Mbona unataka kuturudisha nyuma? Yalishajadiliwa nayo humu.Haya ya Mtei Vs Nyerere tumeyasikia...kuna anayefahamu zengwe la Kambona Vs Nyerere atupashe?
Bubu Ataka Kusema,
..naomba usome kitabu cha Mzee Mtei ili ujue nini kilitokea kuhusu kushusha thamani ya shilingi.
..vilevile mapendekezo ya Mtei na timu yake hayakuhusu kushusha thamani ya shilingi ya Tanzania peke yake, yalihusu masuala mengi ya jinsi ya kujikwamua na matatizo ya uchumi wakati ule.
..binafsi nadhani Mwalimu angekuwa mkweli ktk kutufafanulia Watanzania kwamba kwa kiasi kikubwa tunahusika na kuporomoka kwa uchumi wetu, leo hii tusingekuwa tunabishana kiasi hiki.
..pia lazima tuelewe kwamba IMF na WB walianza kutuingilia ktk kufanya maamuzi baada ya kuchukua mikopo toka kwao na kushindwa kuonyesha tumefanyia nini mikopo hiyo.
NB:
..kuna mtu amegusia kuhusu Mtei kupendekeza NMC irudishwe kwa familia ya kina Chande.
..katika hili itakuwa vizuri kama tutaelewa kwamba familia ya kina Chande walikuwa wamiliki wa NMC kabla haijataifishwa. vilevile Mwalimu alimteua Chande kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya NMC hata baada ya kuitafisha.
..kuna wataalamu toka Sweden walioletwa kufanya uchunguzi kuhusu biashara na uendeshaji wa NMC. timu hiyo ya wataalamu iligundua matatizo makubwa ikiwemo HUJUMA NA UZEMBE WA WATUMISHI WAZALENDO. moja ya mapendekezo yao ilikuwa ni muundo wa shirika la NMC pamoja na umiliki wake.
Mwanafalsafa,Nyerere was by no means perfect. So it is very surprising when people jump on to every mistake Nyerere did as if the man was expected to make no mistakes. I admire Mwl Nyerere very much and I appreciate him for all the good that he has done for our country. I for one am not a fan of Azimio la Arusha and consider it one of his biggest mistakes. abut despite his mistakes when leading the country what matters most is his motives for what he did. If he did what he thought was best for the country then he can be forgiven in my book. Those others things about his personality like him being arrogant, stubborn or whatever.......well.......no one has a perfect personality.
I think the best way to remember Mwl Nyerere is not to pretend that he had no fault neither is it to try to blame him for every single problem this country is facing. History is already written down. If he can not follow him by his examples we can at least learn from his mistakes. People, Nyerere wasn't perfect, but looking at other leaders in Africa around his time I say we should be thankful Tanzania didn't end up with the likes of Mengistu, Mobutu, Iddi Amin and other such characters.
Rest in peace Nyerere.
, je watu tulilielewa vipi na wale waliokuwa viongozi walielewa vipi kauli kama hizi?
Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi: hainaikapanuka na kuenea.
ubepari wala ukabaila. Haina tabaka mbili za watu: tabaka ya
chini ya watu wanaoishi kwa kufanya kazi, na tabaka ya juu ya
watu wanaoishi kwa kufanyiwa kazi. Katika nchi ya Ujamaa
kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye kufanya kazi
hufanya kazi, na kila mfanya kazi hupata pato la haki kwa kazi
aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbali mbali
hayapitani mno.
Katika nchi ya Ujamaa kamili watu peke yao ambao huishi
kwa jasho la wenzao, na ni haki yao kuishi kwa jasho la wenzao
ni watoto wadogo, wazee wasiojiweza, vilema na wale ambao,
kwa muda, Jumuiya imeshindwa kuwapatia kazi yo yote ya
kujipatia riziki kwa nguvu zao wenyewe.
Nchi yetu ni nchi ya Wakulima na Wafanya kazi, lakini si nchi ya
Ujamaa kamili. Ina misingi ya ubepari na ukabaila na
vishawishi vyake. Misingi hii ya ubepari na ukabaila yaweza
Mnyonge hapigani kwa Fedha:Lakini ni dhahiri kwamba tumefanya makosa katika kuchaguamaendeleo. Bila fedha hakuna maendeleo!
