies sijui. God is watching you guys lakini
Ndo nlicho muuliza km mkewe akipewa mimba na shemejiye (yan mdogo wake yeye mume) atakuwa tayar kuchukua huyo mtt maana ni mtt wa mdogo wake. Wajue wanawake wanaumia sn sana ni vile tu labda wanaona wabaki walee watoto wao lkn kikuubwa katika jamii yetu wanawake wengi uchumi mdogo na hata elimu ni ndogo lkn as days go by wanawake wanapata elimu na pia nguvu ya kiuchumi kwa hyo mwanaume akileta uzinzi wake wa waziwazi mwanamke anaweza kujisimamia na kuamua kile anaona kinafaa kwa maisha yake na si kukaa kwa mume km mtumwa. Wanaume mtashangaa sn coz wanawake wa kunyanyaswa wanaenda wanapungua.
 
Wanaume ni viumbe wa ajabu sana linapokuja swala la kufanya huu mchezo, akili yote inapotea na sijuagi ni kitu gani kinasababisha kwa kweli.

We fikiria tu wale wamama ambao ni vichaa wana watoto (wamewazaa huku wakiwa tayari ni vichaa), na waliowazalisha ni wanaume wenye akili timamu kabisa.

Hahaha broo hapo na mimi huwa nachoka sana

vichaa,wanafunzi,mama ntilie,wafanya usafi,baamedi,wazee,kahabaz,beki tatu watu wanakula tuuu WTF???!
 
ushauri gani wa kipumbaFU huu? unahalalisha mzinzi kuzaa na shemejiye? acha hizo mkuu.
Sihalalishi mkuu mana wamekosea,ila tufanyeje sasa kutoa mimba sio option nzuri mana ni mauaji,AZAE tu babaake alee,mana hakuna namnaa
 
Haya mambo huwa yanasumbua sana ila cha kufanya nafikiri ni bora ufuate ushauri wa wazazi, dogo aondoke wewe umsamehe mmeo maana hili tatizo liko karibu sana na wewe aliepata mimba ni mdogo wako na aliempa mimba ni mme wako wa ndoa, suluhisho sio kuikimbia ndoa maana hata ukiikimbia mdogo ako hata acha kuwa mdogo wako na akijifungua kila ukisikia kuhusu huyo mtoto itakukumbusha mmeo na mdogo ako, lakini ukiufungua moyo ukamsamehe maisha yako na mme wako yataendelea kama kawaida na mdogo wako ataendelea na yake atapata mtu mwingine atamuoa na ww utaendelea kuwa na mmeo itabaki tu mme wangu alinikosea akazini na mdogo wangu akapata mimba, hata hapo baadae unaweza kujikuta umempenda yule mtoto bila hata kujijua ila ukiwaacha utawachukia na utajilazimisha kuwasahau ilhali wako karibu na wewe sasa.

Pole yanaumiza lakini tumia busara tu samehe piga moyo konde,dogo arudi msamehe mme.
 
Pole Sana. Nimejikuta nalia kwa huzuni . Binafsi nakuombea Mungu akupe busara wakati huu mgumu.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Pagumu hapo. Pole. Kuna maswali ya kujiuliza..Je, wakiishi pamoja uko tayari kumuita huyo mumeo shemeji? Mumeo alijuta na kuomba msamaha kwa dhati? Hapo kuna tatizo kubwa sana kwenye mahusiano wewe na mdogo wako. Chuki yako haitakwisha kwake akiendelea kuishi na Mumeo na ndo aibu itaendelea milele.
Ushauri mumeo akijirudi itakua nafuu na mdogo wako angeondoka angeolewa baadae na mtu mwingine ungepata nafuu kidogo ya chuki. Kwa sasa hata ukija pata mtu mwingine baadae wa kukuoa akisikia hii story anaweza kubadili mawazo.
Ukiweza kapatane na mumeo.
Hawa watu, mme mdogo mtu na data wataishi maisha ya shida sana. Namna nzuri ni kuanza maisha yako kivyako . Ndugu mtakutana kwenye sherehe na msiba
 
Hahahah....mwaka?!

