Muhingo Rweyemamu on Amina's Death

Muhingo Rweyemamu on Amina's Death

Bi.Senti 50,
Si heri Hospitali moja ingefanywa maalum kwa ajili ya viongozi? Ni jambo la aibu sana kwa nchi kuwa viongozi wetu wote wakiugua/kuzidiwa hupelekwa nje ya nchi! Kifo si kifo tu!
Sasa haya mabadiliko katika sector ya afya ni kwa walala hoi tu na sii kwa viongozi?
 
Nakubaliana kwa kiasi kikubwa na hoja za Muhingo, japo nami najiuliza kutokana na historia yake amapata guts gani za kutamka kwamba mwenyekiti wake wa chama na katibu wake ni 'wamekufa'ni hatua kubwa kwa kada kutamka hayo! ama ana uchungu wa kukosa 'ukuu wa wilaya' alioahidiwa!ama amejirudi baada ya maumivu mengi aliyowasababishia wengine! Inashangaza pia kama alikuwa anawajua waliokuwa wakimtumia kijana wetu mpambanaji kama chambo cha mapambano dhidi ya madawa ya kulevya na kuamua kukaa kimya!Yawezekana na yeye ni muuaji pia! Tuache hayo!

Kifo cha kijana wetu kinatuachia maswali mengi yasiyokuwa na majibu! Mimi ni mmoja wa watu ambao nilikuwa nafuatilia hali ya amina,kujaribu kutafuta suluhu toka mapema, bila mafanikio!Nakumbuka mara ya mwisho kuzungumza na simu na amina ilikuwa na usiku ambao hakutokea kuzungumza na wanahabari. Lengo likiwa ni kufahamu kulikoni hasa ukuzingatia nilimshauri tokea mapema mara baada ya majira kutoa habari juu ya talaka yake kukaa kimya, nikijua kwamba akiongea tu waandishi watakuwa wamepata kwa kutokea! Mazungimzo yetu yalinipa picha kwamba kijana wetu hakuwa vizuri! kwa ufupi alikuwa haeleweki anaongea nini kabisa! Kitu alichonijibu ambayo ilikuwa ni kauli yake ya mwisho kwani baada ya hapo simu yake ikawa haipatikani tena ni kwamba 'amewasiliana na ubalozi wa marekani, na ubalozi husika umemwambia kwamba watarusha live toka kwao kile ambacho ilikuwa akakieleze maelezo'Nilishtuka! Siku mbili baadae baada ya kutokumpata kabisa kwenye simu nilifunga safari mpaka kwao, lengo likiwa ni kumjulia hali na kutaka kusaidia..hatukuruhusiwa kuingia ndani,tukaambiwa amina hayupo- nilijua nadanganywa,nikawa sina jinsi! Ikanilazimu nitafute namba ya mdogo wake , nikawa namshauri wampeleke hospitali! Nakumbuka nilikuwa namwambia mara kwa mara mkicheza amina atakufa!Ilifikia hatua nikawatafutia daktari wa mambo ya depression na psycholigy!hawakuhangaika nae kabisa, walikuwa busy na waganga wakiamini kabisa binti yao amelogwa! Kibaya zaidi wale mabinti wadogo hawakuwa na sauti kwao! Mpakanjia alikuwa na sauti!

Amina amekuja kupelekwa hospitali akiwa kwenye koma, mwili wake ukiwa umebadilika rangi kabisa!Nilifanikiwa kuongea na Mhe. mmoja ambaye yasemekana alikuwa mshauri wake wa karibu, aliniambia alipotea kitanda na kumpita amina! alikuwa mweusi Tii! sio rangi yake, kumbe cell zinazorutubusha ngozi ya bindamu zilikuwa zimeshakufa! Kwa kweli inasikitisha sana!

Jambo ambalo nakuwa nimejiuliza kwa kipindi kirefu!Hali ya Amina ilikuwa inajulikana fika na serikali, kwa nini wazazi wake hawakulazimishwa wampeleke hospitali? Tunajua kabisa Mzee Chifupa ni kada wa chama, chama kingetoa amri lazima angetii, kwa nini chama kiliamua kukaa kimya? Je waliamua kumtoa kafara sababu tu watu aliokuwa akiwazungumzia ndio wanaoongoza kwa kukichangia chama katika kampeni za uchaguzi? au kwa kuwa na baadhi yao wao wanauza? Ni mara ngapi tumekuwa tukishuudia viongozi wenye mafua wakienda tibiwa nje ya nchi? Yaani Amina walikuwa hawajui? Na hawa wabunge wa CCM na manaibu mawaziri(UVCCM) ambao walipeleka umbea kwa mpakanjia (baadhi yao ilikuwa inasemekana walikuwa na uhusiano na amina)kulikopelekea msongo wa mawazo hata kufa kwa amina wamechukuliwa hatua gani?

mimi daima huamini malipo ni hapa hapa duniani! Najua mtanikebehi!anayeua kwa upanga , naye atakufa kwa upanga!
Amina ametangulia, sote tutamfuata!

