Unajizungusha ili usijibu swali ninayokuuliza ,NENO ZABURI,NA ISRAEL huko kwenye uislamu yana maana gani au mmeiba kitu msichojua maana yake
Halafu Mimi nakupa maandiko, makabila yote ,awe lawi, Benyamin,Yuda ,waliitwa Wayahudi ,
Nakupa ushahidi ,hapa ni mwaka 538BC baada ya kutoka utumwani Babeli,
Manabii waliwaita wote WAYAHUDI, sasa kama unabisha leta ushahidi
Ushahidi nakupa maandiko
Ezra 4:12
"Na liwe wazi kwa mfalme, ya kwamba Wayahudi waliokwea kwetu, kutoka kwako, wamefika Yerusalemu; wanajenga tena mji huu wa uasi, tena mbaya, na wanakamilisha kuta zake, na kuondoa misingi yake."
Hapa Ezra anawaita wote Wayahudi, hata kama walikuwa wa makabila tofauti, kwa sababu waliokuwa wakirudi walihesabiwa kama taifa moja.
Ezra 5:1
"Ndipo manabii Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakatabiri kwa Wayahudi waliokuwako katika Yuda na Yerusalemu, kwa jina la Mungu wa Israeli aliyekuwa juu yao."