Basi nielimishe ndugu yangu hii sera imeanza lini? Tanzania inajulikana kuwa na msimamo thabiti. Wakati Machel anapigana na Renamo tulimuunga mkono na hatukumhimiza azungumze naye. Wakati Obote/Museveni wakipambana na Iddi Amin hatukuwahimiza wazungumze naye. Hii sera imeanza lini?
Mzee Jasusi,
Hatujazungumza kitambo ndugu yangu. Imenilazim kuingilia kati kiduchu hii bayana yako,khasa baada ya kuona hayo maneno yakuwa ati
Tanzania tunajulikana kuwa na
msimamo thabit!?
...yawezekana ni kweli lakini sio kwenye hiyo mifano ya
Uganda uliyotoa hapo juu.
Binafsi siamini asilan,ati mfano wa kuwa na msimamo thabit ni kumuunga mkono tena kijeshi muuaji/haramia mmoja dhidi ya mwingine!?
Kwani wale wauaji,maharamia na matapeli akina
Obote na
Museveni unafikiri kweli walikua/wana tafauti kubwa sana na
Idd Amin!?
Nakhis
Idd Amin alikua sio favourite ya
Western mainsteam medias/empires anymore,khasa pale alipoanza mashirikiano yake ya kipumbavu na wale matapeli
Saud Royal Family na kujifanza against
Zionism.
Kwa kifupi baadhi ya vitu ambavyo hata Nyerere ilimlazim kukiri kimya kimya mara kadhaa,ni yale mauaji makubwa na ya kinyama alofanza
Obote na
Museveni na
gangs zao pale
Uganda. Nyerere alijua wazi
reputation na
credibility yake binafsi ilikua hatarini/matatani.
Wengi tunajua na kukubuka wazi jinsi
Nyerere alivyotumia mabavu,maarifa,fitna na kupoteza raslimali nyingi za
Tanzania kufanikisha kuwaweka tena madarakani wale muuaji
Obote na gangs zake,na tunajua kilichofuatia ni nini!?
"Bakhti nzuri" hizi khabar za unyama na ushenzi wao hasikiki mno, wala kuelezwa kwa kina sana kwenye
main stream medias...labda tu kwenye very few reputable
Human Rights Organisation/s!?
Niwie radhi ndugu yangu kama unakhis,labda nimenena lolote ambalo hukupendezwa nalo.
Ahsanta sana.