wifi zako waswahili sana watavumilia miezi sita tuuu[emoji1]
Aah uzuri mimi mwenyewe ni mswahili wa unyakyusani, si Nakubaliana na hubby jamani[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
How old are you?
Partly kabla ya kuanza kumlaumu mumeo nitakulaumu na wewe.
  1. Kutokuufwatilia kwa karibu uhusiano kati ya mdogo wako na shemeji yake. Mbali na kuwa ni ndugu yako wa damu,utakuwa unajua tabia zake na ni mwanamke kama wanawake wengine.
  2. Hilo la kuchelewa kumzalia mumeo mtoto. Inaweza kuwa lilikuwa jambo lako tuu na namna alivyokubali inaweza kuwa kutokana na sababu zako ila je? mliridhiana pasipo shaka kwamba atakubali wewe umalize kusoma ndio umzalie mtoto?
Wanaume ni wadhaifu being a man I know this, na wanahitaji kufuatiliwa kwa ukaribu sana hasa kwenye mambo kama haya yanayohusisha hisia. Ki mtazamo sijui namna mambo unavyoyaendesha nyumbani kwako ni maoni yangu kuwa unaipa sana kazi yako na masomo as priority kuliko mume wako (sisemi usithamini kazi) to me, family comes first. Na hiyo weakness shetani ndio akapitia hapo hapo.

Bottom line: Fuata ushauri wa wazazi, dogo arudi kijijini ajifungue mtoto, mtoto akiwa mkubwa, aje hapo nyumbani, kaeni kikao cha kifamilia mdogo wako na mumeo waombe msamaha kwa jambo lililotokea na mzungumzie utaratibu wa matunzo ya mtoto. Life goes on. Ukishindwa hilo. File for a divorce ukaolewe na mtu atakayekusubiria umalize shule (tena Masters, unga na PHd kabisa) ndio ukubali kumzalia mtoto.
 
Dada leah hilo ni gumu,ila uamuzi utakochukua wa busara na unaonyesha ukomavu ni kumsamehe mme wako. Nakushauri kubali ushauri wa wazazi. pole sana. Chamsingi kuna mahali ukikosea kumwacha mme wako huru,hawa wanahtaji kuchungwa tamaa zao zko karbu tofauti na wanawake.
 
Nyie cheating inaumiza jamani. Na ni kazi sana mke kuanza upya after knowing kwamba mumewe anamcheat (na hapo ni mume kaomba msamaha). Kila mtu anaweza kutenda dhambi, lakini kufanya dhambi afu unaijustify tu, yani easy daaah. Anyway waache tu wafikiri bado tupo enzi za uwimbombo na ulindi
Ndo nlicho muuliza km mkewe akipewa mimba na shemejiye (yan mdogo wake yeye mume) atakuwa tayar kuchukua huyo mtt maana ni mtt wa mdogo wake. Wajue wanawake wanaumia sn sana ni vile tu labda wanaona wabaki walee watoto wao lkn kikuubwa katika jamii yetu wanawake wengi uchumi mdogo na hata elimu ni ndogo lkn as days go by wanawake wanapata elimu na pia nguvu ya kiuchumi kwa hyo mwanaume akileta uzinzi wake wa waziwazi mwanamke anaweza kujisimamia na kuamua kile anaona kinafaa kwa maisha yake na si kukaa kwa mume km mtumwa. Wanaume mtashangaa sn coz wanawake wa kunyanyaswa wanaenda wanapungua.
 
Ninasadifu hekima yako kiongozi. Ni kuomba Mungu ili atuonyeshe kwa nini tulikubali kuitwa waume kwa wake zetu, kuwaheshimu na kuwapenda ni pamoja na kujiheshimu mbele za kila mtu.

Ahsante kwa kuongezea maelezo mujarab mkuu, majaribu na vishawishi vipo na vitaendelea kuwepo. Ukishajua umeingia kwenye taasisi ya ndoa ni jukumu letu kama wanaume kuamua kukataa dhambi na mbaya zaidi kuwaumiza wake zetu kana kwamba tuna haki ya kuchepuka.

Mungu atusaidie katika hili, tunaishi kwenye kipindi ambacho watu wanaona kawaida ndoa kuvunjika, kutokua waaminifu kwa wenzi wao na kutokusimama kwenye nafasi zao. Si laumu lakini nimesikitishwa na baadhi ya michango inayotaka kuhalalisha uchepukaji wa wanaume kama jambo LA kawaida kwenye jamii.

Ubarikiwe mkuu.
 

Hongera sana kwa uamuzi wako wa busara. Wasamehe ili uendelee na maisha yako. Life is like a box of chokolate. You never know what you're gonna get!
 
Cha kwanza huyo mmeo hakurizika na penzi lako au maumbile yako ndo maana kaamua kuonja na kwa mdogo wako. Hivyo ikiwa kalala na mdogo wako hadi kumpa mimba hataishia hapo chakufanya achana nae mzinzi huyo nawe tafuta mme atakae kustiri na ukastirika
 
Back
Top Bottom