Mtwara: Gari la 'Afisa Usalama' lapondwa mawe Msimbati

Mtwara: Gari la 'Afisa Usalama' lapondwa mawe Msimbati

Wadau, kuna habari hii aloiweka Mh. ZZ Kabwe, Facebook. Namnukuu

Taarifa nipatazo kutoka Msimbati, Mtwara sio nzuri sana. Kuna gari imechomwa moto na vurugu kidogo usiku wa kuamkia leo. Sijajua chanzo hasa ni nini, lakini vurugu za aina yeyote ile hazifai. Kutoelewana kati ya Serikali na Wananchi kumalizwe kwa mazungumzo badala ya ubabe na fujo. Nimeambiwa polisi wamemwagwa kijijini Msimbati, wazee kadhaa wa kimila wamepigwa sana. Haya tuyakatae, sio Utanzania
.

Naomba kama kuna mtu mwenye upana zaidi wa yaliyotokea huko atujulishe zaidi. Hili jambo sasa linatishia usalama wa Mtwara, na hatimaye usalama wa nchi.
 
Najiandaa kwenda MTWARA kama local investor.
 
Utemi na ubabe!! Sikujua umburula wa jk ni wa this level!!
 
Kwa wenye marafiki walio Mtwara tufanye mawasiliano tuulize kama habari hizi ni za kweli. Sitaki kuamini kuwa serikali imekosa busara kiasi kikubwa namna hiyo!
 
kwa viongozi wa namna hii tz ndio maana hatuendelei hv hawana ya msingi ya kutafaari na kufanya ili nchi iendelee wan.....
 
lakini sishangai wao kuamini uchawi, kwa sababu wengi wao wameutumia sana kuingia na kuendelea kukaa katika nafasi walizopo wataacha kuuogopa na kuuamini?
 
|Haya sasa! ngoma inogile - serikali itafakari na kuona uwezekano wa kufanya mipango shirikishi
 
Serikali ya kiimla tayari hii, unaweka mkataba na wacina kwakuwa tu mtu wako kamamatwa na unga kwa ajili ya aerdhi na maliya wananchi
 
Tanzania is nomore the land of peace!! maana watunza amani ndio wavunja amani "numero uno"
 
kila namna inayowezekana kuzuia gesi kwenda dar itumieni wana mtwara kitu gani bwan liwalo na liwe
 
Lazima awe na undugu na Kibibi Gula wa "Usiku wa Manane" akilindwa na kina mzee Ole.

umenikumbusha mbali sana kuhusu huyu kibibi Gula, zama ambazo niliweza kusoma maandiko ya waandishi wa Kitanzania na kuyaelewa vizuri kutokana kuakisi nyakati, mazingira na utamaduni.
 
Back
Top Bottom