Mtoto Akataa shule; Bora aende jela

Wala siyo kweli. Nina mifano hai
Mwenyewe najuta muda mwingi niliopoteza shuleni ni bora ningeishia Form 4 nikaenda VETA.
Dunia imebadilika sana kwa sasa. Tumekaririshwa ukisoma ndiyo utakuwa na maisha mazuri. Hii ni dhana potofu
Kuna watu wamemaliza chuo kikuu (wana degree zao) lkn maisha yao yanasikitisha. Maisha ya sasa ili ufanikiwa lazima uwe na ujuzi wowote km vile ufundi magari, nyumba, seremala, kuendesha gari n.k
Km umemaliza kwenye ualimu, uanasheria n.k utajikuta unasota mtaani utakapokosa kazi.
Mpelekee VETA akajifunze fani za maisha na siyo kukariri vitabu.
Mbeleni atajutia maamuzi yake
 
Hapana mkuu. Faida ya elimu kwanza ni kujua kusoma na kuandika. Unaweza ukawa hujasoma ila ukabahatika kupata pesa za kutosha lakini hutazifaidi kwa dunia ya leo hata sms ya muamala ikiingia itabidi ukaombe msaada wa kusomewa ujue kilichomo. Hela zako zoote ila bank hutaweza shika kalamu kuandika cheki etc

Faida ya pili inakupa ka uelewa ka mambo na ujanja katika hizo harakati za kukariri

Sasa kwa kesi ya huyu mtoto hataki shule hapo huwezi jua kama anajua kusoma na kuandika huko veta si atawapa shida waalimu kuanza kumfundisha a e i o u

Elimu sio mpaka degree ila punguza chuki kwa wenye degree. Leo hii wanaobeza elimu na wakapata bahati ya kushika pesa nyingi wanawakazania watoto wao kusoma mpaka degree
Wala siyo kweli. Nina mifano hai
Mwenyewe najuta muda mwingi niliopoteza shuleni ni bora ningeishia Form 4 nikaenda VETA.
Dunia imebadilika sana kwa sasa. Tumekaririshwa ukisoma ndiyo utakuwa na maisha mazuri. Hii ni dhana potofu
Kuna watu wamemaliza chuo kikuu (wana degree zao) lkn maisha yao yanasikitisha. Maisha ya sasa ili ufanikiwa lazima uwe na ujuzi wowote km vile ufundi magari, nyumba, seremala, kuendesha gari n.k
Km umemaliza kwenye ualimu, uanasheria n.k utajikuta unasota mtaani utakapokosa kazi.
Mpelekee VETA akajifunze fani za maisha na siyo kukariri vitabu.
 
Wafrika tumejikuta kwenye duniani ya umasikini kwa kuamini haya mawazo. Vipaji vingi vinapotea shuleni kwa kuamini haya mawazo
Angalia elimu ya Messi, Diamond, Babu Tale, Zuchu
Niki wa pili pamoja na kuwa na Masters lkn anakula kupitia Muziki. Huyo mtoto anatakiwa akomaliwe asome mpk form 4 tu aende kwenye vyuo vya Ufundi.
Mm mwenyew pamoja na kuwa na elimu kubwa lkn nakula kupitia ujuzi nilionao ambao sijasomea chuo
Kweli kabisa siku akipiga kitabu akawa majaliwa ndio atakumbuka kauli yake.
 
Haja kanaweza kujiua kama watakalazimisha,waheshimu mawazo yake.

Maana elimu haina mwisho,kakija kushtuka baadae katarudi shule.
 
Mm mwenyewe nina degree lkn nakula kupitia ujuzi mwingine ambao sijasomea darasani ambapo ningeanza muda kbla sijaenda form 5 ningekuwa mbali sana.
Niwe na chuki na wenye degree wakati wapo mtaani wanafanya kazi mpaka za watu waliomaliza darasa la 7. Wapo wana wengi tu ninaowafahamu wanalia njaa na degree zao
Hapana mkuu. Faida ya elimu kwanza ni kujua kusoma na kuandika. Unaweza ukawa hujasoma ila ukabahatika kupata pesa za kutosha lakini hutazifaidi kwa dunia ya leo hata sms ya muamala ikiingia itabidi ukaombe msaada wa kusomewa ujue kilichomo. Hela zako zoote ila bank hutaweza shika kalamu kuandika cheki etc

Faida ya pili inakupa ka uelewa ka mambo na ujanja katika hizo harakati za kukariri

Sasa kwa kesi ya huyu mtoto hataki shule hapo huwezi jua kama anajua kusoma na kuandika huko veta si atawapa shida waalimu kuanza kumfundisha a e i o u

Elimu sio mpaka degree ila punguza chuki kwa wenye degree. Leo hii wanaobeza elimu na wakapata bahati ya kushika pesa nyingi wanawakazania watoto wao kusoma mpaka degree
 
Sijazungumzia mtoto kutoenda shule kbs. Ninachozungumzia mtoto afike mpaka form 4, hii ndiyo daraja la elimu ambalo kila mtanzania anatakiwa afike iwe kwa viboko au ngumi.
Mm mwanangu akifika form 4 au 6 lazima aende VETA kwanza hiyo ni lazima na siyo ombi
Hapana mkuu. Faida ya elimu kwanza ni kujua kusoma na kuandika. Unaweza ukawa hujasoma ila ukabahatika kupata pesa za kutosha lakini hutazifaidi kwa dunia ya leo hata sms ya muamala ikiingia itabidi ukaombe msaada wa kusomewa ujue kilichomo. Hela zako zoote ila bank hutaweza shika kalamu kuandika cheki etc

Faida ya pili inakupa ka uelewa ka mambo na ujanja katika hizo harakati za kukariri

Sasa kwa kesi ya huyu mtoto hataki shule hapo huwezi jua kama anajua kusoma na kuandika huko veta si atawapa shida waalimu kuanza kumfundisha a e i o u

Elimu sio mpaka degree ila punguza chuki kwa wenye degree. Leo hii wanaobeza elimu na wakapata bahati ya kushika pesa nyingi wanawakazania watoto wao kusoma mpaka degree
 
yuko sahihi, elimu siku hizi si ufunguo wa maisha na tena imegeuka na kuwa kufuli la maisha. mtu mwenye digrii hana ujuzi wowote wa kupambana na mazingira yake. zaidi zaidi elimu imemfungia afikirie kufanya vitu alivyosomea/kariri tu. sasa hapo si inakuwa kufuli la maisha?

dogo asisomeeee, achukue elimu ya kitaa.
 
Back
Top Bottom