Hapana, hujaniudhi hata kiduchu. Huwa napenda kujadiliana na wewe.
Sasa tuanzie suala la Uganda na Idi Amin. Obote alipinduliwa akiwa kwenye mkutano wa Commonwealth Singapore ambako alikuwa kiongozi pekee kumuunga Nyerere mkono katika suala la Uingereza kuiuzia silaha Afrika kusini. Waingereza wangekuwa na uwezo wangempindua Nyerere lakini kwa sababu uwezo huo hawakuwa nao wakaona Obote ndiye weakest link. Nakumbuka waziri mkuu wa Uingereza wakati huo (jina linanitoka, labda unaweza nikumbushia, ilikuwa mwaka 1971) alisema pale kwenye kikao kuwa kuna baadhi yenu mnapaaza sauti hapa lakini hamtaweza kurudi nyumbani kwenu. Na kweli siku mbili baadaye Obote akapinduliwa. Hicho ndicho kisa kikubwa kilichomfanya Nyerere amchukie Amin (msimamo) Pili, Museveni wakati huo alikuwa mwanafunzi pale chuo kikuu cha UDSM (siyo muuaji) Na unakumbuka nchi ya kwanza kumkaribisha Amin ilikuwa Uingereza, mpaka pale alipowatimua Wahindi (1972 au 73) ndio waingereza wakamwona kuwa mtu wa hovyo. Hapo ndipo Amin alipopata marafiki wepya, Saudi Arabia na Libya. Sasa tukimlaumu Nyerere kwa mauaji yaliyotokea Uganda baada ya Museveni na Obote kurudi kwao, shurti pia tumlaumu basi kwa kumsaidia Mugabe kuingia mamlakani na kwa makosa ambayo Mugaba ameyafanya Zimbabwe. Is that fair?
Mzee Jasusi,
Nashukuru ndugu yangu,lakini imenilazim kucheka kiduchu.
Nakumbuka mara nyingi tunapojadiliana,explanations/excuses zako zinakua
triangular!?
Nafikiri mimi nilikua nakujibu tu kiduchu ile hoja yako ya awali yakuwa
Tanzania tunasifika kwa kuwa na
msimamo thabit...ndipo ikanilazim kiduchu nigusie mfano wa
Uganda kama ulivofanza wewe.
Kumbuka
Nyerere alipinga kabisa na wala alikua hataki asilan kusikiza
washauri wake binafsi wa karibu au
Usalama wa Taifa ilipokua kuhusu khabar za
Obote...sasa kwanini alikua akifanza vile!?
Matokeo yake; yale yoote washauri wake au hata
Usalama waliyokua wakimkataza au kumshauri...ndio yale yale yaliyotokea wakti
Obote aliporejea madarakani na alipokhis yakuwa nae muda wake wa kulipiza kisasi umefika!?
Kuhusu
Museveni,wewe binafsi unajua yakuwa yule jamaa tayari aliaanza kuwa mtu mbaya na ana mipango mingi mno ya
kinyama,tangia yuko pale
UDSM.
Nakumbuka mara kadhaa kukutana nae kwenye ile ilokua mikutano ya
MWAKENYA pale
UDSM.
Nyendo zake zoote mbovu,
Nyerere pia alifahamishwa na Usalama na washauri wake wa karibu, nafikiri mwanzoni hakutaka asilan kusikiza.
Kile kile kipindi alichoamuru hatimae
Museveni afukuzwe nafikri ilikua tu ni kwasasabu ya fitna za
Obote...na pia tunajua yakuwa
Obote ndie aliekua
favourite kwa
Nyerere.
Hizo khabar za
Mugabe,Nkomo na Zimbabwe...nafikiri mimi nawe tulishazijadili kwa utuvu.
Nafikiri unakumbuka msimamo wangu!?ahaha!!
Nachelea tusijerejea kule kule tutokeako!?
Kwa kifupi huu mjadala kwangu mimi binafsi ni mzuri mno,kuna kuna vitu vingi mno nachungulia na kujifunza upya.
Nisingependa kuchangia kwa kina,kwa wakti huu. Nakhis ni wakti muafaka kuwaachia
wataalamu wengine nami niwasikize maoni yao.
Natanguliza shukran zangu za dhati pia kwa ndugu yetu
JokaKuu kwa kunalika kwenye jamvi hili pia.
Ahsanta sana.
Cc;JokaKuu.