Muasisi awashukia 'wabaya' wa CHADEMA

Muasisi awashukia 'wabaya' wa CHADEMA

Status
Not open for further replies.
...


Utaratibu ule ni mzuri kwa wairan na unawafaa kuogopa kuingizwa kwa mamluki wa kimarekani ndan yataifa lile,


Kwa maana mimi sion TOFAUTI BAINA YA MZEE MTEI NA JINS ANAVOKIENDESHA CHADEMA NA AYATOLLAH ALKHEMEI NA JINS ANAVOIENDESHA IRAN KAMA NCHI,SEMA TOFAUTI NI KWAMBA AYATOLLAH ANA SAUTI KITAIFA HUKU MZEE MTEI ANA SAUTI KICHAMA.

TUSEME WAZI NA KUMWAMBIA MZEE MTEI KWAMBA CHAMA HIKI KAMA KWELI ANATAKA KIPEWE IMAN NA WANANCHI,AKIACHIE KWA WANANCHI MOJA KWA MOJA,NA AONDOE FIKRA ZA U-YATOLLAH ALKHEMENEI,ATALIGAWA NA KULIGHARIM TAIFA.


#TEAM ZITTO...


Mara Chadema ni chama cha Kikatoliki na leo mnazuka na jingine - Chadema kama anavyofanya Ayatollah, Kiongozi Mkuu wa Kiislam wa Iran! Sijui tuelewe lipi? Hebu muwe na malengo mamoja badala ya kubadili badili kauli kila uchao.
 
Tuizungumzie Chadema kama M'BADALA WA CCM,,,
Ritz
Mimi binafsi nakupongeza kwa hizi bayana zako kitu kigumu kwa Chadema wanataka chama chao kiwe cha kitaifa lakini maamuzi ya chama na maelekezo yatoke kwa waasisi.

Bado chama kinakosa sifa ya utaifa mfano tumeona baadhi ya wanachama wamejipanga kugombea uongozi wanaitwa waasi na wahaini haiwezekani kuwa na fikra moja.

CCM sasa hivi kila kundi lina mipango yake ya kugombea urais hakuna mwenye kauli ya kuwambia wenzake waasi, kuna Sitta, Membe, Lowassa, Sumaye hawa wote wanautaka urais.

Chadema ukionesha nia ya kugombea uongozi wa juu kama Katibu na Mwenyekiti unaitwa muasi au masalia.
 
Last edited by a moderator:
Iran utaratibu ule unawasaidia kama nchi kuepuka kuingiza nchi kwenye umamluki wa marekani,ndio kwa maana ayatollah amepewa nafasi na sauti ya kusema,

...

Kaka, huyo Ayatollah sio binadamu? Hata yeye anaweza kuwa mamluki vilevile. Au ni jini yule?
 
lengo chadema kuwa na mfumo kama huo ni kujiengea utaratibu wa kula hela na kutawala milele watu wa kutoka upande mmoja kitu ambacho ni sumu kubwa kwa ustawi wa demokrasia.


Chadema wana mfumo wa kiislamu siku hizi? Sio ukatoliki tena? Wanafiki wakubwa ninyi.
 
With all of my due respect,baada ya salamu mimi sipo hapa kufanya propaganda wala kumchafua mtu yoyote,

Sijataumwa na yoyote,na nasimama kwa msimamo wangu binafsi katika kuelezea kile kilichopo fikran mwangu,

Kama Mtanzania mzalendo,mchukia mafisadi na muumin wa siasa bora na uongoz imara lazima nisimame kuelezea kitu nachokiona,

Hatuna shida na Mzee Mtei kama miongoni mwa waasisi wa chama hiki,na hatuna shida na wenngine wowote wale ambao kwa namna moja ama nyinine wamekuwa ni wanafamilia wa mwasisi huyo wa chama hiki,

Sisi kama Watanzania linapokuja suala la kuathirika kwa utawala m'bovu huwa tunapata athari hizo sote bila kujali umri,jinisia,kabila,kanda,dini na kadhalika,so as long as wewe na mimi tumekuwa ni wananchi na raia wataifa hili tunaathiriwa moja kwa moja kwa mamuzi ya wanasiasa either wawe wa chama tawala au chama cha upinzani,