silaha; kwani silaha tuliyochagua ni fedha. Tunataka kuondoa
unyonge wetu kwa kutumia silaha ya wenye nguvu, silaha ambayo
sisi wenyewe hatuna. Katika mazungumzo yetu, mawazo yetu, na
vitendo vyetu ni kama tumekata shauri kwamba bila fedha mapinduzi
yetu hayawezekani. Ni kama tumesema, Fedha ndiyo msingi wa
Hii ndiyo imani yetu ya sasa. Viongozi wa TANU mawazo yao ni
kwenye fedha. Viongozi wa Serikali, wanasiasa na watumishi,
mawazo yao na matumaini yao ni kwenye fedha. Viongozi wa
wananchi na wananchi wenyewe katika TANU, NUTA, Bunge, UWT.,
Vyama vya Ushirika, TAPA na makundi mengine ya wananchi,
mawazo yao na maombi yao na matumaini yao ni FEDHA. Ni kama
wote tumekubaliana na tunasema kwa sauti moja, Tukipata fedha
tutaendelea, bila fedha hatutaendea!
Na kusema kuwa Serikali haina fedha maana yake ni nini?kuzipata ni kodi. Kudai Serikali itumie fedha nyingi bila kukubali kodi
Maana yake ni kuwa Wananchi wa Tanzania hawana fedha. Kiasi
walichonacho hutozwa kodi, na kodi hiyo ndiyo inayoendesha
shughuli za Serikali hivi sasa na maendeleo mengine ya nchi.
Tunapotaka Serikali ifanye shughuli zaidi za maendeleo kwa fedha
tunataka Serikali itumie fedha zaidi. Na kama Serikali haina fedha
zaidi tunataka izipate, yaani iongeze kodi.
Ukidai Serikali itumie fedha zaidi unataka izipate; na njia ya
zaidi ni kudai Serikali ifanye miujiza; ni sawa na kudai maziwa zaidizaidi.
bila kutaka Ngombe akamuliwe tena. Lakini kukataa huku kukiri
kwamba tunapodai Serikali itumie fedha zaidi nia yetu ni kutaka
Serikali iongeze kodi kunaonyesha kuwa tunatambua ugumu wa
kuongeza kodi. Tunatambua kuwa ngombe hana maziwa zaidi;
kwamba hata ngombe mwenyewe angependa ayanywe maziwa hayo
au yanywewe na ndama wake au yauzwe yamfae yeye na jamaa
yake; utashi huo hauwezi kuondoa ukweli kwamba hana maziwa
Fedha kutoka nje ya Tanzania, Je?Njia moja tunayotumia kujaribu kuepukana na lazima hii ya kukiri
kodi zaidi ikiwa twataka fedha zaidi ni kutilia sana mkazo fedha za
kutoka nje ya Tanzania. Fedha hizi za kutoka nje ni za aina tatu:-
(a) Zawadi: Yaani Serikali ya nje iipe Serikali yetu fedha za bure
tu kama sadaka kwa ajili ya mpango fulani wa maendeleo.
Wakati mwingine shirika lo lote la nje liipe Serikali yetu au
Shirika jingine katika nchi yetu msaada fulani kwa ajili ya
maendeleo.
(b) Mkopo: Sehemu kubwa ya fedha tunazotazamia kupata
kutoka nchi za kigeni si zawadi au sadaka, bali ni mkopo.
Serikali ya nje au Shirika la nje, kama vile Benki, hukopesha
Serikali yetu fedha fulani kwa ajili ya kazi zetu za
maendeleo. Mkopo huu huwa una masharti yake ya kulipa,
kama vile muda wa kulipa, na kima cha faida.
(c) Raslimali ya Kibiashara: Aina ya tatu ambayo pia ni kubwa
kuliko ya kwanza, ni ile ya fedha za watu au makampuni
yanayotaka kuja katika nchi yetu kuanzisha shughuli mbali
mbali za uchumi kwa manufaa yao wenyewe. Na sharti
kubwa walitakalo jamaa hawa wenye fedha zao ni kwamba
shughuli yenyewe iwe ni ya faida kwao na pia kwamba
Serikali iwaruhusu kuondoa faida hiyo Tanzania na kuipeleka
kwao. Hupenda pia kwa jumla Serikali iwe na siasa
wanayokubaliana nayo au ambayo haihatarishi uchumi wao.