Muhingo, 2010 endelea kuwa mtakatifu, utakatifu ambao umeanza kuuonyesha kwa Amina!

Dooh, hilo la kubadilika rangi ya mwili sababu ya skin cells linanishughulisha sasa... inaashiria alipatwa na main internal Organ failures?!, figo ndio linachuja sumu zote mwilini.. mpaka figo kuathirika vibaya namna hiyo scientifically inaweza kusababishwa na diabetes peke yake kwa muda mfupi namna hiyo, au?
 
Kwa mara ya kwanza nimeamua kuchangia mjadala wa JF. Mimi sina elimu sana kama wengi wenu hapa. Mimi hukubali hoja ambayo ina back ups (ninapenda kuona evidence).

Hizo picha zote za CMB hazina tarehe na muda wa lini zilipigwa. Yeye ndio ametuandikia tarehe na muda, siamini kama hizo tarehe ni hakika mpaka pale nitakapoona picha yenye tarehe na muda sio kwa CMB kutuandikia mwenyewe muda na tarehe. Tafadhali usitumie adobe kuweka tarehe na muda kwa sababu wengi hapa watakuumbua ukifanya hivyo.

Kwa sasa bado nampa Mkandara the benefit of the doubt.

Mwafrika,

Hizo picha kutoka kwa CMB ni official maana yeye ni afisa wa Ikulu na ni kwa matukio rasmi amabyo public lazima ijue. Kwa hiyo nami naungana nawe kuhusu mjadala wa Mugongo na Mkandara. Ni kuwa Mugongo na CMB wako kwa interest za kuprotect statehouse ingawa bado hawakuwa na sababu ya kukanunsha kwa nguvu zote madai ya Mkandara.

CMB na Mugongo walitakiwa wakae kimpya tu ili kivuli cha Mkandara na madai yake vipite unnoticed lakini jiulize. KWA NINI WAMEKIMBILIA KUKANUSHA? Wakati huohuo CMB kutoa na picha kabisa? Basi ujue kuna jambo wanaliigania
 
Hii hapa chini ndiyo post ambayo ulimsahihisha Chinga kwamba sio Balile anayemsaidia Mbowe, bali ni Ngurumo. You seem to be an A-type personality.....ila mimi bado hujanisadikisha kwa lolote.

Mzee Mwanakijiji

I quite don't understand why a member of JF should have to go through your radio to respond to his fellow members.

Chinga,

Umekosea kidogo detail. Anayemsaidia zaidi homework Mbowe in Ansbert Ngurumo sio Balile. Hata zile Tafakuri anaandika Ngurumo. I have always said kwamba sooner or later, it will emerge as to who the real Mbowe is.



Waungwana wa Jambo Forum, nimekutana na hayo niliyoyanukuu hapo juu. Kama kweli mtu yeyote anaweza kuyatetea hayo yanayosemwa juu yangu, nitaacha kuamini chochote katika forum hii. Huu ni uonevu wa hali ya juu. Ni uchafu usioweza kufananishwa nami. Dhamiri yangu si butu kiasi hicho. Tafadhari mhusika ajisafishe kwa wana forum. Mimi ni binadamu wa kawaida. Siogopi kukosea na kukosolewa. Mbona ninazo kasoro zangu nyingi? Kama mtu anataka kunisema si ataje hizo kuliko kunibandika haya matope yasiyofanana kabisa na utu, hulka na dhamiri yangu? Hiki ndicho mwandishi anaita kukosea 'kidogo?'
 
Let's just close this matter and let the late young lady rest with eternal peace.
 
Basi hii thread iondolewe. Haina kazi hapa kama iko dormant na kama hatuwezi kujadiliana kwa kuwa AC ameaga dunia. Lakini mimi sikutaka kumjadili marehemu nilikuwa nawasema wanaonichafua bila sababu, wanaotunga uwongo na kuubandika hapa. Walidhani nisingeuona? Halafu wanazungumzia objectivity! Waombe radhi kwangu na wana JF.
 