Ni jukumu letu sisi wananchi kuhakikisha tunakuwa mabalozi wa siasa safi ili serikali itayokuwa madarakani iwe ni imara itayotuhakikishia maamuz sahihi na usalama wa taifa dhidi ya maadui wa ndan na nje ya nchi,

Ili tufikie hali kama hiyo tunahitaji chama ambacho hakiwez kuegemea kwenye maamuz ya kutoka upande mmoja ambao unajinasibisha kuwa na MORAL AUTHORITY YA KUTOA KAULI ZINAZOHIATJI KUSIKIKA KWA KUWA TUH ETI UPANDE HUO NDIO HASA ULIOPELEKEA KUASISIWA KWA CHAMA HIKO,HILI LAZIMA TULIWEKE WAZI MAPEMA SANA.


Katiba ya chadema hakuna kipengele hata kimoja kinachosema kwamba watu wapewe kipaombele kutokana na ukanda,udini na ukabila hata sehemu moja,yani kwa ufupi katiba ya chadema inapinga kwa nguvu zote mambo ya ukanda,ukabila na udini katika kulijenga taifa hili kwa kizazi cha sasa na cha baadae,hilo liko wazi na sote tunaunga mkono katiba ya namna hiyo...

Katika mukatadha huo basi yatupasa kuwaambia chadema wasimame katika misingi hiyo na kuionesha wazi wazi kwa vitedno na kila mtu aone na sio kuishia kuhubiri mambo hayo majukwaani huku upande wa pili ukionekana kuwa na malalamiko yasiyo kwisha,REJEA YA MAREHEMU CHACHA WANGWE NA HAYA MASAHIBU YANAYO WAKUTA KITILA MKUMBO,MWIGAMBA NA ZITTO KABWE KAMA MIFANO HURU KATIKA MJADALA HUU,


Chadema lazima itambue kwamba watanzania walio wengi pamoja na kuchoshwa na CCM wanahitaji m'badala thabiti na unaoijipambanua wazi wazi kiutawala,kikatiba na kitaifa.

Hoja ya AYATOLLAH ALKHAMENEI,YULE SUPRME LEADER WA IRAN NA JINSI WANAVYOENDESHA DEMOKRASIA YAO NAIFANANISHA MAJA KWA MOJA NA CHADEMA,NASEMA HIVYO KWA SABABU,

1.AYATOLLAH ALKHEMENEI.,yeye yupo juu,rais,mwnyekiti wa chama,bunge na mahakama vyote vinaripoti kwake,

Chama na bunge hawawez kupitisha jina la mgombea urais wa nchi ile bila baraka wala idhin ya YATOLLAH ALKHEMENEI KWA KUOGOPA KUWEKWA KWA MAMLUKI AU VIBARAKA WA MAREKANI KWENYE UTAWALA WA SERIKALI YA IRAN HASA KWENYE KIPINDI KAMA HIKI AMBACHO WANAPAAMBANA NA SIASA KALI ZA ISRAEL NA MAREKANI,HUSUSANI SUALA ZIMA LA NYUKLIA NA UONGOZ KWA UJUMLA,,Utakuja kuona kwamba MAHMOUD AHMEDNIJAD RASI ALIEMALIZA UTAWLA WAKE ALIKUWA MTIIFU KWA SYSTEM YA AYATOLLAH,WATU WAKADHANI KWAMBA KUJA KWA HASSAN ROUHANI RASI WA SASA WA IRAN BASI HATOKUWA MTIIFU KWA MFUMO ULE,HALI HAIKUWA HIVYO KWANI ROUHANI ALIPOINIA ALIONEKAN KUWA MODERATE TOFAUTI NA NIJADI LAKIN WOTE NI WALE WALE,WOTE WANAPOKEA AMRI KUTOKA KWA SUPREME LEADER KWA KILA HATUA..