Hizo ndizo njia tatu kubwa za kupata fedha kutoka nje ya
nchi yetu. Kuna mazungumzo mengi ajabu juu ya jambo hili
la kupata fedha kutoka nchi za kigeni. Serikali yetu na
viongozi wetu wa makundi mbalimbali hawaachi kufikiria njia
za kupata fedha kutoka nje. Na tukizipata au japo tukipata
ahadi tu ya kuzipata mara magazeti yetu, au radio zetu na
viongozi wetu hutangaza jambo hilo ili kila mtu ajue kuwa
neema imekuja au iko njiani inakuja. Tukipata msaada
hutangaza; tukipata mkopo hutangaza; tukipata kiwanda
kipya hutangaza; tukiahidiwa msaada, mkopo au kiwanda
kipya hutangaza. Japo tukianza mazungumzo tu na nchi au
shirika la kigeni juu ya msaada, mkopo au kiwanda, maramazungumzo ya neema!
hutangaza japo hatuna hakika ya matokeo ya mazungumzo
hayo. Na kisa? Ni kuwajulisha wananchi kwamba, tunaanza
TUSITEGEMEE FEDHA KULETA MAENDELEOkodi wakipenda wasipende. Hata hivyo huwa hazitoshi. Ndiyo
Ni jambo la kijinga kuchagua fedha kuwa ndiyo chombo chetu
kikubwa cha maendeleo na hali tunajua kuwa nchi yetu ni maskini.
Ni ujinga vile vile, kwa kweli ni ujinga zaidi, tukidhani kuwa tunaweza
kuondoa hali hii ya unyonge wetu kwa kutegemea fedha za kutoka
nje badala ya fedha zetu wenyewe. Ni ujinga kwa sababu mbili.
Kwanza, hatuwezi kuzipata. Ni kweli kwamba zipo nchi ambazo
zaweza na zapenda kutusaidia. Lakini hakuna nchi moja duniani
ambayo iko tayari kutupa misaada au mikopo au kuja kujenga
viwanda katika nchi yetu kutimiza shabaha zake zote za maendeleo.
Nchi zenye dhiki ni nyingi sana duniani. Na hata kama nchi zote
zenye neema zingekubali kuzisaidia nchi zenye dhiki, bado ingekuwa
msaada huo hautoshi. Lakini nchi zenye neema hazitakubali. Hata
katika nchi ile ile, matajiri huwa hawatoi fedha zao kwa hiari ili
zisaidie Serikali kuondoa dhiki.
Njia ya kuzipata fedha za matajiri ili zisaidie umma ni kuwatoza
maana japo tungewakamua vipi wnanachi na wakazi wa Tanzania,Haiwezekani basi, tupate fedha za ktuosha kwa njia hiyo.
matajiri na maskini, hatuwezi kupata fedha za kutosha kutimiza
mipango yetu ya maendeleo. Wala duniani hakuna Serikali ambayo
yaweza kuyatoza kodi mataifa yenye neema, yakipenda yasipende, ili
kusaidia mataifa yenye dhiki. Hata hizo zisingelitosha. Hakuna
Serikali ya Dunia nzima. Fedha ambazo nchi zenye neema hutoa
huwa kwa wema wao, au hiari yao au kwa manufaa yao wenyewe.
MISAADA NA MIKOPOnyenzo ya juhudi, ni msaada ambao una manufaa. Lakini msaada
VITAHATARISHA UHURU WETU
Pili, japo kama tungeweza kuzipata; hivyo ndivyo tunavyotaka
kweli? Kujitawala ni kujitegemea. Kujitawala kwa kweli
hakuwezekani ikiwa Taifa moja linategemea misaada na mikopo ya
Taifa jingine kwa maendeleo yake. Hata kama pangetokea Taifa au
mataifa ambayo yako tayari kutupa fedha zote tunazohitaji
kuendesha mipango yetu ya maendeleo isingekuwa sawa kwa nchi
yetu kuipokea misaada hiyo bila kujiuliza matokeo yake yatakuwa nini
kwa Uhuru wetu na uzima wetu.
Msaada ambao ni kama chombo cha kuongeza juhudi, au
unaoweza ukawa sumu ya juhudi si msaada wa kupokea bila kujiuliza
maswali.
Kadhalika mikopo. Kweli mkopo ni bora kuliko misaada ya
bure. Mkopo nia yake ni kuongeza jitihada au kuifanya jitihada
itoe matunda mengi zaidi. Sharti moja la mkopo huwa ni kuonyesha
jinsi utavyoweza kuulipa. Maana yake ni kwamba sharti uonyeshe
kuwa unakusudia kuufanyia kazi itakayoleta manufaa ya
kukuwezesha kuulipa.
Lakini hata mikopo ina kikomo. Sharti upime uwezo wa kulipa.
