Hivi udini ni upi kati ya kuteua watu wengi wa dini moja na kusema kuwa walioteuliwa wengi ni watu wa dini moja?
Nasubiri jibu hapa, otherwise nitauliza hili swali over and over again hadi nipate jibu.
Mkuu jmushi1, heshima yako!!
Assume mtu ameteua watu 20, na wote hao ni wa dini moja lakini wakati unafanya uteuzi huo hukusukumwa japo na chembe ndogo kwamba unafanya hivyo ili kuwapendelea hao wenye dini husika...then, katu huo sio udini!!
Kinyume chake. Assume wewe ni Mwislamu unayeishi huku bara na umepewa jukumu la kuteua hao wajumbe 20! Lakini Kila ukipitia mafali, unashindwa kabisa kupata waisalmu wenye sifa wa kumwemo kwenye tume! Unaona haiwezekani, unatumia extra energy...unaanza hata kuulizia watu unaowafamu kama kuna waislamu wenye hizo sifa....hatimae unapata 3 out of 20! Hata kama waislamu hao ni wachache, huo ni udini UNLESS kama sheria ilikuwa inatakamka kwamba lazima wawakilishi wa dini zote mbili wawepo!
Kusema kuwa walioteuliwa wengi ni watu wa dini moja hakuna justification! Purely, huo ni udini! Binafsi, ilipotolewa orodha ile...niliangalia idadi kila upande. Nikakuta ZNZ ni 15 na Bara ni 15! Kiukweli nilishngaa kwavile sikuona mantiki ya kuwa na watu sawa kila upande wakati ZNZ ni wachache! Lakini baada ya kufikiria sana, nikahisi labda wakati mwingine watakuwa wanashindwa kukubaliana mambo fulani fulani yatakayowalazimisha kupata muafaka kwa kupiga kura! Nika-conclude kwamba, endapo scenario ya aina hiyo inaweza kutokea basi ni busara kuwa na idadi sawa ili pasije pakatokea kura za ubara na uzanzibari!
Lakini unapofikia kusema kwamba dini fulani ni wengi, ni kwamba si tu ulihesabu....bali ulikuwa unahesabu huku ukisema "Mkristo!", "Mkristo!", "Mkristo!", "Mwislamu", "Mwislamu","Mkristo!",.............!" Sasa hadi unafika kote huko, unatafuta nini?! Huo ni purely udini!!