Utaratibu ule ni mzuri kwa wairan na unawafaa kuogopa kuingizwa kwa mamluki wa kimarekani ndan yataifa lile,


Sasa nauliza swali,je utaratibu huo unafaa??na je unaweza kusaidia taifa kwa ujumla??mimi naona utaratibu huo kwa chadema kama chama una wafaa,tatizo ni kwamba je wakipewa madaraka ya nchi utaratibu huu utakuwa healthy kwa manufaa ya nchi??

Kwa maana mimi sion TOFAUTI BAINA YA MZEE MTEI NA JINS ANAVOKIENDESHA CHADEMA NA AYATOLLAH ALKHEMEI NA JINS ANAVOIENDESHA IRAN KAMA NCHI,SEMA TOFAUTI NI KWAMBA AYATOLLAH ANA SAUTI KITAIFA HUKU MZEE MTEI ANA SAUTI KICHAMA.

TUSEME WAZI NA KUMWAMBIA MZEE MTEI KWAMBA CHAMA HIKI KAMA KWELI ANATAKA KIPEWE IMAN NA WANANCHI,AKIACHIE KWA WANANCHI MOJA KWA MOJA,NA AONDOE FIKRA ZA U-YATOLLAH ALKHEMENEI,ATALIGAWA NA KULIGHARIM TAIFA.

#TEAM ZITTO...

Huu now ni ujinga mwingine wa Jumamtatu mapema .Haya yote hayana maana .Ya maana yalikuwa Jana na kabla ya jana kwenue Kamati kuu .
 
hayyattullah usimlinganishe na Fisadi mtei,Kiongozi wa juu wa Iran ni Mwadilifu kuliko unavyofikiria,lkn viongozi wa chadema ni Mafisadi wanaotumia rasilimali kujiimarisha na kujineemesha wao na familia zao. Ndio mana hakuna anaestahili kutawala chadema zaidi ya mkwe wa Mzee Mtei, ukithubutu tu utaitwa umetumwa na hivyo wewe utakiwa msaliti. Chadema hawapaswi kuaminiwa hata nusu dakika maana wakishika nchi,activity ya kwanza ni kubadili katiba na kuondoa kikomo cha kutawala ktk urais,Slaa na Mbowe watatumia vyombo vya dola kubaki madarakani na Watanzania tutajuta na naamini yatatokea machafuko.
Mbowe na Slaa watatumia hii propaganda kung`ang`ania madaraka. Na kila atakae jaribu kutaka urais ataambiwa katumwa na Kagame au wamagharibi.
Mabadiliko ni lazima,mbowe must step down.
 
Mabadiliko ni lazima na wasioyataka mabadiliko waondoke chadema. Tunataka kuona kiongozi aliyetokana na kura za wanachadema na si mteule wa Mzee Mtei. Pia tunataka kujua mtei uliwekeza shilingi ngapi chadema ili urejeshewe ili chama kitoke mikononi mwa genge la wahuni wachache na hatimae kiwe cha watanzania.
 
Hivi mnajua siku ya kwanza kabisa mtu na mkwewe wanapanga kuanzisha chama walikuwa na vision gani? Mkijua hilo ndio mtajua mko sahihi ama lah. Ukute aidia ilianzia sebuleni, tena nyumbani kabisa wakiwa wanapata kahawa, wakapanga na mission ya kusaidia kufanikisha vision yao. Leo vyasaka mnataka nini??? Kiruuuu

Labda nyie hii inahusu mapinduzi ya kuing'oa shishiemu, wakati wenzenu labda ni family matter, tena yenye sentimemtal values za hali ya juu, na labda warithi ni wajukuu. Haka kama sio na uhusiano vile, lazima awe anayeweza kushikiwa rimoti bila chenga. Wao watashika rimoti, yeye ni actons tu hii haaa puuf puuf, dishwaa dishwaaa.

Raha ya mdumangu uuanzie mwanzo, ukikubeba juu kwa juu unapotea wewe.
a
Mkuu kweli we umeongea jambo moja zuri sana!!! naomba nikuulize labda unaweza kunisaidia kwenye hiki kirefu cha chedema yaani CHAGGA DEVELOPMENT MANIFESTO, je kuna ukweli kwenye hili?
 