Tunapokopa fedha kutoka nje mlipaji ni Mtanzania. Na kama
tulivyokwisha sema Watanzania ni watu maskini. Kuwabebesha watu
maskini mikopo ambayo inawazidi kimo si kuwasaidia bali ni
kuwaumiza. Na hasa inapokuwa, mikopo hiyo ambayo wanatakiwa
walipe haikuwafaidia wao, bali ilifaidia watu wachache tu.Na Viwanda vya wenye raslimali zao je? Ni kweli tunavitaka.
Hata tumepitisha katika Bunge sheria ya kulinda raslimali ya wageni
wanaoanzisha mipango mbali mbali ya uchumi katika nchi yetu. Nia
yetu na matumaini yetu ni kuwafanya waone kuwa Tanzania ni nchi
inayofaa kuingiza raslimali zao. Kwani raslimali yao itakuwa salama
italeta faida. Na faida hiyo wenyewe wataweza kuiondoa bila
vipangimizi. Tunayo matumaini ya kupata fedha za maendeleo mbali
mbali kwa njia hii. Lakini hatuwezi kupata za kutosha. Lakini hata
kama tungeweza kuwaridhika kabisa Wageni hao na Makampuniambacho hatuna, kiwe ndicho chombo kikubwa cha mipango yetu ya
hayo mpaka yakubali kuanzisha mipango yote ya uchumi tunayohitaji
katika nchi yetu, hivyo ndivyo tunavyotaka kweli?
Kama tungeweza kushawishi wenye raslimai wa kutosha kutoka
Amerika, na Ulaya kuja kwetu na kuanzisha Viwanda vyote, na
mipango mingine yote ya uchumi tunayohitaji katika nchi hii, hivi
kweli tungekubali bila kujiuliza maswali? Tungekubali kweli kuacha
uchumi wetu wote uwe mikononi mwa wageni kwa ajili ya kupata
faida na kuipeleka katika nchi zao? Hata kama wasingedai
kuhamisha faida na kupeleka makwao, bali faida yote watakayopata
wataitumia hapa hapa Tanzania kwa maendeleo zaidi. Hivi kweli
tungekubali jambo hili bila kujiuliza hasara zake kwa Taifa letu? Huu
Ujamaa tunaosema kuwa ndiyo shabaha yetu tungeujengaje?
Twawezaje kutegemea nchi za nje na Kampuni za nje kwa
misaada na mikopo na raslimali kwa maendeleo yetu bila kuhatarisha
uhuru wetu? Waingereza wana methali isimayo Amlipaye mwimbaji
ndiye huchagua wimbo. Tutawezaje kutegemea nchi za kigeni na
Makampuni ya kigeni kwa sehemu kubwa ya maendeleo yetu bila
kuzipa nchi hizo na makampuni hayo sehemu kubwa ya uhuru wetu
wa kutenda tupendavyo. Ukweli wenyewe ni kwamba hatuwezi.
Tukariri basi. Tumefanya makosa kuchagua fedha, kitu
maendeleo. Tunafanya makosa kudhani kuwa tutapata fedha kutokasiasa nyingine za nchi yetu.
nchi za kigeni. Kwanza, kwa sababu kwa kweli hatuwezi kupata
fedha za kutosha kwa maendeleo yetu. Na pili, hata kama
tungeweza, huko kutegemea wengine kungehatarisha uhuru wetu na
Natamani Mwalimu angekuwa bado yuko hai ili naye atueleze ni kipi hasa kilichojiri hadi kuhitilafiana na Mtei. Kila jambo lina pande mbili, labda wale waliokuwa karibu na Mwalimu miaka hiyo ilipotokea hitilafu kati ya Mwalimu na Mtei labda watajitokeza na wao kuzungumza ufahamu wao wa nini hasa kililichotokea hadi kusababisha Mtei kujiuzulu. Mwalimu tulimuita majina mengi sana kama Mzee haambiliki, mchonga meno, Mussa n.k. lakini kwa mano yangu pamoja na kuwa hakuwa perfect kama kiongozi alifanikiwa katika mambo mengi kama Kiongozi wa Tanzania ukilinganisha na mafanikio yaliyopatikana kwa ujumla wakati wa Mwinyi, Mkapa na Kikwete.
Asante mkuu Mkandara kwa kufafanua baadhi ya myth za Ujamaa na Azimio la Arusha. Kama nilivyo sema awali sikuwepo wakati huo kwa hiyo kila kitu ninacho jua kuhusiana na swala hilo ni kujifunza mwenyewe na kusikia kwa watu.
Mkuu you raise a very interesting topic unaposema "WATU na MAZINGIRA". Ni kweli kwamba kila nchi ina resources zake na hata ndani ya nchi kila eneo lina resources zake.