OK,

Kaka Ngurumo nadhani hii hoja imefikia tamati. I will close this topic today around 00:00 East African times. Kama kuna hoja za kupinga ufanyaji hivyo naomba nipewe prior to the next action.

Regards
 
wana jf,
mengi yamesemwa kuhusu kulinda heshima ya forum. wengi ama wamefuta kauli zao au wameomba msamaha pale walipokosea fact au mkosea mtu.

kwenye thread ya "muhingo rweyemamu ..." bwana ngurumo amedai amekosewa na kumtaka mhusika athibitishe madai yake lakini thread imefungwa na malalamiko ya bwana ngurumo yaelekea kumezwa.

sasa kwa msingi ule ule wa kulinda heshima ya forum ni vyema m/wahusika a/wakajisafisha. malalamiko ya bwana ngurumo naambatanisha hapa chini.

idumu forum,

Mnanionea bure

--------------------------------------------------------------------------------

Quote: Invincible
"Hii hapa chini ndiyo post ambayo ulimsahihisha Chinga kwamba sio Balile anayemsaidia Mbowe, bali ni Ngurumo. You seem to be an A-type personality.....ila mimi bado hujanisadikisha kwa lolote.

Mzee Mwanakijiji

I quite don't understand why a member of JF should have to go through your radio to respond to his fellow members.

Chinga,

Umekosea kidogo detail. Anayemsaidia zaidi homework Mbowe in Ansbert Ngurumo sio Balile. Hata zile Tafakuri anaandika Ngurumo. I have always said kwamba sooner or later, it will emerge as to who the real Mbowe is."




Waungwana wa Jambo Forum, nimekutana na hayo niliyoyanukuu hapo juu. Kama kweli mtu yeyote anaweza kuyatetea hayo yanayosemwa juu yangu, nitaacha kuamini chochote katika forum hii. Huu ni uonevu wa hali ya juu. Ni uchafu usioweza kufananishwa nami. Dhamiri yangu si butu kiasi hicho. Tafadhari mhusika ajisafishe kwa wana forum. Mimi ni binadamu wa kawaida. Siogopi kukosea na kukosolewa. Mbona ninazo kasoro zangu nyingi? Kama mtu anataka kunisema si ataje hizo kuliko kunibandika haya matope yasiyofanana kabisa na utu, hulka na dhamiri yangu? Hiki ndicho mwandishi anaita kukosea 'kidogo?'
__________________
Our success or failure depends on how best we put our mental faculties to use
 
Ingekuwa vizuri kama ungetenganisha quotes na maoni yako binafsi. Kwa sasa hivi yamechanganyikana kiasi uwa uliloandika halieleweki vizuri
 
Ni porojo tu zisizo na msingi, kama kweli huyu mtu alikuwa mshauri wa amina Amina asingekutwa na yaliyomkuta, sasa hivi kwa sababu anajua jina la Amina linavutia wasomaji ndio anaandika upuuzi wake. NI aibu kuwatumia marehemu kujipatia faida na umaarufu
 
Media ndiyo ilimuua Amina(RIP). Nashangaa watu kutafuta mchawi kwa kuandika makala mbalimbali.
Mbona Zitto hawakumuandama kama marehemu?
 
asalamu alaykum.

ikiwa medi ndio iliomuuwa Amina kwa kumuandika makala mbali mbali basi angekufa Abdallah Kigoda kwanza maana aliandamwa zaidi na siku nyingi kesi ya mtoto aliyezaliwa na bibi Agnes ambaye kigoda alikataa kuwa sio wake. na wengi tu waliwahi kuandwa kuliko hata Amina.

Amina alikuwa ni mwandishi wa habari kwa hivyo suala la kuandikwa alikuwa analijua vizuri sana na halikumpa tabu na ndio maana baadhi ya wakati alikuwa akijibu na anapotaka hukaa kimya bila ya kujibu kitu tokea awali ya ndoa yake.

kwa fikra zangu lipo lililochangia kumuuwa Amina na sio media. mchawi anajulikana na inshaallah atajulikana zaidi siku zinavyosonga maana hadhulumu mtu ila na yeye atadhulumiwa katika duani hii.

stonetowner
 
Nimeikumbuka hii baada ya jana kumuiona Nchimbi.......
 
Kwa mtazamo wangu iwe msongo, media na chochote kifo cha amina kilisababishwa.na kama kilisababishwa basi amina aliuawa.hata baadhi ya sumu hufanya mwili kubadilika rangi.na kwanini ghafla vile kwa tatizo kama la ndoa ukichukulia amina alikuwa akideal na jambo hatari kiasi kile.walimuua basi.
 
Back
Top Bottom