THE BIG SHOW.
Nimesoma maelezo yako, ni kweli chama kinabidi kiwe cha WANANCHI na sio baadhi ya viongozi, lakini ukitaka mzee Mtei asitoe mawazo yake huoni kama utakua pia unamnyima hiyo demokrasia unayotaka awenayo yeye kama mwanachadema na mwananchi wa Tz?

Sidhani kama mzee Mtei ni sawa na Ayatolla, mzee Mtei yeye hatoi maamuzi ila anaombwa ushauri kama jinsi ambavyo CCM inaomba ushauri kwa viongozi wake wa zamani. Mzee Mtei kukubali maamuzi ya Baraza lililowavua uongozi Zitto na Dr Mkumbo nako pia kuna mfanya awe mtiifu kwa maamuzi ya Chama kama walivyofanya wengine Dar,Mbeya n.k kupongeza maamuzi ya chama.Sasa mbona unamlaumu mzee Mtei pekee ukaacha kuwalaumu viongozi wa Nyanda za juu Kusini kubariki maamuzi ya Chama, je yeye Mtei kama alivyo mwanachama mwingine haruhusiwi kuwa na fikra zake?? au awe mnafiki??

Naamini mzee Mtei kama mwasisi angependa siku moja aone chama kikishika madaraka angali hai, labda siku zake zikiisha basi huko mbele za haki apate kuwahadithia (kama pia wanaongea kama sisi) waasisi wenzeke kuwa ndoto zao zimetimia. Naamini kwa sababu hiyo hawezi kukaa kimya mambo yakienda vibaya kwa kuhofia kuitwa Mkanda, Ayatollah au jina lolote lile. Anataka aione ndoto yake ikitimia.

Naamini kilichokupeleka kuandika uzi huu ni maamuzi ya kumvua Zitto na Dr Mkumbo uongozi, ukihofia kuwa labda propaganda za ccm za ukanda zinaukweli. Lakini nenda nyuma na rejea kumbukumbu kwa uaminifu wa hali ya juu na ujiulize maswali, je ni mara ngapi Zitto amekuwa akihusishwa na CCM?? Je Mwigulu aliyesema hadharani kuwa adui yake ni Shetani na CHADEMA kwanini amlilie Zitto kusimamishwa uongozi???? Je alivyosema kiongozi wa juu wa Chadema yupo tayari kutoa ushahidi wa video ya ugaidi wa Lwakarate, na Zitto kutoka hadharani akitaka Lwakatare ajiuzulu nafasi yake Chamani inakupa picha gani????

Labda yawezekana Zitto hana usaliti wowote ndani ya chama lakini wenzake wanamuona kama anatumika na adui yao mkuu CCM,sasa katika mazingira hayo bado anahitajika kufanya kazi na watu wasio na imani naye?? ni ama wao wajitoe au yeye ajitoe ili pasiwepo na kutoaminiana kazini/ofisini. Rejea msemo wa Julius Kaisari (Julius Caesar) "Caesar's wife must be above suspicion" kwa nini wewe kiongozi wa ngazi ya juu utuhumiwe kusaliti chama?? hata kama sio kweli lakini ulipaswa uwe juu ya tuhuma hizi.

THE BIG SHOW mzee Mtei kama Mtanzania na mwanachadema mwingine anayo haki ya kusema, sio lazima kila asemalo liwe hivyo au sahihi lakini kumzuia kusema kwa kuhofia kuitwa Wakanda,Wakabila,Wadini,Wamangimeza n.k n.k pia ni uoga na unafiki.

"CCM lazima itoke magogoni ili kunusuru Tanzania yetu leo na mbeleni" by mimi mwenyewe



Shukran sana Mkuu,

Ni kweli haya yote yamenza kufumuka baada ya hili seke seke la zito na bado yataendelea kufunguka mengine mengi sana,

Zitto ni kama mwendelezo tuh,tunajua wapo waliojaribu hapo mwanzo kuuchallange mfumo kama marehem chacha wangwe lakini mwsho wa siku mungu hakupenda aendelee kubakia ulimwenguni akamchukua,