Sasa je mkuu unadhani Ujamaa ulitufaa sisi na mazingira yetu. Kwa maana je Azimio la Arusha liliweka policies tailor made for us au zilikua ni policies zilizo azimwa? Maana I'm under the impression kwamba hata hilo Azimio la Arusha ni policies za sehemu zingine na watu wengine ambalo lilipewa tu jina la kiswahili. Kwa sababu mimi nadhani kama kweli Azimio la Arusha liliaddress sisi kama sisi na matatizo yet unique basi linge fanikiwa. Sasa je tatizo lilikua policies zilizo azimwa au kwenye implementation ya hizo sera?
Swala la pili. Tanzania tume jaliwa rasilimali nyingi. Kila mkoa tuseme una rasilimali zake. Je hizi rasilimali za kila mkoa zitumike kwa manufaa ya nchi nzima au tuendeleze mkoa mmoja mmoja kutokana na rasilimali zake? Mimi nafikiri kwa mazingira yetu federal system ingetufaa sana. Kwa maana kila mkoa uendelezwe kutokana na rasilimali zake badala ya tunavyo fanya sasa ambapo rasilimali za kila mkoa zina tumika kama mali ya taifa zima ila hatuoni hiyo mikoa wala taifa lenyewe liki nufaika na rasilimali hizo.
Socrates,
Msukuma alikuwa ni mwindaji, mfugaji na akijilimia vitu vichache. Katika mfumo wake wa Kijima ambao Mzungu alisema ni wa KIS HE NZI, Msukuma aliweza kujitosheleza yeye na familia yake, alifanya kazi kwa kushirikiana na wenzake, walitoa Zaka kwa Mungu wao Manumbu na walimpa Mtemi wao yale mazao yaliyo bora.
Masalio waligawanyana katika nyumba na koo, na kisha wakaenda Ukuriani, Unyirambani na kubadilishana bidhaa na Wahaya, Wanyamwezi na Waha.
Huu mfumo ulikuwa na tatizo gani kuendelezwa na kuboresha na badala yake tukasokomezewa mfumo mpya kabisa wa Kizungu huku tukidharauliwa na kuambiwa Historia na Utamaduni wetu ni wa kijinga?
Hata kama leo Dhahabu ziko Mwanza, Uranium iko Singida, Alizeti iko Kilimanjaro, je kwa nini tuachane na jadi letu la kushirikiana na kubadilishana bidhaa kisa eti mikoa ijitosheleze ka Ubinafsi?
Kwa nini leo Mkandara ambaye ni Mkerewe, atakwenda Usukumani kwa Nyani Julius na kumsaidia kuzika pamoja na kuwa wanaitana Watani?
Haya ndio maswali ya kuwauliza hao wanao tuongoza!So basically mkuu the system I was proposing ilikuwepo kabla ya ukoloni. Kwamba kila eneo ilitumia rasilimali zake kuji tosheleza. That's what I'm advocating. Kwa nini sasa tusi boreshe huo mfumo tulio kuwa nao na kuufanya ulingane na hali halisi ya leo?(kwa maana leo hii kumuambia mtu arudi kwao akawinde itakua ngumu). Maana siku hizi karibia kila mtu anaona kukimbilia Dar Es Salaam ndipo paku patia mafanikio. Let's promote the different industries which are allowed by our resources the excess of which will flow to other parts of the country.
Ukiweka mfumo mzuri hata ubinafsi unaweza kunufaisha taifa zima. Kwa mfano kwamba hata tajiri akiwa na tamaa ya kutajirika zaidi ni lazima kodi yake itaongezeka kwa jinsi anavyo tajirika na hapo ata nufaisha taifa zima.
So basically mkuu the system I was proposing ilikuwepo kabla ya ukoloni. Kwamba kila eneo ilitumia rasilimali zake kuji tosheleza. That's what I'm advocating. Kwa nini sasa tusi boreshe huo mfumo tulio kuwa nao na kuufanya ulingane na hali halisi ya leo? (kwa maana leo hii kumuambia mtu arudi kwao akawinde itakua ngumu). Maana siku hizi karibia kila mtu anaona kukimbilia Dar Es Salaam ndipo paku patia mafanikio. Let's promote the different industries which are allowed by our resources the excess of which will flow to other parts of the country.
Ukiweka mfumo mzuri hata ubinafsi unaweza kunufaisha taifa zima. Kwa mfano kwamba hata tajiri akiwa na tamaa ya kutajirika zaidi ni lazima kodi yake itaongezeka kwa jinsi anavyo tajirika na hapo ata nufaisha taifa zima.