Mtu kapigwa risasi Mlimani City Dar es salaam

Mtu kapigwa risasi Mlimani City Dar es salaam

Dah hii ni noma kwakweli, polisi sijui wanafanya nini??
 
Hii ni hatari mi naona boda boda zifungiwe kabisa leo asubuh saa kumi nambili wamechomwa boda boda wawili moto njee ya geti yangu baada ya kumkwapua dada kIPOCHI na kukamatwa hapa tabata Liwiti sasa wamezidi mwanangu
 
Itakusaidia nini? Ni Mtanzania habari imeishia hapo.

hivi ungekauka tu aliye msiban akanijibu ungepungukiwa nin? m nimeuliza kwasababu jina lake linafanana na watu wa kwetu nilikuwa nataka jamaa anidhibitishie.usikariri mkuu
 
Dah hii ni noma kwakweli, polisi sijui wanafanya nini??
Wapo mkuu na wanafanya kazi kweli kweli!
Nilikuwa nafuatilia clips ya ITV habari jana ikimuonyesha kamanda Kova alivyojipanga kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama kuhakikisha ukaaji wa wazee wastaafu wa mpira kutoka Ulaya na Ufaransa wanakula holiday yao kwa amani bila bugudha.

Atafadhali, atakayetuwekea hiyo clip nitampatia 'like' 10,000.
 
Hii habari ya kupigwa mtu risasi Mlimani city na majambazi ni kweli au uzushi?





------------------

Something very wrong with the areas surrounding mlimani city. Kuna siku mama mmoja aliporwa pochi kwa mama kamche halafu prado moja ikablock njia ili boda boda wakimbie. Ile Prado I think walikuwa wana uhusiano wa moja kwa moja na waporaji. Mana alijidai haoni sehemu ya kupaki.
 
Mlimani City na maeneo ya survey yanatakiwa yaangaliwe kwa karibu na vyombo vya usalama. Naanza kupata wasiwasi Kuna genge la wahalifu linaoperate maeneo yale
 
Wengi naona hawajui chanzo cha yote haya, jamani bila serikali kuweka mipango mizuri kwa ajili ya kupambana na umaskini pamoja na ukosefu wa ajira mtazidi kuwalaumu polisi bure. Hata ukiweka cctv bado si jibu la mtu mwenye njaa ambaye serikali imeshindwa kumuekea mazingira ya yeye kupenya. Haya ndio matokeo ya mipango mibovu ya serikali na hata wao viongozi bado hawatakaa salama. Nakumbuka Mh Ngoyai Lowassa uwa anasema bila kutafuta fursa kwa ajili ya vijana ni sawa na kutengeneza bomu siku moja litalipuka.
 
Tsh 18Mil ndio ipelekee kumuua mtu,kweli hali ya maisha ngumu,Au labda walipewa wrong information kwamba zilikua mil 180?
R.I.P Mr Adson Cheyo.

serikali ya ccm ndio imetufikisha hapa,kwa hali ngumu tuliyo nayo mtu anaweza kukuua kwa sababu ya mia tano tu ina uma sana yani....poleni familia ya marehemu mungu awa letee wepesi kipindi hiki kigumu cha majonzi.
 
Wengi naona hawajui chanzo cha yote haya, jamani bila serikali kuweka mipango mizuri kwa ajili ya kupambana na umaskini pamoja na ukosefu wa ajira mtazidi kuwalaumu polisi bure. Hata ukiweka cctv bado si jibu la mtu mwenye njaa ambaye serikali imeshindwa kumuekea mazingira ya yeye kupenya. Haya ndio matokeo ya mipango mibovu ya serikali na hata wao viongozi bado hawatakaa salama. Nakumbuka Mh Ngoyai Lowassa uwa anasema bila kutafuta fursa kwa ajili ya vijana ni sawa na kutengeneza bomu siku moja litalipuka.

Penye njaa hapana amani asilani,ila majambaz ya sk hiz yamezid,kwanin yasitishie katika uporaji wao,mpaka waue,Mh Raisi usalama wa raia upo mashakani,kwani hayo majambazi hayakamatiki,na sisi wananchi tuache kujitoa ufahamu kuchomesha mtu akiwa anapeleka pesa benki,na wapeleka hela epukeni same routine daily,unakuwa easy kuwa targeted,or marked by snitchers,either way muombe escort ya polisi,mbona nackia wanacharge hela kidogo tu.(ni hayo tu)
 
Jamani suala la ujambazi Dar sasa linatisha, tena wanauwa wawekezaji wetu wazawa kinyama? Suala hili inahitaji mkakati mpya kukabilina nalo tusipoangalia Dar inageuka kuwa Johannesburg muda si mrefu.
 
dah kama ni kweli police wanatakiwa watoe maelezo ya kina zile land cruiser ni za kazi gani kama zimewashinda wanipe nikazikate niziingize kwenye utalii mi sielewi hapo mlimani city ni mjini sana

kifupi biashara ya bodaboda ipigwe marufuku tubaki na bajaji tu.
 
Tsh 18Mil ndio ipelekee kumuua mtu,kweli hali ya maisha ngumu,Au labda walipewa wrong information kwamba zilikua mil 180?
R.I.P Mr Adson Cheyo.

18mils ndogo?!u cant be serious kibongobongo?!!
watu wamepinda asa hv wanaua kwa milioni 2.....!!!
mi nahisi deal limeanzia kwa watu wake wa karibu from nowhere haiwezekani tu wamfate na kumuua only him
 
Poleni wafia; na Adson akapumzike kwa amani; amen.

Serikali, hivi wale askari walopewa bodaboda kuna siku wameweza kudhiti uharamia au taarifa hizo ni siri. Mi kwa macho yangu nimekwishwa washuhudia wakisimamisha magari ya mizogo na kuyakagua sasa sijui wao ni maofisa wa TRA au askari wa usalama barabarani.
Kama taifa bado tunasafari ndefu ya kuweka mifumo ya kuwasaidia na kulinda usalama wa raia na mali zao
 
Huu ni mchongo majambazi hawawezi kuvamia na kupora kwa kukurupuka
 
Mkuu ubebaji wa hela ni kitu cha muhimu sana siyo unabeba hela kma laptop,kwa mjini ni heri uwe n mpesa ambayo unaweza weka hela nyingi.
Mimi naweza beba hiyo 18m kwenye mwili wangu na usijue.ila cku yko ikifika ndio hvyo

Mkuu yawezekana uko sahihi lakini tatizo ni kwamba wanakuwa na wewe tokea bank, hivyo hata uzibandike gundi mwilini wao watazitaka. Wafanyakazi wa mabenki wengi siyo waaminifu kabisa wanashirikiana na majambazi, ukiwa unadraw pesa nyingi kisha ghafla teller anashika simu yake anambeep jambazi kuwa kuna mteja "mkubwa". Ukitoka uko nao hadi wazipate.

Jambo la msingi inapotokea hali hii ilitakiwa teller aliyemhudumia simu zake zichunguzwe. Pia iwe ni marufuku teller kuwa na simu awapo counter. Hizi counter ziwekewe tinted hata kwa mteja ili wateja wengine wasijue kiasi anachochukua yule aliyepo counter.



mkuu huyo jamaa ni mwenyeji wa mkoa gani.

Anatoka mkoa wa Mbeya
 
Back
Top Bottom