Mtei haishii tuh kuambiwa akae mbali na chama,mtei kama muasisi alimsimika mtu kama mbowe awe mwenyekiti wa chama ambae kifamilia ni mkwe wake,kwahiyo utaona jins graph inavyokwenda,

Kama hiyo haitoshi.wanapotokea watu kutangaza nia ya kutaka kumvaa huyo mwenyekiti yeye huwa kikwazo na huwa mbele mbele kuwakatisha tamaa watu hao kwa sababu mbali mbali ambazo hazina msingi jambo ambalo hutafsiriwa kama ni muendlezo wa UYATOLLAH NDAN YA CHAMA HIKI
 
Huyu mzee ni majanga. Ukitemwa na nyerere wewe hufai tena katika uwanja wa siasa.



Aah wapi mkuu hebu acha kupotosha umma. Wengine tulikuwa wakubwa wa kuelewa kile kilichojiri kuhusu kutofautiana kati Nyerere Vs. Mtei.! Hata Nyerere mwenyewe alikuwa 'on very wrong side of history' katika tofautiana yake na Mzee Edwin Mtei.

Briefly;

Tanzania ilikuwa ikihitaji mikopo ili kujijenga tena kiuchumi mara baada ya vita ya Kagera mwishoni mwaka 1979. IMF/World Bank wakiiwa wakopeshaji wakuu walikubali kukopesha kwa moja ya masharti kuwa thamani ya shillingi ishushwe (depreciated). Mzee Mtei akiwa Waziri wa Fedha alikubaliana na kuwa na maono juu ya hoja ile na kumshauri boss wake Nyerere kwa uaminifu mkubwa kabisa.

Kumbuka kushusha thamani ya shilingi ndio ulikuwa 'mwarobaini' pekee Tanzania inao weza kuumeza ili kuweza kutibu mtikisikio wa kiuchumi ambao ulisha athirika vibaya sana maisha ya WaTanzania mara baada vita ya Kagera mwaka 1979. Nchi ilikuwa imefilisika (bankruptcy). Hakuna bidhaa wala vyakula madukani. Mafuta ya mgao. Kuetembeza magari jumapili bila kibali baada ya saa 7 mchana mwiko. Haya yote yalitokea Nyerere na Mtei yalianzia mwaka 1980.

Mwisho wa siku Nyerere anamfukuza kazi Mzee Mtei baada kuukata ushauri wake kuwa shilingi ishuke thamani. Maandamano yanakuwa mobilized ki CCM style nchi nzima baada hotuba ya Nyerere kule Kigoma (I think it was May Day 1980 then😉. Maandamano ya kulaani IMF/World bank kwa kutushauri kushusha thamani ya shilingi yetu.

WaTanzania wengine kwa "Umaamuma' wao wa jambo hili wakidhani Mzee Mtei ndio alikuwa tatizo au aliyetaka kuiuza nchi kwa WorldBank na IFM. Tanzania baada ya hapo inaamua kuvunja mahusiano na wakopeshaji hao maarufu. Wananchi wanaendelea kuteseka na hali ngumu ya uchumi.


Mwaka 1985 Rais Nyerere anaondoka madarakani. Rais Ali Hassan Mwinyi anachukua uongozi ili hali kiuchumi Tanzania ikiwa kwenye hali mbaya mno. Jambo la kwanza analofanya Mwinyi ni kufungua mahusiano na IFM /World ili aweze kukopa na serikali iweze kujinasua kutoka kwenye hali mbaya kifedha.

IFM/World wanawakumbushaia masharti ya awali Tanzania iliyokataa miaka mitano nyuma kuwa thamani ya shilingi ni lazima iteremke na mengineyo. Hilo linafanyika mara moja. Na hapo hali ya uchumi unaanza dalili za kufufuka. Na ndio enzi za 'Rukhusa' zinaanza. Inakuwa ndio chanzo cha sera ya uchumi huria 'Trade liberalization' nayo inapiga hodi Tanzania. WaTanzania waanza kupumua kidogo kupata ahueni ya kiuchumi/maisha kwani maduka fedha za kigeni yakaanza, nguo za mitumba, bidhaa madukani tele, watu waakanza walau kuagiza magari (mitumba Peugeot 504/505, Vi Costa hizoo, Pick up Double Cabin🙂

Kikubwa ninachotaka kusema hapa ni kuwa miaka minne tu mbele ya safari baada ya Nyerere kumuona Mtei hafai Tanzania ilikuwa haina jinsi bali kukubaliana na hoja ile ile ya IMF/World na ushauri wa aliyekuwa Waziri wa Fedha Mzee Mtei.

Mzee Mtei aliachia ngazi huku akiamini bila ya kuyumba wala mashaka kuwa ni lazima "thamani ya shilingi ishuke' ili kuweza kufanya uchumi wetu uweze kuunguruma tena. Nchi ilisha athirika na matumizi makubwa yaliopitiliza na ya ghafla ambayo nchi haiku yapangia. Vita iliyo tugharimu karibia Tshs 4.5 billioni siku hizo (wakati huo dola nafikiri kati Tshs 4/= lakini ilikuwa haizidi 7/= sina hakika sana maana muda umekwenda kidogo🙂

Nyerere kule kwenye hotuba ya Kigoma alisema msimamo wake kwa IMF/World bank ni kuwa 'hawezi kugeuka nyuma.... akawa jiwe la chumvi' (refer to a biblical story). Ukweli ni kuwa Tanzania iligeuka nyuma kwa IFM/World na wakasaini masharti (conditions) yale yale waliyokataa punde baada ya Mwinyi kushika madaraka kama Rais na Nyerere akiwa ni Mwenyekiti wa CCM.

Nakumbuka Nyerere alitoa speech moja nafikiri akiwa tayari ameshang'atuka kabisa sikumbuki mahala na muktadha. Katika maongezi yake alikumbushia kisa chake na IMF/World bank and how roughly he pushed away Mtei from his post. Kwa kweli alisikika katika sauti yake alikuwa 'so guilty, very sorry na very emotion' (japokuwa hakusema sorry moja kwa moja lakini kama wewe ni mtu mzima unajua kabisa how deep inside Mwalimu was sorry about his actions. Hapo pia nilipata kuona kuwa Mwalimu hakumchukia Edwin (as Mwalimu refer Mtei) kama watu wengi wanavyo dhani.

Kwa maoni yangu juu ya kisa hiki ni kama Mwalimu ali vent all his frustrations with IMF /World Bank kwa Edwin Mtei (ambaye alikuwa mrahisi wake) kisa tu kuwa na yeye alikubalina na conditions zile za IFM kuwa ni tiba au 'mwarobaini' wa kunusuru uchumi wa nchi walau nchi iweze kukopesheka (credit worthy) tena.

Na kwa upande mwingine binafsi nimeona kuwa Mzee Mtei ni mtu muungwana sana kwa viwango vya Wazee wengi wa kiTanzania waliofanya kazi na Mwalimu. Si mtu mwenye chuki/kisirani wala kinyongo kwa Mwalimu. Ukweli ni kuwa sijapata kuona mahala popote akieleza kwa njia ya chuki (past bitterness) jinsi mahusiano yao ya kikazi yalivyofikia njia panda.
Hajapata kumvunjia heshima kwa kumponda Mwalimu (hata baada ya Mwalimu kufariki) kama Wazee wengine ambao walipata kukorofishana na Mwalimu katika utumishi wa umma jinsi wanavyomwaga nyongo kama simba aliyejeruhuiwa🙂

Kuna kisa kimoja ambacho nilipata kukisikia juu ya Nyerere na Mtei baada ya kuwa wameshakwenda separate ways. Bahati nzuri Mzee Mtei yupo hapa jamvini ikitokea akisoma na pengine akiamua kunisahihisha kama si kweli lakini wacha nishee na wewe;Nia ikiwa ni ku enlight mahusiano ya hawa watu wawili;

Ilikuwa hivi; baada ya kuwa Nyerere na Mtei mahusiano yao ya kikazi yameshafikia njia panda. Safari moja Nyerere nasikia alikuwa either Moshi au Arusha kwa shughuli fulani. Akiwa pale kwenye shughuli na kusalimiana na mazungumzo na watu pale high table aliuliza kama How Edwin Mtei he was doing? Akaambiwa mbona yupo hapa lakini yuko nyuma huko kidogo kutoka kwenye high table ilipo (...Mwalimu akaagiza wamstue aje pale alipoketi wasalimiane). Nasikia Mzee alipokuwa akikaribia ilipo meza kuu alipokaa Mwalimu alisimama na wote wakasalimiana wakiwa ni watu wenye furaha na nyuzo za bashasha....Na umati wote ukashangaa kwa furaha kuwa hawa watu walio kuwa wakifikiri kuwa ni maadui wakubwa kumbe they still have some love and respect for each other.

Imenilazimu kutoa maelezo marefu kidogo ili hawa members ambao wa 'kizazi kipya' wapate kuelewa ni nini haswa kilijiri na hata kusabisha uhusiano wao wa kikazi kufikia njia panda hapo mwaka 1980. Na kwa mujibu wa mapokeo (memor) zangu juu ya kile kilichojiri.

Mwisho, nahitimisha kwa kutofautiana na wewe kwa kusema 'Mzee Mtei sio janga'. Na si kila yule aliyetemwa na Nyerere kuwa hafai katika uwanja wa siasa.
 
Mimi binafsi nakupongeza kwa hizi bayana zako kitu kigumu kwa Chadema wanataka chama chao kiwe cha kitaifa lakini maamuzi ya chama na maelekezo yatoke kwa waasisi.

Bado chama kinakosa sifa ya utaifa mfano tumeona baadhi ya wanachama wamejipanga kugombea uongozi wanaitwa waasi na wahaini haiwezekani kuwa na fikra moja.

CCM sasa hivi kila kundi lina mipango yake ya kugombea urais hakuna mwenye kauli ya kuwambia wenzake waasi, kuna Sitta, Membe, Lowassa, Sumaye hawa wote wanautaka urais.

Chadema ukionesha nia ya kugombea uongozi wa juu kama Katibu na Mwenyekiti unaitwa muasi au masalia.


Shukran sana Mkuu Ritz,

Hapa lazima tuweke maslahi ya TAIFA MBELE KWANZA
 
Uchaguzi ndani ya chadema mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa 2015! sasa asiyetaka aende CCM. Dr.Slaa alishasema CDM haiwezi kuwa CCM B...

Masahihisho kidogo Dr Slaa alisema uchaguzi mpaka CDM itakapo kuwa imara na hii inamaana hadi 2095!

Yaani hadi 2095 asiye taka akihame chama! Hii ndio demokrasia tunayoitaka!
 
Naona unajisumbua tu chadema hakuna uchaguzi mbowe na slaa ni viongozi wa chadema milele mpaka watafia chadema wote mnaotaka madaraka chadema tutawafukuza.

Kwa mantiki hiyo CDM siyo chama cha wananchi bali ni chama chenye maslahi kwa wachache? Kinaongozwa kwa mujibu wa katiba,au kwa matakwa ya Mtei? Mi nashauri tuache ushabiki wa kichama na kutukana matusi,na tuangalie km katiba ya CDM inasemaje juu ya muda wa uongozi ndani ya chama. Km Cdm ikitawala,tutegemee utawala wa kifalme. Yaani Rais mpaka afe ndo unafanyika uchaguzi. Ndo chama kweli tunachopigania tukipe dola? "TUTAFAKARI NA TUCHUKUE HATUA"
 
Kwa mantiki hiyo CDM siyo chama cha wananchi bali ni chama chenye maslahi kwa wachache? Kinaongozwa kwa mujibu wa katiba,au kwa matakwa ya Mtei? Mi nashauri tuache ushabiki wa kichama na kutukana matusi,na tuangalie km katiba ya CDM inasemaje juu ya muda wa uongozi ndani ya chama. Km Cdm ikitawala,tutegemee utawala wa kifalme. Yaani Rais mpaka afe ndo unafanyika uchaguzi. Ndo chama kweli tunachopigania tukipe dola? "TUTAFAKARI NA TUCHUKUE HATUA"

Ndio CDM hiyo hadi Mbowe afariki ndio uchaguzi ufanyike
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom